< 1 Samweli 9 >

1 Kulikuwako Mbenyamini mmoja, mtu maarufu, ambaye aliitwa Kishi mwana wa Abieli, mwana wa Serori, mwana wa Bekorathi, mwana wa Afia wa Benyamini.
And `a man was of Beniamyn, `Cys bi name, the sone of Abiel, sone of Seor, sone of Bethor, sone of Aphia, sone of the man Gemyny, strong in bodili myyt.
2 Alikuwa na mwana aliyeitwa Sauli, kijana anayevutia sana, hakuwepo aliyelingana naye miongoni mwa Waisraeli, alikuwa mrefu kuliko wengine wote.
And to hym was a sone, Saul bi name, chosun and good; and no man of the sones of Israel was betere than he; fro the schuldur and aboue he apperide ouer al the puple.
3 Basi punda wa Kishi baba yake Sauli walipotea, naye Kishi akamwambia mwanawe Sauli, “Mchukue mmoja wa watumishi mwende pamoja naye kuwatafuta punda.”
Sotheli the femal assis of Cys, the fadir of Saul, perischyden. And Cys seide to Saul his sone, Take with thee oon of the children, and rise thou, and go, and seke the femal assis. And whanne thei hadden go bi the hil of Effraym,
4 Hivyo akapita katika nchi ya vilima ya Efraimu na katika eneo la Shalisha, lakini hawakuwapata. Wakaendelea katika sehemu ya Shaalimu, lakini punda hawakuwepo huko. Kisha wakapita katika nchi ya Benyamini, lakini hawakuwapata.
and bi the lond of Salisa, and hadden not foundun, thei passiden also bi the lond of Salym, and tho weren not there; but also 'thei passiden bi the lond of Gemyny, and founden not.
5 Walipofika sehemu ya Sufu, Sauli akamwambia mtumishi aliyekuwa pamoja naye, “Njoo, sisi na turudi, au baba yangu ataacha kufikiria juu ya punda na kuanza kufadhaika kutuhusu sisi.”
Sotheli whanne thei hadden come in to the lond of Suph, and hadden not founde, Saul seide to his child that was with hym, Come thou, and turne we ayen; lest perauenture my fadir hath lefte the femal assis, and is bisy for vs.
6 Lakini mtumishi akajibu, “Tazama, katika mji huu yupo mtu wa Mungu, anayeheshimiwa sana na kila kitu asemacho hutokea kweli. Sasa na twende huko. Huenda atatuambia twende njia ipi.”
Which child seide to hym, Lo! the man of God is in this citee, a noble man; al thing that he spekith, cometh with out doute. Now therfor go we thidir, if perauenture he schewe to vs of oure weie, for which we camen.
7 Sauli akamwambia mtumishi wake, “Kama tukienda, tutampa nini huyo mtu? Chakula kimekwisha kwenye mifuko yetu. Hatuna zawadi ya kumpelekea huyo mtu wa Mungu. Je tuna nini?”
And Saul seide to his child, Lo! we schulen go; what schulen we bere to the man of God? Breede failide in oure scrippis, and we han no present, that we yyue to the man of God, `nether ony othir thing.
8 Mtumishi akamjibu Sauli tena, akasema, “Tazama, nina fedha robo shekeli. Hiyo nitampa huyo mtu wa Mungu ili aweze kutuambia twende kwa njia ipi.”
Eft the child answeride to Saul, and seide, Lo! the fourthe part of `a stater, that is, a cicle, of siluer is foundun in myn hond; yyue we to the man of God, that he schewe to vs oure weie.
9 (Zamani katika Israeli, kama mtu alikwenda kuuliza neno kwa Mungu, angalisema, “Njoo na twende kwa mwonaji,” kwa sababu nabii wa sasa alikuwa akiitwa mwonaji.)
