< 2 Wafalme 10 >

1 Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
Achab zaś miał siedemdziesięciu synów w Samarii. I Jehu napisał list, i wysłał [go] do Samarii do książąt Jizreel – do starszych i do tych, którzy wychowywali [synów] Achaba – ze słowami:
2 “Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
Jak tylko dotrze do was ten list, a są przecież z wami synowie waszego pana, macie też rydwany, konie, miasto obronne i uzbrojenie;
3 mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
Upatrzcie sobie najlepszego i najodpowiedniejszego z synów waszego pana, posadźcie na tronie jego ojca i walczcie o dom waszego pana.
4 Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
Lecz oni bardzo się przerazili i powiedzieli: Oto dwaj królowie nie ostali się przed nim, a jakże my się ostoimy?
5 Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
Wtedy ten, który był [postawiony] nad domem, i ten, który był nad miastem, starsi oraz wychowawcy [synów króla] wysłali do Jehu wiadomość: Jesteśmy twoimi sługami. Uczynimy wszystko, co nam rozkażesz. Nie ustanowimy żadnego króla. Czyń, co uznasz za dobre w swoich oczach.
6 Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
I napisał do nich drugi list ze słowami: Jeśli jesteście moi i chcecie słuchać mego głosu, weźcie głowy synów waszego pana i przyjdźcie do mnie jutro o tym czasie do Jizreel. A synów królewskich było siedemdziesięciu mężczyzn, przebywających u znakomitych obywateli miasta, którzy ich wychowywali.
7 Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
A gdy doszedł do nich list, wzięli synów królewskich, zabili wszystkich siedemdziesięciu, włożyli ich głowy do koszy i posłali je do niego do Jizreel.
8 Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
Posłaniec przyszedł i oznajmił mu: Przyniesiono głowy synów królewskich. A [on] powiedział: Ułóżcie je w dwa stosy u wejścia bramy – aż do poranku.
9 Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
Rano zaś wyszedł, stanął i przemówił do całego ludu: Jesteście sprawiedliwi. Oto uknułem spisek przeciw swemu panu i zabiłem go, ale kto zabił tych wszystkich?
10 Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
Wiedzcie teraz, że nie upadnie na ziemię [nic] ze słowa PANA, które PAN wypowiedział przeciwko domowi Achaba. PAN bowiem uczynił to, co wypowiedział przez swego sługę Eliasza.
11 Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
Jehu więc zabił wszystkich, którzy pozostali z domu Achaba w Jizreel, wszystkich jego możnych, jego bliskich i jego kapłanów, tak że nie zostawił spośród nich żadnego przy życiu.
12 Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
Potem wstał, odszedł i wyruszył do Samarii. Po drodze, [gdy] był w domu, gdzie pasterze strzygli owce;
13 Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
Jehu spotkał braci Achazjasza, króla Judy, i zapytał: Kim jesteście? Odpowiedzieli: Jesteśmy braćmi Achazjasza i idziemy pozdrowić synów króla i synów królowej.
14 Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
Wtedy rozkazał: Pojmijcie ich żywcem. I pojmali ich żywcem, i zabili przy studni tego domu, gdzie strzyżono owce [w liczbie] czterdziestu dwóch mężczyzn. Nie oszczędził żadnego z nich.
15 Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
Potem odjechał stamtąd i spotkał Jonadaba, syna Rechaba, idącego mu naprzeciw. Pozdrowił go i zapytał: Czy twoje serce jest tak szczere jak moje serce wobec twojego serca? Jonadab odpowiedział: Jest. A jeśli jest, to daj mi swoją rękę. Wtedy dał mu swą rękę i wziął go do siebie na rydwan.
16 Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
Potem powiedział: Jedź ze mną i zobaczysz moją gorliwość dla PANA. I wiózł go na swoim rydwanie.
17 Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
A gdy przyjechał do Samarii, zabił wszystkich, którzy pozostali [z domu] Achaba w Samarii, i wytracił ich według słowa PANA, które wypowiedział do Eliasza.
