< 2 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa ishirini na saba wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
W dwudziestym siódmym roku Jeroboama, króla Izraela, Azariasz, syn Amazjasza, króla Judy, zaczął królować.
2 Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
Miał szesnaście lat, kiedy zaczął królować, i królował pięćdziesiąt dwa lata w Jerozolimie. Jego matka miała na imię Jekolia, [była] z Jerozolimy.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
Czynił on to, co słuszne w oczach PANA, wszystko tak jak czynił Amazjasz, jego ojciec.
4 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
Wyżyn jednak nie zniesiono. Lud jeszcze składał ofiary i palił kadzidło na wyżynach.
5 Bwana akampiga mfalme kwa ukoma mpaka siku aliyokufa, naye aliishi katika nyumba iliyotengwa peke yake. Yothamu mwana wa mfalme akawa msimamizi wa jumba la mfalme, na akawatawala watu wa nchi.
I PAN dotknął króla – i był trędowaty aż do [dnia] swojej śmierci, i mieszkał w odosobnionym domu. Jotam więc, syn króla, zarządzał domem i sądził lud ziemi.
6 Matukio mengine ya utawala wa Azaria na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
A pozostałe dzieje Azariasza i wszystko, co czynił, czy nie są zapisane w księdze kronik królów Judy?
7 Azaria akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika Mji wa Daudi, na Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
I Azariasz zasnął ze swymi ojcami, i pogrzebano go wraz z nimi w mieście Dawida, a Jotam, jego syn, królował w jego miejsce.
8 Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, naye akatawala miezi sita.
W trzydziestym ósmym roku Azariasza, króla Judy, Zachariasz, syn Jeroboama, [zaczął] królować nad Izraelem w Samarii i [królował] sześć miesięcy.
9 Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama baba zake walivyofanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
I czynił to, co złe w oczach PANA, jak czynili jego ojcowie. Nie odstąpił od grzechów Jeroboama, syna Nebata, który przywiódł Izraela do grzechu.
10 Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya shauri baya dhidi ya Zekaria. Akamshambulia mbele ya watu, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Szallum, syn Jabesza, uknuł przeciwko niemu spisek i zranił go przed ludem, zabił go i królował w jego miejsce.
11 Matukio mengine ya utawala wa Zekaria yameandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
A pozostałe dzieje Zachariasza oto są zapisane w księdze kronik królów Izraela.
12 Kwa hiyo neno la Bwana lililonenwa kwa Yehu likatimia, kwamba, “Wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Takie było słowo PANA, które wypowiedział do Jehu: Twoi synowie do czwartego pokolenia będą zasiadać na tronie Izraela. I tak się stało.
13 Shalumu mwana wa Yabeshi akawa mfalme katika mwaka wa thelathini na tisa wa Uzia mfalme wa Yuda, naye akatawala katika Samaria kwa mwezi mmoja.
Szallum, syn Jabesza, zaczął królować w trzydziestym dziewiątym roku Uzjasza, króla Judy, i królował jeden miesiąc w Samarii.
14 Kisha Menahemu mwana wa Gadi akaenda kutoka Tirsa mpaka Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi huko Samaria, akamuua na kuingia mahali pake kuwa mfalme.
Bo Menachem, syn Gadiego, przyszedł z Tirsy i wszedł do Samarii, i pobił Szalluma, syna Jabesza w Samarii, zabił go i królował w jego miejsce.
15 Matukio mengine ya utawala wa Shalumu, na mauaji aliyoyafanya, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
A pozostałe dzieje Szalluma i jego spisek, który uknuł, oto są zapisane w księdze kronik królów Izraela.
16 Wakati ule, akianzia Tirsa, Menahemu alishambulia Tifsa na kila mtu ndani yake, na wale waliokuwa maeneo jirani, kwa sababu walikataa kufungua malango yao. Akaiangamiza Tifsa yote, na kuwapasua matumbo wanawake wote wenye mimba.
Wtedy Menachem pobił Tifsach i wszystkich, którzy w nim byli, oraz wszystkie jego okolice, [począwszy] od Tirsy, gdyż nie otworzyli mu [bram] – dlatego je pobił, a wszystkie brzemienne mieszkanki rozpruwał.
17 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akawa mfalme wa Israeli, akatawala huko Samaria kwa miaka kumi.
W trzydziestym dziewiątym roku Azariasza, króla Judy, Menachem, syn Gadiego, [zaczął] królować nad Izraelem i [królował] dziesięć lat w Samarii.
18 Akatenda maovu machoni pa Bwana. Katika wakati wa utawala wake wote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Czynił on to, co złe w oczach PANA. Przez wszystkie swoje dni nie odstąpił od grzechów Jeroboama, syna Nebata, który przywodził Izraela do grzechu.
19 Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaishambulia Israeli. Menahemu mfalme wa Israeli akampa talanta elfu moja za fedha ili amsaidie na kumwezesha katika utawala wake.
A gdy Pul, król Asyrii, napadł na ziemię, Menachem dał Pulowi tysiąc talentów srebra, aby [ten] mu pomógł umocnić królestwo w swoim ręku.
20 Menahemu akatoza fedha hizi kwa nguvu kutoka kwa Israeli. Kila mtu tajiri alilazimika kuchanga shekeli hamsini za fedha ambazo alipewa mfalme wa Ashuru. Basi mfalme wa Ashuru akajiondoa na hakuendelea kuikalia nchi.