Sumtyme in Israel ech man goynge to counsel God spak thus, Come ye, and go we to the seere; for he, that is seid `to dai a profete, was clepid sumtyme a seere.
10 Sauli akamwambia mtumishi wake, “Vyema, njoo na twende.” Basi wakaenda mjini alipokuwepo huyo mtu wa Mungu.
And Saul seide to his child, `Thi word is the beste; come thou, go we. And thei yeden in to the citee, `in which the man of God was.
11 Walipokuwa wakipanda mlima kwenda mjini, wakakutana na baadhi ya wasichana wanakuja kuchota maji, nao wakawauliza, “Je, mwonaji yuko?”
And whanne thei stieden in to the hiynesse of the citee, thei founden damesels goynge out to drawe watir, and thei seiden to the dameselis, Whether the seere is here?
12 Wakajibu, “Yuko, yu mbele yenu amewatangulia, sasa fanyeni haraka, ndiyo tu amekuja mjini kwetu leo, kwa kuwa watu wana dhabihu huko mahali pa juu.
Whiche dameselis answeriden, and seiden to hem, He is here; lo! he is bifor thee; `haste thou now, for to day he cam in to the citee; for to dai is sacrifice of the puple in the hiy place.
13 Mara tu mwingiapo mjini, mtamkuta kabla hajapanda kwenda mahali pa juu kula. Watu hawataanza kula mpaka atakapofika kwa sababu ni lazima kwanza yeye abariki dhabihu, ndipo wale walioalikwa watakapokula. Pandeni sasa, mtamkuta kwa wakati huu.”
Ye schulen entre in to the citee, and anoon ye schulen fynde hym, bifor that he stie in to the hiy place to ete; for the puple schal not ete til he come, for he schal blesse the sacrifice, and afterward thei schulen ete that ben clepid. Now therfor stie ye, for to day ye schulen fynde hym.
14 Wakapanda mjini, nao walipokuwa wakiingia mjini, tazama, Samweli alikuwa akija kuelekea walikokwenda mahali pa juu.
And thei stieden in to the citee. And whanne thei yeden in the myddis of the citee, Samuel apperide goynge out ayens hem, that he schulde stie in to the hiy place.
15 Basi siku moja kabla Sauli hajaja, Bwana alikuwa amemfunulia Samweli jambo hili:
Forsothe the Lord `hadde maad reuelacioun in the eere of Samuel `bifor o dai, that Saul cam, and seide,
16 “Kesho wakati kama huu nitakupelekea mtu kutoka nchi ya Benyamini. Umtie mafuta awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli, ndiye atakayewakomboa watu wangu na mkono wa Wafilisti. Nimewaangalia watu wangu, kwa kuwa kilio chao kimenifikia.”
In this same our which is now to morewe, Y schal sende to thee a man of the lond of Beniamyn, and thou schalt anoynte hym duyk on my puple Israel, and he schal saue my puple fro the hond of Filisteis; for Y haue biholde my puple, for `the cry of hem cam to me.
17 Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, “Huyu ndiye mtu niliyekuambia habari zake, kwamba yeye atawatawala watu wangu.”
And whanne Samuel hadde biholde Saul, the Lord seide to Samuel, Lo! the man, whom Y seide to thee; this man schal be lord of my puple.
18 Sauli akamkaribia Samweli langoni na kumuuliza, “Tafadhali, je, waweza kuniambia mahali nyumba ya mwonaji ilipo?”
Forsothe Saul neiyede to Samuel in the myddis of the yate, and seide, Y preye, schewe thou to me, where is the hows of the seere?
19 Samweli akamjibu Sauli, “Mimi ndiye mwonaji, panda utangulie mbele yangu mpaka mahali pa juu, kwa kuwa leo itakupasa kula pamoja nami na asubuhi nitakuruhusu uende na nitakuambia yale yote yaliyo moyoni mwako.