18 Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
Potem Jehu zebrał cały lud i powiedział do niego: Achab mało służył Baalowi, Jehu będzie mu służył bardziej.
19 Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
Teraz więc zwołajcie do mnie wszystkich proroków Baala, wszystkie jego sługi i wszystkich jego kapłanów, niech nikogo nie zabraknie. Złożę bowiem wielką ofiarę Baalowi. Ktokolwiek się nie stawi, nie pozostanie przy życiu. Lecz Jehu działał podstępnie, chcąc wytracić czcicieli Baala.
20 Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
Jehu dalej rozkazał: Ogłoście święto dla Baala. I obwołano [je].
21 Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
Potem Jehu rozesłał posłańców po całym Izraelu. I zeszli się wszyscy czciciele Baala, tak że nie było [spośród nich] nikogo, kto by nie przyszedł. Weszli do domu Baala i wypełnił się dom Baala od krańca aż do krańca.
22 Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
Następnie powiedział przełożonemu szatni: Wyłóż szaty dla wszystkich czcicieli Baala. I wyłożył dla nich szaty.
23 Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
Wtedy Jehu wraz z Jonadabem, synem Rechaba, wszedł do domu Baala i powiedział czcicielom Baala: Zbadajcie i upewnijcie się, że nie ma z wami nikogo z czcicieli PANA, ale tylko czciciele Baala.
24 Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
Weszli więc, aby złożyć ofiary i całopalenia. Lecz Jehu postawił sobie na zewnątrz osiemdziesięciu mężczyzn, którym powiedział: Jeśli ujdzie ktokolwiek z tego ludu, który wydaję w wasze ręce, to wasze życie będzie [zapłatą] za jego życie.
25 Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
A gdy dokończono składanie całopalenia, Jehu powiedział żołnierzom i dowódcom: Wejdźcie i zabijajcie ich, [aby] nikt nie uszedł. Zabili więc [ich] ostrzem miecza i żołnierze i dowódcy powyrzucali ich. Potem poszli do miasta domu Baala.
26 Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
Wyrzucili posągi z domu Baala i spalili je.
27 Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
Rozbili też posąg Baala, zburzyli dom Baala i uczynili z niego wychodek, [i jest tak] aż do dziś.
28 Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
W ten sposób Jehu wytępił Baala z Izraela.
29 Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
Nie odstąpił jednak od grzechów Jeroboama, syna Nebata, który do grzechu przywiódł Izraela – od złotych cielców, które [były] w Betel i w Dan.
30 Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
Wtedy PAN powiedział do Jehu: Ponieważ dobrze postąpiłeś, wykonując to, co słuszne w moich oczach, i uczyniłeś domowi Achaba według wszystkiego, co było w moim sercu, to twoi synowie aż do czwartego pokolenia będą zasiadać na tronie Izraela.
31 Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
Lecz Jehu nie pilnował [tego], aby postępować z całego swego serca według prawa PANA, Boga Izraela. Nie odstąpił od grzechów Jeroboama, który przywiódł Izraela do grzechu.
32 Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
W tych dniach PAN zaczął umniejszać Izrael: Chazael pobił ich na całym obszarze Izraela;
33 mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
Od Jordanu ku wschodowi, całą ziemię Gileadu, Gadytów, Rubenitów i Manassytów, od Aroeru, który leży nad rzeką Arnon – Gilead i Baszan.
34 Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
A pozostałe dzieje Jehu i wszystko, co czynił, cała jego potęga, czy nie są zapisane w kronikach królów Izraela?
35 Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
I Jehu zasnął ze swymi ojcami, i pogrzebano go w Samarii. A w jego miejsce królował jego syn Jehoachaz.
36 Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.
A czas, w którym Jehu królował nad Izraelem w Samarii, [wynosił] dwadzieścia osiem lat.

< 2 Wafalme 10 >