< 2 Wakorintho 7 >

1 Wapenzi, kwa kuwa tunazo ahadi hizi, basi na tujitakase nafsi zetu kutokana na kila kitu kitiacho mwili na roho unajisi, tukitimiza utakatifu kwa kumcha Mungu.
Having therefore these promises, beloved friends, let us purify ourselves from all defilement of body and of spirit, and secure perfect holiness through the fear of God.
2 Tupatieni nafasi mioyoni mwenu. Hatujamkosea mtu yeyote, hatujampotosha mtu yeyote, wala hatujamdhulumu mtu yeyote.
Make room for us in your hearts. There is not one of you whom we have wronged, not one to whom we have done harm, not one over whom we have gained any selfish advantage.
3 Sisemi haya ili kuwahukumu, kwa kuwa nilisema mwanzo, kwamba ninyi mko mioyoni mwetu hata kwa kufa pamoja au kuishi pamoja.
I do not say this to imply blame, for, as I have already said, you have such a place in our hearts that we would die with you or live with you.
4 Mara nyingi najivuna kwa ajili yenu; naona fahari juu yenu. Nimejawa na faraja. Nina furaha kupita kiasi katika mateso yetu yote.
I have great confidence in you: very loudly do I boast of you. I am filled with comfort: my heart overflows with joy amid all our affliction.
5 Kwa maana hata tulipoingia Makedonia, miili yetu haikuwa na raha. Tulisumbuliwa kila upande, kwa nje kulikuwa na mapigano na mioyoni mwetu tulikuwa na hofu.
For even after our arrival in Macedonia we could get no relief such as human nature craves. We were greatly harassed; there were conflicts without and fears within.
6 Bali Mungu, yeye awafarijie wenye huzuni, alitufariji kwa kufika kwake Tito.
But He who comforts the depressed--even God-- comforted us by the coming of Titus, and not by his coming only,
7 Lakini si kule kuja kwa Tito tu, bali pia kwa faraja mliyompa. Alitueleza jinsi mlivyonionea shauku, huzuni yenu kubwa na juhudi yenu kwa ajili yangu, ili kwamba furaha yangu ipate kuwa kubwa kuliko wakati wowote.
but also by the fact that he had felt comforted on your account, and by the report which he brought of your eager affection, of your grief, and of your jealousy on my behalf, so that I rejoiced more than ever.
8 Hata kama niliwahuzunisha kwa barua yangu, sijutii. Ingawa nilijuta kwa muda mfupi, kwa kuwa najua kwamba barua yangu iliwaumiza, lakini ni kwa kitambo tu,
For if I gave you pain by that letter, I do not regret it, though I did regret it then. I see that that letter, even though for a time it gave you pain, had a salutary effect.
9 lakini sasa nina furaha, si kwa sababu mlihuzunika, bali kwa kuwa huzuni hiyo iliwafanya mtubu. Kwa maana mlihuzunishwa kama Mungu alivyokusudia watu wahuzunike na hivyo sisi hatukuwadhuru kwa njia yoyote.
Now I rejoice, not in your grief, but because the grief led to repentance; for you sorrowed with a godly sorrow, which prevented you from receiving injury from us in any respect.
10 Kwa maana huzuni ya kimungu huleta toba iletayo wokovu na wala haina majuto. Lakini huzuni ya kidunia husababisha mauti.
For godly sorrow produces repentance leading to salvation, a repentance not to be regretted; but the sorrow of the world finally produces death.
11 Tazameni jinsi huzuni hii ya kimungu ilivyoleta faida ndani yenu: bidii mliyo nayo, juhudi mliyofanya kujitetea, uchungu wenu, hofu yenu, upendo wenu, shauku yenu na jinsi mlivyokuwa tayari kutoa adhabu inayostahili. Kwa kila njia mmejithibitisha kuwa safi katika jambo hilo.
For mark the effects of this very thing--your having sorrowed with a godly sorrow--what earnestness it has called forth in you, what eagerness to clear yourselves, what indignation, what alarm, what longing affection, what jealousy, what meting out of justice! You have completely wiped away reproach from yourselves in the matter.
12 Hivyo ingawa niliwaandikia, haikuwa kwa sababu ya huyo aliyekosa au huyo aliyekosewa. Lakini nilitaka ninyi wenyewe mwone, mbele za Mungu, jinsi mlivyojitoa kwa ajili yetu.
Therefore, though I wrote to you, it was not to punish the offender, nor to secure justice for him who had suffered the wrong, but it was chiefly in order that your earnest feeling on our behalf might become manifest to yourselves in the sight of God.
13 Kwa ajili ya haya tumefarijika. Zaidi ya kule sisi kutiwa moyo, tulifurahi sana kumwona Tito alivyo na furaha, kwa sababu roho yake imeburudishwa na ninyi nyote.
For this reason we feel comforted; and--in addition to this our comfort--we have been filled with all the deeper joy at Titus's joy, because his spirit has been set at rest by you all.
14 Nilikuwa nimewasifu ninyi kwake, nanyi hamkuniaibisha. Lakini kila kitu tulichowaambia ninyi, kilikuwa kweli, hivyo kule kujisifu kwetu kwa Tito kuwahusu ninyi kumethibitishwa kuwa kweli pia.
For however I may have boasted to him about you, I have no reason to feel ashamed; but as we have in all respects spoken the truth to you, so also our boasting to Titus about you has turned out to be the truth.
15 Upendo wake kwenu unaongezeka sana anapokumbuka jinsi mlivyokuwa watiifu, na kumpokea kwa hofu na kutetemeka.
And his strong and tender affection is all the more drawn out towards you when he recalls to mind the obedience which all of you manifested by the timidity and nervous anxiety with which you welcomed him.
16 Nafurahi kwamba ninaweza kuwatumaini ninyi kabisa.
I rejoice that I have absolute confidence in you.

< 2 Wakorintho 7 >