< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
Or David partit de là, et se sauva dans la caverne d'Hadullam; ce que ses frères et toute la maison de son père ayant appris, ils descendirent là vers lui.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
Tous ceux aussi qui étaient mal dans leurs affaires, et qui avaient des créanciers [dont ils étaient tourmentés], et qui avaient le cœur plein d'amertume, s'assemblèrent vers lui, et il fut leur chef; et il y eut avec lui environ quatre cents hommes.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
Et David s'en alla de là à Mitspé de Moab; et il dit au Roi de Moab: Je te prie que mon père et ma mère se retirent vers vous jusqu'à ce que je sache ce que Dieu fera de moi.
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
Et il les amena devant le Roi de Moab, et ils demeurèrent avec lui, tout le temps que David fut dans cette forteresse.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
Or Gad le prophète dit à David: Ne demeure point dans cette forteresse, [mais] va-t'en, et entre dans le pays de Juda. David donc s'en alla, et vint en la forêt de Hérets.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
Et Saül apprit qu'on avait découvert David et les gens qui étaient avec lui. Or Saül était assis au coteau sous un chêne à Rama, ayant sa hallebarde en sa main, et tous ses serviteurs se tenaient devant lui.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
Et Saül dit à ses serviteurs qui se tenaient devant lui: Ecoutez maintenant, Benjamites: Le fils d'Isaï vous donnera-t-il à vous tous des champs et des vignes? Vous établira-t-il tous gouverneurs sur milliers, et sur centaines?
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
Que vous ayez tous conspiré contre moi, et qu'il n'y ait personne qui m'avertisse que mon fils a fait alliance avec le fils d'Isaï, et qu'il n'y ait aucun de vous qui ait pitié de moi, et qui m'avertisse; car mon fils a suscité mon serviteur contre moi pour me dresser des embûches, comme il paraît aujourd'hui.
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Alors Doëg Iduméen, qui était établi sur les serviteurs de Saül, répondit, et dit: J'ai vu le fils d'Isaï venir à Nob vers Ahimélec fils d'Ahitub;
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
Qui a consulté l'Eternel pour lui, et lui a donné des vivres, et l'épée de Goliath le Philistin.
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Alors le Roi envoya appeler Ahimélec le Sacrificateur fils d'Ahitub, et toute la famille de son père, [savoir] les Sacrificateurs qui étaient à Nob; et ils vinrent tous vers le Roi.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
Et Saül dit: Ecoute maintenant, fils d'Ahitub; et il répondit: Me voici, mon Seigneur.
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
Alors Saül lui dit: Pourquoi avez-vous conspiré contre moi, toi et le fils d'Isaï, vu que tu lui as donné du pain, et une épée, et que tu as consulté Dieu pour lui, afin qu'il s'élevât contre moi pour me dresser des embûches, comme il paraît aujourd'hui.
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
Et Ahimélec répondit au Roi, et dit: Entre tous tes serviteurs y en a-t-il un comme David, qui est fidèle, et gendre du Roi, et qui est parti par ton commandement, et qui est si honoré en ta maison?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Ai-je commencé aujourd'hui à consulter Dieu pour lui? A Dieu ne plaise! Que le Roi ne charge donc d'aucune chose son serviteur, ni toute la maison de mon père; car ton serviteur ne sait chose ni petite ni grande de tout ceci.
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
Et le Roi lui dit: Certainement tu mourras, Ahimélec, et toute la famille de ton père.
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
Alors le Roi dit aux archers qui se tenaient devant lui: Tournez-vous, et faites mourir les Sacrificateurs de l'Eternel; car ils sont aussi de la faction de David parce qu'ils ont bien su qu'il s'enfuyait, et qu'ils ne m'en ont point averti. Mais les serviteurs du Roi ne voulurent point étendre leurs mains, pour se jeter sur les Sacrificateurs de l'Eternel.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
Alors le Roi dit à Doëg: Tourne-toi, et te jette sur les Sacrificateurs; et Doëg Iduméen se tourna, et se jeta sur les Sacrificateurs; et il tua en ce jour-là quatre vingt cinq hommes qui portaient l'Ephod de lin.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
Et il fit passer Nob, ville des Sacrificateurs, au fil de l'épée, les hommes et les femmes, les grands et ceux qui tètent, même [il fit passer] les bœufs, les ânes, et le menu bétail au fil de l'épée.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
Toutefois un des fils d'Ahimélec, fils d'Ahitub, qui avait nom Abiathar, se sauva, et s'enfuit auprès de David.
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
Et Abiathar rapporta à David, que Saül avait tué les Sacrificateurs de l'Eternel.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
Et David dit à Abiathar: Je connus bien en ce jour-là, puisque Doëg Iduméen était là, qu'il ne manquerait pas de le rapporter à Saül; je suis cause [de ce qui est arrivé] à toutes les personnes de la famille de ton père.
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Demeure avec moi, ne crains point; car celui qui cherche ma vie, cherche la tienne; certainement tu seras gardé avec moi.

< 1 Samweli 22 >