< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
David partiu de lá e fugiu para a caverna de Adullam. Quando seus irmãos e toda a casa de seu pai ouviram isso, foram até lá para ele.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
Todos os que estavam em perigo, todos os que estavam em débito e todos os que estavam descontentes se reuniram a ele; e ele se tornou capitão sobre eles. Havia com ele cerca de quatrocentos homens.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
David foi de lá para Mizpeh dos Moab; e disse ao rei dos Moab: “Por favor, deixe meu pai e minha mãe virem até você, até que eu saiba o que Deus fará por mim”.
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
Ele os trouxe diante do rei dos moabitas; e eles viveram com ele todo o tempo que Davi esteve na fortaleza.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
O profeta Gad disse a David: “Não fique na fortaleza”. Parta, e vá para a terra de Judá”. Então David partiu, e entrou na floresta de Hereth.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
Saul soube que David foi descoberto, com os homens que estavam com ele. Agora Saul estava sentado em Gibeah, debaixo da tamargueira em Ramah, com sua lança na mão, e todos os seus servos estavam de pé ao seu redor.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
Saul disse a seus servos que estavam ao seu redor: “Ouçam agora, seus benjamitas! O filho de Jessé dará a todos vocês campos e vinhedos? Ele fará de vocês todos capitães de milhares e capitães de centenas?
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
É por isso que todos vocês conspiraram contra mim, e não há ninguém que me revele quando meu filho faz um tratado com o filho de Jessé, e não há nenhum de vocês que tenha pena de mim, ou que me revele que meu filho agitou meu servo contra mim, para ficar à espera, como é hoje”?
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Então Doeg o edomita, que estava ao lado dos servos de Saul, respondeu e disse: “Eu vi o filho de Jesse chegando a Nob, a Ahimelech o filho de Ahitub.
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
Ele perguntou a Javé por ele, deu-lhe comida e deu-lhe a espada de Golias, o filisteu”.
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Então o rei enviou para chamar Ahimelech o sacerdote, o filho de Ahitub, e toda a casa de seu pai, os sacerdotes que estavam em Nob; e todos eles vieram para o rei.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
Saul disse: “Ouvi agora, filho de Ahitub”. Ele respondeu: “Aqui estou eu, meu senhor”.
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
Saul disse-lhe: “Por que conspiraste contra mim, tu e o filho de Jessé, na medida em que lhe deste pão, e uma espada, e pediste a Deus por ele, que se levantasse contra mim, para ficar à espera, como é hoje”?
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
Então Ahimelech respondeu ao rei, e disse: “Quem entre todos os seus servos é tão fiel como Davi, que é genro do rei, capitão de sua guarda corporal, e honrado em sua casa?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Comecei hoje a perguntar a Deus por ele? Fique longe de mim! Não deixe o rei imputar nada a seu servo, nem a toda a casa de meu pai; pois seu servo nada sabia de tudo isso, menos ou mais”.
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
O rei disse: “Certamente morrerás, Ahimelech, tu e toda a casa de teu pai”.
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
O rei disse ao guarda que estava de pé sobre ele: “Vira-te e mata os sacerdotes de Javé, porque sua mão também está com Davi, e porque eles sabiam que ele fugiu e não me revelaram”. Mas os servos do rei não estendiam a mão para cair sobre os sacerdotes de Yahweh.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
O rei disse a Doeg: “Virem-se e ataquem os padres”! Doeg o Edomita virou-se, e atacou os padres, e matou naquele dia oitenta e cinco pessoas que usavam um éfode de linho.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
Ele atingiu Nob, a cidade dos padres, com o fio da espada - ambos homens e mulheres, crianças e bebês lactantes, e gado, burros e ovelhas, com o fio da espada.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
Um dos filhos de Ahimelech, o filho de Ahitub, chamado Abiathar, escapou e fugiu atrás de David.
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
Abiathar disse a David que Saul havia matado os sacerdotes de Yahweh.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
David disse a Abiathar: “Eu sabia naquele dia, quando Doeg, o Edomita, estava lá, que ele certamente diria a Saul. Eu sou responsável pela morte de todas as pessoas da casa de seu pai”.
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Fique comigo. Não tenha medo, pois aquele que procura minha vida procura a sua vida. Você estará a salvo comigo”.

< 1 Samweli 22 >