< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
David therefore went from thence and fled to the cave of Odollam. And when his brethren, and all his father’s house had heard of it, they went down to him thither;
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
And all that were in distress and oppressed with debt, and under affliction of mind gathered themselves unto him: and he became their prince, and there were with him about four hundred men.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
And David departed from thence into Maspha of Moab: and he said to the king of Moab: Let my father and my mother tarry with you, I beseech thee, till I know what God will do for me.
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
And he left them under the eyes of the king of Moab, and they abode with him all the days that David was in the hold.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
And Gad the prophet said to David: Abide not in the hold, depart, and go into the land of Juda. And David departed, and came into the forest of Haret.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
And Saul heard that David was seen, and the men that were with him. Now whilst Saul abode in Gabaa, and was in the wood, which is by Rama, having his spear in his hand, and all his servants were standing about him,
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
He said to his servants that stood about him: Hear me now, ye sons of Jemini: will the son of Isai give everyone of you fields, and vineyards, and make you all tribunes, and centurions:
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
That all of you have conspired against me, and there is no one to inform me, especially when even my son hath entered into league with the soil of Isai? There is not one of you that pitieth my case, nor that giveth me any information: because my son hath raised up my servant against me, plotting against me to this day.
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
And Doeg the Edomite who stood by, and was the chief among the servants of Saul, answering, said: I saw the son of Isai, in Nobe with Achimelech the son of Achitob the priest.
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
And he consulted the Lord for him, and gave him victuals, and gave him the sword of Goliath the Philistine.
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
Then the king sent to call for Achimelech the priest the son of Achitob, and all his father’s house, the priests that were in Nobe, and they came all of them to the king.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
And Saul said to Achimelech: Hear, thou son of Achitob. He answered: Here I am, my lord.
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
And Saul said to him: Why have you conspired against me, thou, and the son of Isai, and thou hast given him bread and a sword, and hast consulted the Lord for him, that he should rise up against me, continuing a traitor to this day.
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
And Achimelech answering the king, said: And who amongst all thy servants is so faithful as David, who is the king’s son in law, and goeth forth at thy bidding, and is honourable in thy house?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Did I begin today to consult the Lord for him? far be this from me: let not the king suspect such a thing against his servant, or any one in all my father’s house: for thy servant knew nothing of this matter, either little or great.
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
And the king said: Dying thou shalt die, Achimelech, thou and all thy father’s house.
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
And the king said to the messengers that stood about him: Turn, and kill the priests of the Lord, for their hand is with David, because they knew that he was fled, and they told it not to me. And the king’s servants would not put forth their hands against the priests of the Lord.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
And the king said to Doeg: Turn thou, and fall upon the priests. And Doeg the Edomite turned, and fell upon the priests and slew in that day eighty-five men that wore the linen ephod.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
And Nobe the city of the priests he smote with the edge of his sword, both men and women, children, and sucklings, and ox and ass, and sheep with the edge of the sword.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
But one of the sons of Achimelech the son of Achitob, whose name was Abiathar, escaped, and fled to David,
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
And told him that Saul had slain the priests of the Lord.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
And David said to Abiathar: I knew that day when Doeg the Edomite was there, that without doubt he would tell Saul: I have been the occasion of the death of all the souls of thy father’s house.
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Abide thou with me, fear not: for he that seeketh my life, seeketh thy life also, and with me thou shalt be saved.

< 1 Samweli 22 >