< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
And David goeth thence, and is escaped unto the cave of Adullam, and his brethren hear, and all the house of his father, and go down unto him thither;
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
and gather themselves unto him do every man in distress, and every man who hath an exactor, and every man bitter in soul, and he is over them for head, and there are with him about four hundred men.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
And David goeth thence to Mizpeh of Moab, and saith unto the king of Moab, 'Let, I pray thee, my father and my mother go out with you, till that I know what God doth for me;'
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
and he leadeth them before the king of Moab, and they dwell with him all the days of David's being in the fortress.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
And Gad the prophet saith unto David, 'Thou dost not abide in a fortress, go, and thou hast entered for thee the land of Judah;' and David goeth and entereth the forest of Hareth.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
And Saul heareth that David hath become known, and the men who [are] with him, and Saul is abiding in Gibeah, under the grove in Ramah, and his spear [is] in his hand, and all his servants standing by him.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
And Saul saith to his servants who are standing by him, 'Hear, I pray you, ye Benjamites; also to all of you doth the son of Jesse give fields and vineyards! all of you he doth appoint heads of thousands and heads of hundreds!
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
for ye have conspired all of you against me, and there is none uncovering mine ear about my son's covenanting with the son of Jesse, and there is none of you grieving for me, and uncovering mine ear, that my son hath raised up my servant against me, to lie in wait as [at] this day.'
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
And answer doth Doeg the Edomite, who is set over the servants of Saul, and saith, 'I have seen the son of Jesse coming in to Nob, unto Ahimelech son of Ahitub,
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
and he asketh for him at Jehovah, and provision hath given to him, and the sword of Goliath the Philistine hath given to him.
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
And the king sendeth to call Ahimelech son of Ahitub, the priest, and all the house of his father, the priests, who [are] in Nob, and they come all of them unto the king;
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
and Saul saith, 'Hear, I pray thee, son of Ahitub;' and he saith, 'Here [am] I, my lord.'
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
And Saul saith unto him, 'Why have ye conspired against me, thou and the son of Jesse, by thy giving to him bread and a sword, and to ask for him at God, to rise against me, to lie in wait, as [at] this day?'
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
And Ahimelech answereth the king and saith, 'And who among all thy servants [is] as David — faithful, and son-in-law of the king, and hath turned aside unto thy council, and is honoured in thy house?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
To-day have I begun to ask for him at God? far be it from me! let not the king lay anything against his servant, against any of the house of my father, for thy servant hath known nothing of all this, less or more.'
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
And the king saith, 'Thou dost surely die, Ahimelech, thou, and all the house of thy father.'
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
And the king saith to runners, those standing by him, 'Turn round, and put to death the priests of Jehovah, because their hand also [is] with David, and because they have known that he is fleeing, and have not uncovered mine ear;' and the servants of the king have not been willing to put forth their hand to come against the priests of Jehovah.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
And the king saith to Doeg, 'Turn round thou, and come against the priests;' and Doeg the Edomite turneth round, and cometh himself against the priests, and putteth to death in that day eighty and five men bearing a linen ephod,
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
and Nob, the city of the priests, he hath smitten by the mouth of the sword, from man even unto woman, from infant even unto suckling, and ox, and ass, and sheep, by the mouth of the sword.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
And there escapeth one son of Ahimelech, son of Ahitub, and his name [is] Abiathar, and he fleeth after David,
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
and Abiathar declareth to David that Saul hath slain the priests of Jehovah.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
And David saith to Abiathar, 'I have known on that day when Doeg the Edomite [is] there, that he doth certainly declare [it] to Saul; I have brought [it] round to every person of the house of thy father;
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
dwell with me; fear not; for he who seeketh my life seeketh thy life; for a charge [art] thou with me.'

< 1 Samweli 22 >