< 2 Wafalme 25 >

1 Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli, akiwa na jeshi lake lote, alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Akapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote.
It happened that in the ninth year of the reign of King Zedekiah, in the tenth month, and on the tenth day of the month, Nebuchadnezzar king of Babylon came with all his army against Jerusalem. He camped opposite it, and they built a siege wall around it.
2 Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.
So the city was besieged until the eleventh year of King Zedekiah's reign.
3 Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu.
On the ninth day of the fourth month of that year, the famine was so severe in the city that there was no food for the people of the land.
4 Kisha ukuta wa mji ukavunjwa, na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba.
Then the city was broken into, and all the fighting men fled at night by the way of the gate between the two walls, by the king's garden, although the Chaldeans were all around the city. The king went in the direction of the Arabah.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia mfalme na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika,
But the army of Chaldeans pursued King Zedekiah and overtook him in the plains of the Jordan River valley near Jericho. All his army was scattered away from him.
6 naye akakamatwa. Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, mahali ambapo hukumu yake ilitangazwa.
They captured the king and brought him up to the king of Babylon at Riblah, where they passed sentence on him.
7 Wakawaua wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Kisha wakayangʼoa macho yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
As for Zedekiah's sons, they slaughtered them before his eyes. Then he put out his eyes, bound him in bronze chains, and brought him to Babylon.
8 Mnamo siku ya saba ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, afisa wa mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu.
Now in the fifth month, on the seventh day of the month, which was the nineteenth year of the reign of Nebuchadnezzar king of Babylon, Nebuzaradan, a servant of the king of Babylon and commander of his bodyguards, came to Jerusalem.
9 Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu.
He burned the house of Yahweh, the king's palace, and all the houses of Jerusalem; also every important building in the city he burned.
10 Jeshi lote la Wakaldayo, chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme, walivunja kuta zilizoizunguka Yerusalemu.
As for all the walls around Jerusalem, all the army of the Babylonians who were under the commander of the bodyguard destroyed them.
11 Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi akawapeleka uhamishoni watu waliokuwa wamebaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli.
As for the rest of the people who were left in the city, those who had deserted to the king of Babylon, and the remainder of the population—Nebuzaradan, the commander of the bodyguard, took them away into exile.
12 Lakini yule jemadari wa askari walinzi akawaacha baadhi ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
But the commander of the bodyguard did leave some of the poorest of the land to work the vineyards and fields.
13 Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba na kuipeleka Babeli.
As for the bronze pillars that were in the house of Yahweh, and the stands and the bronze sea that were in the house of Yahweh, the Chaldeans broke them into pieces and carried the bronze back to Babylon.
14 Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu.
The pots, shovels, lamp trimmers, spoons, and all the utensils of bronze with which the priests had served in the temple—the Chaldeans took them all away.
15 Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua vile vyetezo na yale mabakuli ya kunyunyizia, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.
The pots for removing ashes and the bowls that were made of gold, and those made of silver—the captain of the king's guard took them away as well.
16 Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika.
The two pillars, the sea, and the stands that Solomon had made for the house of Yahweh contained more bronze than could be weighed.
17 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane. Sehemu ya shaba juu ya nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tatu na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na wavu wake ilifanana na hiyo ya kwanza.
The height of the first pillar was eighteen cubits, and a capital of bronze was on top of it. The capital was three cubits high, with latticework and pomegranates all around on the capital, all made of bronze. The other pillar and its latticework were the same as the first.
18 Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu.
The commander of the bodyguard took Seraiah the chief priest, together with Zephaniah, the second priest, and the three gatekeepers.
19 Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri watano wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji.
From the city he took prisoner an officer who was in charge of soldiers, and five men of those who advised the king, who were still in the city. He also took prisoner the king's army officer responsible for drafting men into the army, along with sixty important men from the land who were in the city.
20 Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla.
Then Nebuzaradan, the commander of the bodyguard, took them and brought them to the king of Babylon at Riblah.
21 Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe. Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao.
The king of Babylon put them to death at Riblah in the land of Hamath. In this way, Judah went out of its land into exile.
22 Nebukadneza mfalme wa Babeli akamteua Gedalia mwana wa Ahikamu, mwana wa Shafani, awe msimamizi wa watu aliowaacha Yuda.
As for the people who remained in the land of Judah, those whom Nebuchadnezzar king of Babylon had left, he put Gedaliah son of Ahikam, son of Shaphan, in charge of them.
23 Maafisa wote wa jeshi na watu wao waliposikia kwamba mfalme wa Babeli amemteua Gedalia kuwa mtawala, wakamjia Gedalia huko Mispa. Hawa walikuwa Ishmaeli mwana wa Nethania, Yohanani mwana wa Karea, Seraya mwana wa Tanhumethi Mnetofathi, na Yezania mwana wa Mmaaka, pamoja na watu wao.
Now when all the commanders of the soldiers, they and their men, heard that the king of Babylon had made Gedaliah governor, they went to Gedaliah at Mizpah. These men were Ishmael son of Nethaniah, Johanan son of Kareah, Seraiah son of Tanhumeth the Netophathite, and Jaazaniah son of the Maakathite—they and their men.
24 Gedalia akaapa ili kuwatia moyo wao na watu wao. Akasema, “Msiwaogope maafisa wa Kikaldayo. Kaeni katika nchi na kumtumikia mfalme wa Babeli, na itakuwa vyema kwenu.”
Gedaliah made an oath to them and to their men, and said to them, “Do not be afraid of the Chaldean officials. Live in the land and serve the king of Babylon, and it will go well with you.”
25 Hata hivyo, katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi, nao wakamuua Gedalia, na pia watu wa Yuda, pamoja na Wakaldayo waliokuwa naye huko Mispa.
But it happened that in the seventh month Ishmael son of Nethaniah son of Elishama, from the royal family, came with ten men and attacked Gedaliah. Gedaliah died, along with the men of Judah and the Babylonians who were with him at Mizpah.
26 Baada ya haya, watu wote kuanzia aliye mdogo sana hadi aliye mkubwa kabisa, pamoja na maafisa wa jeshi, wakakimbilia Misri kwa kuwaogopa Wakaldayo.
Then all the people, from the least to the greatest, and the commanders of the soldiers, arose and went to Egypt, because they were afraid of the Babylonians.
27 Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini kutoka gerezani siku ya ishirini na saba ya mwezi wa kumi na mbili.
It happened later in the thirty-seventh year of the exile of Jehoiachin king of Judah, in the twelfth month, on the twenty-seventh day of the month, that Awel-Marduk king of Babylon released Jehoiachin king of Judah from prison. This happened in the year that Awel-Marduk began to reign.
28 Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli.
He spoke kindly to him and gave him a seat more honorable than that of the other kings who were with him in Babylon.
29 Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme.
Awel-Marduk removed Jehoiachin's prison clothes, and Jehoiachin ate regularly at the king's table for the rest of his life.
30 Siku kwa siku mfalme alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake.
A regular food allowance was given to him every day for the rest of his life.

< 2 Wafalme 25 >