And Samuel answeride to Saul, and seide, Y am the seere; stie thou bifor me in to the hiy place, that thou ete with me to dai, and Y schal delyuere thee in the morewtid, and Y schal schewe to thee alle thingis that ben in thin herte.
20 Kuhusu wale punda uliowapoteza siku tatu zilizopita, usifadhaike kwa habari yao; wamepatikana. Ni kwa nani ambaye shauku yote ya Israeli imeelekea, kama si kwako na jamaa yote ya baba yako?”
And be thou not bisy of the femal assis, whiche thou lostist the thridde dai agoon, for tho ben foundun; and whose schulen be alle the beste thingis of Israel, whether not to thee, and to al the hows of thi fader?
21 Sauli akajibu, “Je, mimi si Mbenyamini, kutoka kabila dogo kuliko yote ya Israeli, nao ukoo wangu si ndio mdogo kuliko koo zote za kabila la Benyamini? Kwa nini uniambie jambo la namna hiyo?”
Sotheli Saul answeride, and seide, Whether Y am not a sone of Gemyny, of the leeste lynage of Israel, and my kynrede is the laste among alle the meynees of the lynage of Beniamyn? Whi therfor hast thou spoke to me this word?
22 Kisha Samweli akamleta Sauli na mtumishi wake ndani ukumbini na kuwaketisha mahali pa heshima zaidi miongoni mwa wale waliokuwa wamealikwa; jumla yao walikuwa kama watu thelathini.
Therfor Samuel took Saul, and his child, and ledde hem in to the chaumbur of thre ordris, and he yaf to hem a place in the bigynnyng of hem that weren clepid; for thei weren as thretti men.
23 Samweli akamwambia mpishi, “Leta ile sehemu ya nyama niliyokupa, ile niliyokuambia iweke kando.”
And Samuel seide to the cook, Yyue thou the part, which Y yaf to thee, and comaundide, that thou schuldist kepe bi it silf anentis thee.
24 Hivyo mpishi akachukua mguu pamoja na kile kilichokuwa juu yake akaiweka mbele ya Sauli. Samweli akasema, “Hiki ndicho ambacho kimewekwa kwa ajili yako. Ule, kwa sababu kilitengwa kwa ajili yako kwa tukio hili, tangu niliposema, ‘Nimewaalika wageni.’” Naye Sauli akala pamoja na Samweli siku ile.
Sotheli the cook reiside the schuldir, and settide bifor Saul. And Samuel seide, Lo! that, that lefte, `sette thou bifor thee, and ete; for of purpos it was kept to thee, whanne Y clepide the puple. And Saul eet with Samuel in that dai.
25 Baada ya kushuka kutoka mahali pa juu na kufika mjini, Samweli alizungumza na Sauli juu ya dari ya nyumba yake.
And thei camen doun fro the hiy place in to the citee; and Samuel spak with Saul in the soler, and Saul `araiede a bed in the soler, and slepte.
26 Walipoamka mapema alfajiri, Samweli akamwita Sauli darini, akamwambia, “Jiandae, nami nitakuaga uende zako.” Sauli alipokuwa tayari yeye na Samweli wakatoka nje pamoja.
And whanne thei hadden rise eerli, and `now it bigan to be cleer, Samuel clepide Saul in to the soler, and seide, Rise thou, that Y delyuere thee. And Saul roos, and bothe yeden out, that is, he, and Samuel.
27 Hata walipokuwa wakiteremka kuelekea mwisho wa mji, Samweli akamwambia Sauli, “Mwambie mtumishi atangulie mbele yetu.” Naye mtumishi akafanya hivyo. “Lakini subiri hapa kwa kitambo kidogo, ili nipate kukupa ujumbe kutoka kwa Mungu.”
And whanne thei yeden doun in the laste part of the citee, Samuel seide to Saul, Seie thou to the child, that he go bifor vs, and passe; forsothe stonde thou a litil, that Y schewe to thee the word of the Lord.

< 1 Samweli 9 >