< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
David partit donc de là et se réfugia dans la caverne d'Adullam. Ses frères et toute la maison de son père l'apprirent, et ils descendirent auprès de lui.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
Tous ceux qui étaient dans la détresse, tous ceux qui avaient des dettes et tous ceux qui étaient mécontents se rassemblèrent auprès de lui, et il devint leur chef. Il y avait avec lui environ quatre cents hommes.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
David se rendit de là à Mitspé de Moab, et il dit au roi de Moab: « Laisse sortir vers toi mon père et ma mère, jusqu'à ce que je sache ce que Dieu fera pour moi. »
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
Il les amena devant le roi de Moab, et ils habitèrent avec lui tout le temps que David fut dans la forteresse.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
Le prophète Gad dit à David: « Ne reste pas dans la forteresse. Pars, et va dans le pays de Juda. » David partit, et arriva dans la forêt de Hereth.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
Saül apprit que David avait été découvert, avec les hommes qui étaient avec lui. Saül était assis à Guibea, sous le tamaris de Rama, sa lance à la main, et tous ses serviteurs se tenaient autour de lui.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
Saül dit à ses serviteurs qui se tenaient autour de lui: « Écoutez, Benjamites! Le fils de Jessé donnera-t-il à chacun de vous des champs et des vignes? Vous établira-t-il tous chefs de milliers et chefs de centaines?
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
Est-ce pour cela que vous avez tous conspiré contre moi, et qu'il n'y a personne qui me dise que mon fils a conclu un traité avec le fils d'Isaï, et qu'il n'y a aucun d'entre vous qui ait pitié de moi, ou qui me dise que mon fils a excité mon serviteur contre moi, pour le mettre à l'affût, comme c'est le cas aujourd'hui? »
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Alors Doëg, l'Edomite, qui se tenait près des serviteurs de Saül, prit la parole et dit: « J'ai vu le fils d'Isaï venir à Nob, chez Ahimélec, fils d'Ahitub.
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
Il a consulté Yahvé à son sujet, lui a donné à manger et lui a remis l'épée de Goliath le Philistin. »
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Alors le roi envoya appeler le prêtre Achimélec, fils d'Achitub, et toute la maison de son père, les prêtres qui étaient à Nob; et ils vinrent tous auprès du roi.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
Saül dit: « Écoute maintenant, fils d'Achitub. » Il a répondu: « Me voici, mon seigneur. »
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
Saül lui dit: « Pourquoi avez-vous conspiré contre moi, vous et le fils d'Isaï, en lui donnant du pain et une épée, et en demandant à Dieu pour lui, afin qu'il se lève contre moi, pour me guetter, comme il le fait aujourd'hui? »
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
Achimélec prit la parole devant le roi et dit: « Qui, parmi tous tes serviteurs, est aussi fidèle que David, gendre du roi, chef de ta garde et honoré dans ta maison?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Ai-je aujourd'hui commencé à demander à Dieu de le faire? Que cela soit loin de moi! Que le roi n'impute rien à son serviteur, ni à toute la maison de mon père, car ton serviteur n'a rien su de tout cela, ni en moins ni en plus. »
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
Le roi dit: « Tu mourras, Achimélec, toi et toute la maison de ton père. »
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
Le roi dit aux gardes qui se tenaient autour de lui: « Tournez et tuez les prêtres de l'Éternel, car leur main est aussi avec David, et parce qu'ils savaient qu'il s'était enfui et ne me l'ont pas révélé. » Mais les serviteurs du roi ne voulurent pas étendre leur main pour tomber sur les prêtres de Yahvé.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
Le roi dit à Dœg: « Retourne-toi et attaque les prêtres! » Dœg, l'Edomite, se retourna et attaqua les prêtres, et il tua en ce jour quatre-vingt-cinq personnes qui portaient un éphod de lin.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
Il frappa Nob, la ville des prêtres, du tranchant de l'épée: hommes et femmes, enfants et nourrissons, bétail, ânes et moutons, du tranchant de l'épée.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
L'un des fils d'Ahimélec, fils d'Ahitub, nommé Abiathar, s'échappa et s'enfuit après David.
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
Abiathar raconta à David que Saül avait tué les prêtres de l'Éternel.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
David dit à Abiathar: « Je savais que ce jour-là, lorsque Dœg l'Édomite était là, il ne manquerait pas de dire à Saül. Je suis responsable de la mort de toutes les personnes de la maison de ton père.
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Reste avec moi. N'aie pas peur, car celui qui cherche ma vie cherche ta vie. Tu seras en sécurité avec moi. »

< 1 Samweli 22 >