< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
Therfor Dauid yede fro thennus, and fledde in to the denne of Odollam; and whanne hise britheren, and al the hows of his fadir hadden herd this, thei camen doun thidur to hym.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
And alle men that weren set in angwisch, and oppressid with othere mennus dette, and in bittir soule, camen togidere to hym; and he was maad the prince `of hem, and as foure hundrid men weren with hym.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
And Dauid yede forth fro thennus in to Masphat, which is of Moab; and he seide to the kyng of Moab, Y preye, dwelle my fadir and my modir with you, til Y wite what thing God schal do to me.
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
And he lefte hem bifor the face of the kyng of Moab; and thei dwelliden at hym in alle daies, `in whiche Dauid was in `the forselet, ether stronghold.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
And Gad, the profete, seide to Dauid, Nyle thou dwelle in `the forselet; go thou forth, and go in to the lond of Juda. And Dauid yede forth, and cam in to the forest of Areth.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
And Saul herde, that Dauid apperide, and the men that weren with hym. Forsothe whanne Saul dwellide in Gabaa, and was in the wode which is in Rama, and `helde a spere in the hond, and alle hise seruauntis stoden aboute hym,
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
he seide to hise seruauntis that stoden nyy hym, The sones of Gemyny, here me now; whether the sone of Ysai schal yyue to alle you feeldis and vyneris, and schal make alle you tribunes and centuriouns?
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
For alle ye han swore, ether conspirid, togidere ayens me, and noon is that tellith to me; moost sithen also my sone hath ioyned boond of pees with the sone of Ysai; noon is of you, that sorewith `for my stide, nether that tellith to me, for my sone hath reisid my seruaunt ayens me, settynge tresoun to me `til to dai.
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Sotheli Doech of Ydumye answeride, that stood nyy, and was the firste among `the seruauntis of Saul, and seide, Y siy `the sone of Ysai in Nobe, at Achymelech, preest, the sone of Achitob;
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
which counseilide the Lord for Dauid, and yaf meetis `to hym, but also he yaf to Dauid the swerd of Goliath Filistei.
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Therfor the kyng sente to clepe Achymelech, the preest, `the sone of Achitob, and al the hows of his fadir, of preestis that weren in Nobe; whiche alle camen to the kyng.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
And Saul seide to Achymelech, Here, thou sone of Achitob.
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
Which answeride, Lord, Y am redi. And Saul seide to hym, Whi hast thou conspirid ayens me, thou, and the sone of Ysai, and yauest looues and a swerd to hym, and councelidist the Lord for hym, that he schulde rise ayens me, and he dwellith a tretour `til to dai?
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
And Achymelech answeride to the kyng, and seide, And who among alle thi seruauntis is as Dauid feithful, and the sone in lawe `of the kyng, and goynge at thi comaundement, and gloriouse in thin hows?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Whether Y bigan to dai to counsele the Lord for hym? Fer be this fro me; suppose not the kyng ayens his seruaunt `siche a thing in al `the hows of my fadir; for thi seruaunt knew not ony thing, ether litil ethir greet, of this cause.
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
And the kyng seide, Achymelech, thou schalt die bi deeth, thou, and al the hows of thi fadir.
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
And the kyng seide to men able to be sent out, that stoden aboute hym, Turne ye, and sle the preestis of the Lord, for the hond of hem is with Dauid; and thei wisten that he fledde, and thei schewiden not to me. Sotheli the seruauntis of the kyng nolden holde forth her hond in to the preestis of the Lord.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
And the kyng seide to Doech, Turne thou, and hurle in to the preestis of the Lord. And Doech of Ydumee turnede, and hurlide in to the preestis, and stranglide in that dai foure score and fyue men, clothid with `ephoth of lynnun cloth.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
Forsothe he smoot Nobe, the citee of preestis, by the scharpnesse of swerd, men and wymmen, litle children and soukynge, and oxe, and asse, and sheep, bi the scharpnesse of swerd.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
Forsothe o sone of Achymelech, sone of Achitob, ascapide, of which sone the name was Abiathar; and he fledde to Dauid,
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
and telde to hym that Saul hadde slayn the preestis of the Lord.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
And Dauid seide to Abiathar, Sotheli Y wiste, `that is, Y coniectide, ether dredde, in that dai, that whanne Doech of Ydumee was there, he wolde telle with out doute to Saul; Y am gilti of alle the lyues of thi fadir.
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Dwelle thou with me, drede thou not; if ony man sekith thi lijf, he schal seke also my lijf, and thou schalt be kept with me.

< 1 Samweli 22 >