I Menachem wymusił te pieniądze od Izraela, od wszystkich zamożnych – po pięćdziesiąt syklów srebra od każdego – aby je dać królowi Asyrii. Wycofał się więc król Asyrii i nie pozostał w tej ziemi.
21 Matukio mengine ya utawala wa Menahemu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
A pozostałe dzieje Menachema i wszystko, co czynił, czy nie są zapisane w księdze kronik królów Izraela?
22 Menahemu akalala pamoja na baba zake. Naye Pekahia mwanawe akawa mfalme baada yake.
I Menachem zasnął ze swymi ojcami, a Pekachiasz, jego syn, królował w jego miejsce.
23 Katika mwaka wa hamsini wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, akatawala miaka miwili.
W pięćdziesiątym roku Azariasza, króla Judy, Pekachiasz, syn Menachema, [zaczął] królować nad Izraelem w Samarii [i królował] dwa lata.
24 Pekahia akafanya uovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Czynił on to, co złe w oczach PANA. Nie odstąpił od grzechów Jeroboama, syna Nebata, który przywiódł Izraela do grzechu.
25 Mmoja wa maafisa wake wakuu, Peka mwana wa Remalia, akafanya shauri baya dhidi yake. Akachukua watu hamsini wa Gileadi pamoja naye, akamuua Pekahia, pamoja na Argobu na Aria, katika ngome ya jumba la kifalme huko Samaria. Kwa hiyo Peka akamuua Pekahia, naye akaingia mahali pake kuwa mfalme.
A Pekach, syn Remaliasza, jego dowódca, uknuł spisek przeciwko niemu i zabił go w Samarii, w pałacu domu królewskiego, a wraz z nim Argoba i Aria oraz pięćdziesięciu ludzi spośród Gileadczyków. Zabił go i królował po nim.
26 Matukio mengine ya utawala wa Pekahia na yote aliyoyafanya yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
A pozostałe dzieje Pekachiasza i wszystko, co czynił, oto są zapisane w księdze kronik królów Izraela.
27 Katika mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala miaka ishirini.
W pięćdziesiątym drugim roku Azariasza, króla Judy, Pekach, syn Remaliasza, [zaczął] królować nad Izraelem w Samarii [i królował] dwadzieścia lat.
28 Akafanya maovu machoni pa Bwana. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda.
Czynił on to, co złe w oczach PANA. Nie odstąpił od grzechów Jeroboama, syna Nebata, który przywiódł Izraela do grzechu.
29 Wakati wa utawala wa Peka mfalme wa Israeli, Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alikuja na kuteka Iyoni, Abel-Beth-Maaka, Yanoa, Kedeshi na Hazori. Akateka miji ya Gileadi na Galilaya, pamoja na nchi yote ya Naftali, na kuwahamishia watu wote Ashuru.
Za dni Pekacha, króla Izraela, nadciągnął Tiglat-Pileser, król Asyrii, i zdobył Ijon, Abel-Bet-Maaka, Janoach, Kedesz, Chasor, Gilead i Galileę, i całą ziemię Neftalego, a pojmanych uprowadził do Asyrii.
30 Kisha Hoshea mwana wa Ela akafanya shauri baya dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akamshambulia na kumuua, kisha akaingia mahali pake kuwa mfalme katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
Wtedy Ozeasz, syn Eli, uknuł spisek przeciwko Pekachowi, synowi Remaliasza. Pobił go i zabił, i [zaczął] królować w jego miejsce w dwudziestym roku Jotama, syna Uzjasza.
31 Matukio mengine ya utawala wa Peka na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
A pozostałe dzieje Pekacha i wszystko, co czynił, oto są zapisane w księdze kronik królów Izraela.
32 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Uzia mfalme wa Yuda alianza kutawala.
W drugim roku Pekacha, syna Remaliasza, króla Izraela, Jotam, syn Uzjasza, króla Judy, [zaczął] królować.
33 Alikuwa na miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
Miał dwadzieścia pięć lat, kiedy zaczął królować, i królował szesnaście lat w Jerozolimie. Jego matka miała na imię Jerusza [i była] córką Sadoka.
34 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya.
Czynił on to, co słuszne w oczach PANA. Czynił wszystko tak, jak czynił Uzjasz, jego ojciec.
35 Hata hivyo, mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko. Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana.
Wyżyn jednak nie zniesiono. Lud jeszcze składał ofiary i palił kadzidło na wyżynach. On zbudował Górną Bramę domu PANA.
36 Matukio mengine ya utawala wa Yothamu na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
A pozostałe dzieje Jotama i wszystko, co czynił, są zapisane w księdze kronik królów Judy.
37 (Katika siku hizo, Bwana akaanza kuwatuma Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia dhidi ya Yuda.)
W tych dniach PAN zaczął posyłać przeciw Judzie Resina, króla Syrii, i Pekacha, syna Remaliasza.
38 Yothamu akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi, mji wa baba zake. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
I Jotam zasnął ze swymi ojcami, i został pogrzebany z nimi w mieście Dawida, swego ojca. I Achaz, jego syn, królował w jego miejsce.

< 2 Wafalme 15 >