< 1 Samweli 2 >

1 Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
Wtedy Anna modliła się i powiedziała: Moje serce raduje się w PANU, mój róg jest wywyższony w PANU. Moje usta szeroko otworzyły się przeciwko moim wrogom, gdyż raduję się z twego zbawienia.
2 “Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
Nikt nie jest tak święty jak PAN. Nie ma bowiem nikogo oprócz ciebie i nikt nie jest taką skałą jak nasz Bóg.
3 “Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
Nie mówcie już pysznych słów i niech z waszych ust nie wychodzą słowa wyniosłe. PAN bowiem [jest] Bogiem wiedzy, on waży czyny.
4 “Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
Łuki mocarzy [zostały] złamane, a słabi są przepasani mocą.
5 Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
Syci najmują się za chleb, a głodni przestali [głodować]. Nawet niepłodna urodziła siedmioro, a wielodzietna więdnie.
6 “Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol h7585)
PAN zabija i ożywia, wprowadza do grobu i wyprowadza. (Sheol h7585)
7 Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
PAN czyni ubogim i bogatym, poniża i wywyższa.
8 Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
Podnosi z prochu ubogiego, a z gnoju podnosi żebraka, by posadzić ich z książętami i pozwolić im odziedziczyć tron chwały. Do PANA bowiem należą filary ziemi, na nich osadził świat.
9 Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
Strzeże stóp swych świętych, a bezbożni zamilkną w ciemności, bo nie swoją siłą zwycięży człowiek.
10 wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
PAN pokruszy swoich przeciwników i zagrzmi przeciwko nim z nieba. PAN będzie sądził krańce ziemi, udzieli siły swemu królowi i wywyższy róg swego pomazańca.
11 Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
Potem Elkana wrócił do Rama, do swego domu, a dziecko służyło PANU przy kapłanie Helim.
12 Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
Lecz synowie Heliego byli synami Beliala i nie znali PANA.
13 Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
Był bowiem taki zwyczaj kapłanów wobec ludu: kiedy ktoś składał ofiarę, sługa kapłana przychodził, gdy mięso się gotowało, z trójzębnymi widelcami w ręce.
14 Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
I wkładał je do garnka, kotła, rondla lub misy i to, co wyjął widełkami, kapłan zabierał dla siebie. Tak czynili w Szilo wszystkim Izraelitom, którzy tam przychodzili.
15 Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
Ponadto, zanim jeszcze spalono tłuszcz, przychodził sługa kapłana i mówił do człowieka składającego ofiary: Daj mięso na pieczeń dla kapłana, bo nie weźmie on od ciebie mięsa gotowanego, tylko surowe.
16 Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
A jeśli taki człowiek mu odpowiedział: Niech najpierw spalą tłuszcz, a potem weź sobie, czego pragnie twoja dusza, wtedy on mówił: Nic z tego! Daj teraz! A jeśli nie dasz, zabiorę siłą.
17 Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
Tak więc grzech tych sług był bardzo wielki przed PANEM, gdyż ludzie lekceważyli ofiary PANA.
18 Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
Samuel zaś służył przed PANEM jako chłopiec, przepasany lnianym efodem.
19 Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
A jego matka robiła mu mały płaszcz i przynosiła mu [go] co roku, gdy chodziła z mężem składać doroczną ofiarę.
20 Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
I Heli błogosławił Elkanie i jego żonie, mówiąc: Niech PAN da ci potomstwo z tej kobiety za uproszonego, którego oddała PANU. I wracali do swojego domu.
21 Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
I PAN nawiedził Annę, a ona poczęła i urodziła trzech synów i dwie córki. A chłopiec Samuel dorastał przed PANEM.
22 Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
Heli zaś bardzo się zestarzał i usłyszał o wszystkim, co jego synowie czynili wobec całego Izraela, oraz o tym, że obcowali z kobietami, które się zbierały przy wejściu do Namiotu Zgromadzenia.
23 Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
I powiedział do nich: Dlaczego czynicie takie rzeczy? Słyszę o waszych złych czynach od całego ludu.
24 Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
Nie, moi synowie, gdyż niedobra to wieść, którą słyszę. Doprowadzacie lud PANA do przestępstwa.
25 Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
Jeśli człowiek zgrzeszy przeciw człowiekowi, będzie go sądzić sędzia, ale jeśli człowiek zgrzeszy przeciw PANU, któż się za nim wstawi? Oni jednak nie posłuchali głosu swego ojca, bo PAN chciał ich zabić.
26 Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
A chłopiec Samuel rósł i podobał się zarówno PANU, jak i ludziom.
27 Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
Potem przyszedł mąż Boży do Heliego i powiedział mu: Tak mówi PAN: Czy nie objawiłem się wyraźnie domowi twego ojca, gdy byli w Egipcie w domu faraona?
28 Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
I wybrałem go sobie spośród wszystkich pokoleń Izraela na kapłana, aby składał ofiary na moim ołtarzu, palił kadzidło i nosił efod przede mną. Dałem też domowi twego ojca wszystkie ofiary ogniowe od synów Izraela.
29 Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
Dlaczego podeptaliście moją ofiarę krwawą i pokarmową, które rozkazałem [składać] w przybytku? Dlaczego [bardziej] uczciłeś swoich synów ode mnie, abyście utuczyli się z pierwocin wszystkich ofiar pokarmowych Izraela, mojego ludu?
30 “Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
Dlatego PAN, Bóg Izraela, mówi: Wprawdzie powiedziałem: Twój dom i dom twego ojca będzie chodzić przede mną na wieki, ale teraz PAN mówi: Nie będzie tak! Tych bowiem, którzy mnie czczą, ja będę czcić, a ci, którzy mną gardzą, będą wzgardzeni.
31 Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
Oto nadchodzą dni, gdy odetnę twe ramię i ramię domu twego ojca, aby już nie było starca w twoim domu;
32 nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
I zobaczysz przeciwnika w przybytku, wśród całego szczęścia, którego Bóg udzieli Izraelowi, i nie będzie starca w twoim domu po wszystkie dni.
33 Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
Lecz nie wytracę od swego ołtarza każdego człowieka spośród ciebie, aby trapić twe oczy i ścisnąć boleścią twoją duszę. Cały przyrost twego domu umrze w sile wieku.
34 “‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
A to będzie znakiem, który przyjdzie na twoich dwóch synów, Chofniego i Pinchasa: obydwaj umrą tego samego dnia.
35 Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
I wzbudzę sobie kapłana wiernego, [który] będzie postępował według mego serca i mojej myśli. Zbuduję mu trwały dom, a on będzie chodził przed moim pomazańcem po wszystkie dni.
36 Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”
I stanie się tak, że ktokolwiek pozostanie w twoim domu, ten przyjdzie i pokłoni mu się za srebrną monetę i za kawałek chleba, mówiąc: Dopuść mnie, proszę, do jednego z [urzędów] kapłańskich, abym mógł jeść kawałek chleba.

< 1 Samweli 2 >