< 1 Samweli 22 >

1 Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
A tak odšel odtud David, skryl se v jeskyni Adulam. To když uslyšeli bratří jeho i všecken dům otce jeho, sešli se tam k němu.
2 Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
A shromáždili se k němu, kteřížkoli byli v ssoužení, a kteřížkoli byli zadlužilí, a kteřížkoli byli v hořkosti ducha, a byl nad nimi knížetem, tak že jich bylo s ním okolo čtyř set mužů.
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
Potom odšel odtud David do Masfa Moábského a řekl králi Moábskému: Prosím, nechť vcházejí k vám i vycházejí otec můj a matka má, dokudž nezvím, co se mnou učiní Bůh.
4 Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
I přivedl je před krále Moábského, a bydlili s ním po všecky dny, v nichž zůstával David na tom hradě.
5 Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
Ale prorok Gád řekl Davidovi: Nebývejž déle na tom hradě, jdi, navrať se do země Judské. I odšel David, a přišel do lesa Haret.
6 Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
V tom uslyšel Saul, že by se zjevil David i muži, kteříž byli s ním. Saul pak bydlil v Gabaa pod hájem v Ráma, maje kopí své v rukou svých, a všickni služebníci jeho stáli před ním.
7 Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
I řekl Saul služebníkům svým, kteříž stáli před ním: Slyšte medle, synové Jemini: Všechněm-li vám dá syn Izai pole a vinice? Všecky-li vás postaví za správce nad tisíci a sty,
8 Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
Že jste se všickni spikli proti mně, aniž jest, kdo by mi oznámil? Již i syn můj učinil smlouvu s synem Izai, a však žádný z vás nelituje mne, aniž mi kdo oznámí, že pozdvihl syn můj služebníka mého proti mně, aby mi zálohy strojil, jakož se to již děje.
9 Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
Odpověděl pak Doeg Idumejský, kterýž též stál s služebníky Saulovými, a řekl: Viděl jsem syna Izai, an přišel do Nobe k Achimelechovi synu Achitobovu.
10 Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
Kterýž radil se o něho s Hospodinem a dal jemu potravy, také i meč Goliáše Filistinského dal jemu.
11 Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
I poslal král, aby zavolali Achimelecha syna Achitobova, kněze, i vší čeledi otce jeho, totiž kněží, kteříž byli v Nobe. I přišli všickni před krále.
12 Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
Tedy řekl Saul: Slyš nyní, synu Achitobův. Kterýž odpověděl: Ej, pane můj.
13 Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
I dí k němu Saul: Proč jste se spikli proti mně, ty a syn Izai, když jsi jemu dal chléb a meč, a radils se s Bohem o něj, aby povstal proti mně k strojení mi záloh, jakož se to již děje?
14 Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
Odpovídaje Achimelech králi, řekl: A kdo jest tak věrný ze všech služebníků tvých jako David, kterýž i zetěm královým jest, kterýž kráčí v poslušenství tvém, a vzácný jest v domě tvém?
15 Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
Zdaliž jsem se nyní počal tázati Boha o něj? Odstup to ode mne. Nesčítejž král takové věci na služebníka svého, ani na koho z čeledi otce mého, neboť neví služebník tvůj o ničemž o tom ani nejmenší věci.
16 Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
Ale král řekl: Smrtí umřeš Achimelechu, ty i všecken dům otce tvého.
17 Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
I řekl král drabantům, kteříž stáli před ním: Obraťte se a zbíte kněží Hospodinovy, nebo i jejich ruka jest s Davidem; přes to vědouce, že utíká, nedali mi znáti. Služebníci však královští nechtěli vztáhnouti rukou svých, ani se obořiti na kněží Hospodinovy.
18 Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
A protož řekl král Doegovi: Obrať ty se, a pobí ty kněží. Takž Doeg Idumejský obrátiv se, obořil se na kněží, a zbil toho dne osmdesáte a pět mužů, kteříž nosili efod lněný.
19 Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
Nobe také město kněžské vyhubil ostrostí meče, od muže až do ženy, od malého až do požívajícího prsí, voly i osly, i dobytky pobil ostrostí meče.
20 Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
Jediný toliko syn Achimelechův, syna Achitobova, jehož jméno bylo Abiatar, ušel a utekl k Davidovi.
21 Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
Tedy oznámil Abiatar Davidovi, že Saul zmordoval kněží Hospodinovy.
22 Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
I řekl David Abiatarovi: Vědělť jsem toho dne, když tam byl Doeg Idumejský, že jistotně oznámí Saulovi; jáť jsem přičinu dal k zhubení všech duší domu otce tvého.
23 Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”
Zůstaň u mne, neboj se; nebo kdož hledati bude bezživotí mého, hledati bude bezživotí tvého, ale ochráněn budeš u mne.

< 1 Samweli 22 >