< 2 Wakorintho 2 >

1 Hivyo nilikusudia moyoni mwangu nisifanye ziara nyingine yenye kuwaumiza ninyi.
But, so far as I am concerned, I have resolved not to have a painful visit the next time I come to see you.
2 Kwa kuwa kama nikiwahuzunisha ninyi, ni nani aliyebaki wa kunifurahisha isipokuwa ninyi ambao nimewahuzunisha?
For if I of all men give you pain, who then is there to gladden my heart, but the very persons to whom I give pain?
3 Niliandika hivyo kama nilivyofanya, ili nikija nisihuzunishwe na wale watu ambao wangenifanya nifurahi. Nina uhakika na ninyi nyote, kwamba wote mngeshiriki furaha yangu.
And I write this to you in order that when I come I may not receive pain from those who ought to give me joy, confident as I am as to all of you that my joy is the joy of you all.
4 Kwa maana niliwaandikia kutokana na dhiki kubwa na kutaabika sana kwa moyo wangu tena kwa machozi mengi, shabaha yangu si ili niwasababishe mhuzunike bali kuwaonyesha kina cha upendo wangu kwenu.
For with many tears I write to you, and in deep suffering and depression of spirit, not in order to grieve you, but in the hope of showing you how brimful my heart is with love for you.
5 Lakini ikiwa mtu yeyote amesababisha huzuni, kwa kiasi fulani hakunihuzunisha mimi kama vile alivyowahuzunisha ninyi nyote, ili nisiwe mkali kupita kiasi.
Now if any one has caused sorrow, it has been caused not so much to me, as in some degree--for I have no wish to exaggerate--to all of you.
6 Adhabu hii aliyopewa na wengi inamtosha.
In the case of such a person the punishment which was inflicted by the majority of you is enough.
7 Basi sasa badala yake, inawapasa kumsamehe na kumfariji, ili asigubikwe na huzuni kupita kiasi.
So that you may now take the opposite course, and forgive him rather and comfort him, for fear he should perhaps be driven to despair by his excess of grief.
8 Kwa hiyo, nawasihi, mpate kuuthibitisha tena upendo wenu kwa ajili yake.
I beg you therefore fully to reinstate him in your love.
9 Sababu ya kuwaandikia ni kuona kama mngeweza kushinda hilo jaribio na kutii katika kila jambo.
For in writing to you I have also this object in view--to discover by experience whether you are prepared to be obedient in every respect.
10 Kama ninyi mkimsamehe mtu yeyote, mimi pia nimemsamehe. Kile nilichosamehe, kama kulikuwa na kitu chochote cha kusamehe, nimekwisha kusamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
When you forgive a man an offence I also forgive it; for in fact what I have forgiven, if I have forgiven anything, has always been for your sakes in the presence of Christ,
11 ili Shetani asitushinde. Kwa maana hatuachi kuzijua hila zake.
for fear Satan should gain an advantage over us. For we are not ignorant of his devices.
12 Basi nilipofika Troa kuhubiri Injili ya Kristo na kukuta kwamba Bwana alikuwa amenifungulia mlango,
Now when I came into the Troad to spread there the Good News about the Christ, even though in the Lord's providence a door stood open before me,
13 bado nilikuwa sina utulivu akilini mwangu kwa sababu sikumkuta ndugu yangu Tito huko. Hivyo niliagana nao nikaenda Makedonia.
yet, obtaining no relief for my spirit because I did not find our brother Titus, I bade them farewell and went on into Macedonia.
14 Lakini Mungu ashukuriwe, yeye ambaye siku zote hutufanya tuandamane kwa ushindi tukiwa ndani ya Kristo. Naye kupitia kwetu hueneza kila mahali harufu nzuri ya kumjua yeye.
But to God be the thanks who in Christ ever heads our triumphal procession, and by our hands waves in every place that sweet incense, the knowledge of Him.
15 Kwa maana sisi kwa Mungu ni harufu nzuri ya manukato ya Kristo miongoni mwa wale wanaookolewa na kwa wale wanaopotea.
For we are a fragrance of Christ grateful to God in those whom He is saving and in those who are perishing;
16 Kwa wale wanaopotea, sisi ni harufu ya mauti iletayo mauti; lakini kwa wale wanaookolewa, sisi ni harufu nzuri iletayo uzima. Ni nani awezaye mambo hayo?
to the last-named an odor of death predictive of death, and to the others an odor of life predictive of life. And for such service as this who is competent?
17 Tofauti na watu wengine wengi, sisi hatufanyi biashara na Neno la Mungu kwa ajili ya kupata faida. Kinyume chake, katika Kristo tunalisema Neno la Mungu kwa unyoofu, kama watu tuliotumwa kutoka kwa Mungu.
We are; for, unlike most teachers, we are not fraudulent hucksters of God's Message; but with transparent motives, as commissioned by God, in God's presence and in communion with Christ, so we speak.

< 2 Wakorintho 2 >