< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
Entonces David se fue de allí y se escondió en una cueva en Adullam; y sus hermanos y toda la gente de su padre, oyéndolo, descendieron a él allí.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
Y todos los que estaban en problemas, y todos los que estaban endeudados, y todos los que tenían un alma amargada, se reunieron con él, y se convirtió en capitán sobre ellos, se unieron a él unos cuatrocientos hombres.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
Y de allí, David fue a Mizpa en la tierra de Moab; y dijo al rey de Moab: Que vengan mi padre y mi madre, y vivan contigo hasta que esté claro para mí lo que Dios hará de mí.
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
Luego los llevó al rey de Moab y se fueron a vivir con él mientras David estaba en su lugar seguro.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
Y el profeta Gad dijo a David: No sigas viviendo en este lugar, sino que vete a la tierra de Judá. Entonces David se fue y vino al bosque de Haret.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
Y a Saúl se le comunicó que habían visto a David y a los hombres que estaban con él: ahora Saúl estaba en Guibea, sentado debajo del árbol en el lugar alto, con su lanza en la mano, rodeado de todos sus oficiales.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
Entonces Saúl dijo a sus siervos que estaban allí cerca de él: Escuchen ahora, hombres de Benjamín; ¿Dará el hijo de Isaí a cada uno de ustedes campos y vides, les hará a todos capitanes de cientos y capitanes de miles?
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
Todos ustedes hicieron planes contra mí, y ninguno de ustedes me dijo nada cuando mi hijo llegó a un acuerdo con el hijo de Isaí, y ninguno de ustedes se compadeció de mí ni me abrió los ojos. ¿Al hecho de que mi sirviente haya sido influenciado por mi hijo en mi contra, como lo hace ahora?
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Entonces respondió Doeg, el edomita, que estaba al lado de los sirvientes de Saúl, y dijo: Vi al hijo de Isaí venir a Nob, a Ahimelec, hijo de Ahitob.
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
Recibió las instrucciones del Señor para él, y le dio de comer, y puso en su mano la espada de Goliat el filisteo.
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Entonces el rey envió al sacerdote Ahimelec, hijo de Ahitob, y a todos los hombres de la familia de su padre que eran sacerdotes en Nob; y todos vinieron al rey.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
Entonces Saúl dijo: Escucha ahora, hijo de Ahitob. Y respondiendo, dijo: Aquí estoy, señor mío.
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
Entonces Saúl le dijo: ¿Por qué has hecho planes contra mí con el hijo de Isaí, le has dado comida y una espada y has recibido instrucciones del Señor para él, y le has ayudado a tomar las armas contra mí? ¿Estar en guardia para atacarme en secreto como lo está haciendo ahora?
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
Entonces respondiendo Ahimelec, dijo al rey: Quien entre todos tus siervos te es tan fiel como David, que es el yerno del rey, y es capitán de tus hombres armados, y tiene un lugar de honor en tu casa?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
¿Es esta la primera vez que tengo instrucciones de Dios para él? ¡Lejos sea de mi! no permita que el rey haga tal declaración contra su sirviente o la familia de mi padre, porque su sirviente no tiene conocimiento, ni grande ni pequeño, de esto.
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
Y el rey dijo: Ciertamente morirás, Ahimelec, tú y toda la familia de tu padre.
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
Entonces el rey dijo a su guardia personal: pongan a los sacerdotes del Señor a muerte; porque están del lado de David, y sabiendo que él estaba huyendo, no me lo dijeron. Pero los siervos del rey no extendían sus manos para atacar a los sacerdotes del Señor.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
Entonces el rey dijo a Doeg: Tú debes matar a los sacerdotes. Y Doeg el edomita, que se volvió contra los sacerdotes y los atacó, mató ese día a ochenta y cinco hombres que tomaron el efod.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
Y fue a Nob, el pueblo de los sacerdotes, puso a la espada a todos los hombres y mujeres, niños y bebés en el pecho, y bueyes, asnos y ovejas.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
Y Abiatar, uno de los hijos de Ahimelec, hijo de Ahitob, se escapó y huyó después de David;
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
Y le dio la noticia de cómo Saúl había dado muerte a los sacerdotes del Señor.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
Y David le dijo a Abiatar: Estaba seguro ese día, cuando Doeg el edomita estaba allí, que llevaría la noticia a Saúl. Soy responsable de la vida de toda la familia de tu padre.
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Quédate aquí conmigo y no tengas miedo; porque el que quiere matarte también quiere matarme a mí, pero conmigo estarás a salvo.

< 1 Samweli 22 >