< 2 Nyakati 22 >

1 Watu wa Yerusalemu wakamfanya Ahazia, mdogo wa wote wa wana wa Yerohamu, kuwa mfalme mahali pa baba yake, kwa sababu washambuliaji wa ghafula waliokuwa wameingia kambini pamoja na Waarabu, walikuwa wamewaua wana wakubwa wote wa Yehoramu. Kwa hiyo Ahazia mwana wa Yehoramu mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
Et les habitants de Jérusalem firent Achazia, son fils cadet, roi en sa place; car tous les aînés avaient été tués par la horde venue avec les Arabes au camp. Ainsi devint roi Achazia, fils de Joram, roi de Juda.
2 Ahazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala katika Yerusalemu kwa mwaka mmoja. Mama yake aliitwa Athalia, mjukuu wa Omri.
Achazia avait quarante-deux ans à son avènement, et il régna un an à Jérusalem. Or le nom de sa mère était Athalie, fille d'Omri.
3 Ahazia naye akaenenda katika njia za nyumba ya Ahabu, kwa sababu mama yake alimshawishi katika kutenda maovu.
Lui aussi marcha sur les errements de la maison d'Achab, car sa mère était sa conseillère d'impiété.
4 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana kama walivyokuwa wamefanya nyumba ya Ahabu, kwa kuwa baada ya kufa kwa baba yake nyumba ya Ahabu ndio waliokuwa washauri wake, kwa uangamivu wake.
Et il fit ce qui est mal aux yeux de l'Éternel, comme la maison d'Achab, car là furent ses conseillers après la mort de son père, pour sa perte.
5 Pia akafuata shauri lao alipokwenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu mfalme wa Israeli kupigana na Hazaeli mfalme wa Aramu huko Ramoth-Gileadi. Waaramu wakamjeruhi Yoramu.
Ce fut aussi d'après leur conseil qu'il se conduisit, et qu'il marcha avec Joram, fils d'Achab, roi d'Israël, à l'attaque de Hazaël, roi de Syrie, à Ramoth en Galaad. Et les Syriens blessèrent Joram,
6 Hivyo akarudi Yezreeli ili apate kuuguza majeraha aliyojeruhiwa huko Ramothi alipopigana na Hazaeli mfalme wa Aramu. Ndipo Ahazia mwana wa Yehoramu, mfalme wa Yuda, akashuka kwenda Yezreeli kumtazama Yoramu mwana wa Ahabu, kwa sababu alikuwa amejeruhiwa.
qui alors rebroussa pour se faire traiter à Jizréel des blessures qu'il avait reçues à Rama, lorsqu'il se battait contre Hazaël, roi de Syrie. Et Azaria, fils de Joram, roi de Juda, descendit pour visiter Joram, fils d'Achab, à Jizréel, parce qu'il était malade.
7 Mungu alikuwa ameamuru kwamba kuanguka kwa Ahazia kungetokea atakapokwenda kumwona Yoramu. Ahazia alipowasili, wakatoka pamoja na Yoramu ili kwenda kukutana na Yehu mwana wa Nimshi, ambaye Bwana alikuwa amemtia mafuta kuangamiza nyumba ya Ahabu.
Et c'est par la volonté de Dieu qu'Achazia se perdit en venant auprès de Joram; et à son arrivée il s'achemina avec Joram, au-devant de Jéhu, fils de Nimsi, que l'Éternel avait oint pour extirper la maison d'Achab.
8 Yehu alipokuwa anatekeleza hukumu juu ya nyumba ya Ahabu, akawakuta wakuu wa Yuda na wana wa jamaa ya Ahazia waliokuwa wanamhudumia Ahazia, naye akawaua.
Et comme Jéhu faisait justice de la maison d'Achab, il atteignit les chefs de Juda et les fils des frères d'Achab, qui étaient au service d'Achazia, et les massacra.
9 Ndipo akaenda kumsaka Ahazia, nao watu wake wakamkamata alipokuwa amejificha huko Samaria. Akaletwa kwa Yehu, naye Yehu akamuua. Wakamzika kwani walisema, “Alikuwa mwana wa Yehoshafati, ambaye alimtafuta Bwana kwa moyo wake wote.” Hivyo hapakuwa na mtu mwenye uwezo katika nyumba ya Ahazia aliyeweza kushika ufalme.
Et il chercha Achazia, qui fut pris comme il se cachait dans Samarie, et on l'emmena à Jéhu, et on le fit mourir, et on lui donna la sépulture; car ils disaient: C'est le fils de Josaphat qui cherchait l'Éternel de tout son cœur. Et dans la maison d'Achazia il n'y avait personne d'apte à régner.
10 Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kuwa mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya mfalme ya nyumba ya Yuda.
Mais Athalie, mère d'Achazia, voyant son fils mort, se mit en devoir de détruire toute la race royale de la maison de Juda.
11 Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa mfalme waliokuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala. Kwa kuwa Yehosheba, aliyekuwa binti wa Mfalme Yehoramu, na pia alikuwa mke wa kuhani Yehoyada, alikuwa dada yake Ahazia, akamficha huyo mtoto ili Athalia asimuue.
Alors Josabeath, fille de roi, prit Joas, fils d'Achazia, et parvint à le soustraire du milieu des fils du roi qu'on mettait à mort, et le logea lui et sa nourrice dans la salle des lits; ainsi le cacha Josabeath, fille du roi Joram, femme de Joiada, le Prêtre (car elle était sœur d'Achazia) aux regards d'Athalie, afin que celle-ci ne le fît pas mourir;
12 Alibaki amefichwa pamoja nao katika Hekalu la Mungu kwa muda wa miaka sita wakati Athalia alikuwa akitawala nchi.
et il fut avec eux dans la maison de Dieu, caché pendant six ans. Cependant Athalie régissait le pays.

< 2 Nyakati 22 >