< 2 Samweli 21 >

1 Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
I za czasów Dawida panował głód przez trzy lata, rok po roku. Dawid szukał więc oblicza PANA, a PAN odpowiedział: To z powodu Saula i jego krwawego domu, ponieważ wymordował Gibeonitów.
2 Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
Wtedy król wezwał Gibeonitów i przemówił do nich. A Gibeonici nie wywodzili się z synów Izraela, ale z resztki Amorytów. I chociaż synowie Izraela przysięgli im, Saul jednak usiłował wytępić ich w swej gorliwości względem synów Izraela i Judy.
3 Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
Dawid zapytał więc Gibeonitów: Cóż mam dla was uczynić? A czym was ułagodzić, abyście błogosławili dziedzictwo PANA?
4 Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
I odpowiedzieli mu Gibeonici: Nie chodzi nam o srebro ani o złoto od Saula i jego domu, ani o to, żeby zabito kogoś w Izraelu. A [on] odpowiedział: Cokolwiek powiecie, to dla was uczynię.
5 Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
Oni powiedzieli do króla: [Co do] mężczyzny, który nas wygubił i zmierzał do tego, aby nas wytępić, żeby nikt z nas nie pozostał we wszystkich granicach Izraela;
6 tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
Wydajcie nam siedmiu z jego synów, a my powiesimy ich przed PANEM w Gibea Saula, [który był] wybrańcem PANA. Król odpowiedział: Wydam [ich].
7 Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
Lecz król oszczędził Mefiboszeta, syna Jonatana, syna Saula, z powodu przysięgi PANA, która [była] między nimi, między Dawidem a Jonatanem, synem Saula.
8 Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
Ale król wziął dwóch synów Rispy, córki Aji, których urodziła Saulowi, Armoniego i Mefiboszeta, i pięciu synów [siostry] Mikal, córki Saula, których urodziła Adrielowi, synowi Barzillaja z Mecholi;
9 Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
I wydał ich w ręce Gibeonitów, a oni powiesili ich na górze przed PANEM. Razem umarło ich siedmiu, zostali zabici w pierwsze dni żniw, na początku żniw jęczmienia.
10 Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
Wtedy Rispa, córka Aji, wzięła wór i rozciągnęła go na skale, na początku żniw, aż do czasu, gdy spadł na nich deszcz z nieba, i nie pozwalała, aby ptactwo powietrzne zbliżało się do nich za dnia, ani zwierzęta polne – nocą.
11 Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
Potem doniesiono Dawidowi o tym, co uczyniła Rispa, córka Aji, nałożnica Saula.
12 alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
Dawid poszedł więc i wziął kości Saula i kości Jonatana, jego syna, od starszych Jabesz-Gilead, którzy ukradli je z placu Bet-Szan, gdzie ich zawiesili Filistyni w dniu zabicia Saula przez Filistynów w Gilboa.
13 Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
Wziął więc stamtąd kości Saula i kości Jonatana, jego syna; zebrano też kości powieszonych;
14 Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
I pogrzebali kości Saula i Jonatana, jego syna, w ziemi Beniamina w Sela, w grobie Kisza, jego ojca. Uczynili wszystko, co król nakazał. Potem Bóg dał się ubłagać co do ziemi.
15 Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
Później znowu doszło do wojny między Filistynami a Izraelem. I Dawid wyruszył wraz ze swymi sługami i walczyli z Filistynami, a Dawid był znużony.
16 Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
Wtedy Iszbibenob, który wywodził się z synów pewnego olbrzyma, a którego włócznia ważyła trzysta syklów brązu i który miał przepasany nowy [miecz], postanowił, że zabije Dawida.
17 Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
Lecz Abiszaj, syn Serui, przyszedł mu z pomocą, uderzył Filistyna i zabił go. Wtedy ludzie Dawida przysięgli mu: Nie będziesz już wyruszał z nami do bitwy, abyś nie zgasił pochodni Izraela.
18 Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
Potem znowu była bitwa z Filistynami w Gob. Wtedy Sibbekaj Chuszatyta zabił Safa, który pochodził z synów tego olbrzyma.
19 Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Była też jeszcze inna wojna z Filistynami w Gob, podczas której Elchanan, syn Jaara Oregima z Betlejem, zabił [brata] Goliata Gittyty, którego drzewce włóczni były jak wał tkacki.
20 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
Ponadto toczyła się jeszcze wojna w Gat, gdzie był człowiek [wysokiego] wzrostu, mający po sześć palców u rąk i po sześć palców u nóg, razem dwadzieścia cztery. On także był synem tego olbrzyma.
21 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
Gdy urągał on Izraelowi, zabił go Jonatan, syn Szimei, brata Dawida.
22 Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
Ci czterej byli synami [tego] olbrzyma z Gat, a polegli z ręki Dawida i z ręki jego sług.

< 2 Samweli 21 >