< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
Davut Gat'tan ayrılıp Adullam Mağarası'na kaçtı. Bunu duyan kardeşleri ve ailesinin öteki bireyleri yanına gittiler.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
Sıkıntısı, borcu, hoşnutsuzluğu olan herkes Davut'un çevresinde toplandı. Davut sayısı dört yüze varan bu adamlara önderlik yaptı.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
Davut oradan Moav'daki Mispa Kenti'ne gitti. Moav Kralı'ndan, “Tanrı'nın bana ne yapacağı belli oluncaya dek annemle babamın gelip yanınızda kalmasına izin verir misin?” diye bir istekte bulundu.
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
Böylece Davut annesiyle babasını Moav Kralı'nın yanına bıraktı. Davut sığınakta kaldığı sürece onlar da Moav Kralı'nın yanında kaldılar.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
Ne var ki, Peygamber Gad Davut'a, “Sığınakta kalma. Yahuda ülkesine git” dedi. Bunun üzerine Davut oradan ayrılıp Heret Ormanı'na gitti.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
Bu sırada Saul Davut'la yanındakilerin nerede olduklarını öğrendi. Saul elinde mızrağıyla Giva'da bir tepedeki ılgın ağacının altında oturuyordu. Askerleri de çevresinde duruyordu.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
Saul onlara şöyle dedi: “Ey Benyaminliler, şimdi dinleyin! İşay'ın oğlu her birinize tarlalar, bağlar mı verecek? Her birinizi binbaşı, yüzbaşı mı yapacak?
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
Hepiniz bana karşı düzen kurdunuz. Çünkü oğlum İşay'ın oğluyla antlaşma yaptığında bana haber veren olmadı. İçinizden bana acıyan tek kişi çıkmadı. Bugün olduğu gibi, bana pusu kurması için oğlumun kulum Davut'u kışkırttığını bana bildiren olmadı.”
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Bunun üzerine Saul'un askerlerinin yanında duran Edomlu Doek, “İşay oğlu Davut'un Nov Kenti'ne, Ahituv oğlu Kâhin Ahimelek'in yanına geldiğini gördüm” dedi,
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
“Ahimelek Davut için RAB'be danıştı. Ona hem yiyecek sağladı, hem de Filistli Golyat'ın kılıcını verdi.”
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Kral Saul, Ahituv oğlu Kâhin Ahimelek'i ve babasının ailesinden Nov'da yaşayan bütün kâhinleri çağırmak için ulaklar gönderdi. Hepsi kralın yanına geldi.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
Saul Ahimelek'e, “Ey Ahituv oğlu, beni dinle!” dedi. Ahimelek, “Buyur, efendim” diye yanıtladı.
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
Saul, “Neden sen ve İşay oğlu bana karşı düzen kurdunuz?” dedi, “Çünkü ona ekmek, kılıç verdin ve onun için Tanrı'ya danıştın. O da bana karşı ayaklandı ve bugün yaptığı gibi pusu kurdu.”
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
Ahimelek, “Bütün görevlilerin arasında Davut kadar sana bağlı biri var mı?” diye karşılık verdi, “Davut senin damadın, muhafız birliği komutanın ve ailende saygın biridir.
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Ben Davut için Tanrı'ya danışmaya o gün mü başladım? Kesinlikle hayır! Kral ben kulunu ve babasının ailesini suçlamasın. Çünkü kulun bu konuda hiçbir şey bilmiyor.”
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
Ama Saul, “Ey Ahimelek, sen de bütün ailen de kesinlikle öleceksiniz” dedi.
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
Sonra yanında duran nöbetçi askerlere, “Gidin ve Davut'u destekleyen RAB'bin kâhinlerini öldürün!” dedi, “Çünkü onun kaçtığını bildikleri halde bana haber vermediler.” Ne var ki, kralın görevlileri el kaldırıp RAB'bin kâhinlerini öldürmek istemediler.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
Bunun üzerine kral, Doek'e, “Sen git, kâhinleri öldür” diye buyurdu. Edomlu Doek de gidip kâhinleri öldürdü. O gün Doek keten efod giymiş seksen beş kişi öldürdü.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
Kadın erkek, çoluk çocuk demeden kâhinler kenti Nov'un halkını kılıçtan geçirdi. Sığırları, eşekleri, koyunları da öldürdü.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
Yalnız Ahituv oğlu Kâhin Ahimelek'in oğullarından Aviyatar adında biri kurtulup Davut'a kaçtı.
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
Aviyatar Saul'un RAB'bin kâhinlerini öldürttüğünü Davut'a söyledi.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
Davut Aviyatar'a, “O gün orada bulunan Edomlu Doek'in olup biteni Saul'a bildireceğini anlamıştım zaten” dedi, “Babanın bütün aile bireylerinin ölümüne ben neden oldum.
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Yanımda kal ve korkma! Seni öldürmek isteyen beni de öldürmek istiyor. Yanımda güvenlikte olursun.”

< 1 Samweli 22 >