< 1 Wafalme 14 >

1 Wakati ule Abiya mwana wa Yeroboamu akaugua,
W tym czasie zachorował Abiasz, syn Jeroboama.
2 naye Yeroboamu akamwambia mke wake, “Nenda ukajibadilishe, ili watu wasijue kwamba wewe ni mke wa Yeroboamu. Kisha uende Shilo. Nabii Ahiya yuko huko, yule aliyeniambia kuwa nitakuwa mfalme juu ya watu hawa.
I Jeroboam powiedział do swojej żony: Wstań teraz, przebierz się, aby nie poznano, że jesteś żoną Jeroboama, i idź do Szilo. [Jest] tam prorok Achiasz, który mi powiedział, że będę królem nad tym ludem.
3 Chukua mikate kumi, maandazi kadhaa na gudulia la asali na umwendee. Atakuambia kitakachotokea kwa kijana.”
Weź ze sobą dziesięć chlebów, placki i dzban miodu i idź do niego. On ci oznajmi, co się stanie z dzieckiem.
4 Basi mke wa Yeroboamu akafanya kama alivyosema mumewe, akaenda kwenye nyumba ya Ahiya huko Shilo. Wakati huu Ahiya alikuwa kipofu naye alishindwa kuona kwa sababu ya umri wake.
Żona Jeroboama tak uczyniła. Wstała i poszła do Szilo, i przybyła do domu Achiasza. Lecz Achiasz już nie widział, gdyż jego oczy osłabły z powodu jego starości.
5 Lakini Bwana alikuwa amemwambia Ahiya, “Mke wa Yeroboamu anakuja kukuuliza kuhusu mwanawe, kwa kuwa ni mgonjwa, nawe utamjibu hivi na hivi. Atakapowasili, atajifanya kuwa ni mtu mwingine.”
A PAN powiedział do Achiasza: Oto żona Jeroboama nadchodzi, aby dowiedzieć się czegoś od ciebie o swoim synu, gdyż jest chory. Powiesz jej tak i tak, bo gdy wejdzie, będzie udawała kogoś innego.
6 Hivyo Ahiya aliposikia kishindo cha hatua zake mlangoni, akasema, “Karibu ndani, mke wa Yeroboamu. Kwa nini kujibadilisha? Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya.
Gdy więc Achiasz usłyszał odgłos jej kroków, gdy wchodziła przez drzwi, powiedział: Wejdź, żono Jeroboama. Dlaczego udajesz kogoś innego? Zostałem posłany do ciebie z przykrą nowiną.
7 Nenda, ukamwambie Yeroboamu kwamba hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Nilikuinua miongoni mwa watu na kukufanya kiongozi juu ya watu wangu Israeli.
Idź, powiedz Jeroboamowi: Tak mówi PAN, Bóg Izraela: Mimo że wywyższyłem cię spośród ludu i ustanowiłem cię księciem nad moim ludem Izraelem;
8 Nikararua ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupa wewe, lakini hukuwa kama mtumishi wangu Daudi, ambaye aliyashika maagizo yangu na kunifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu lile lililokuwa sawa machoni pangu.
Wyrwałem domowi Dawida królestwo i dałem je tobie, ty jednak nie byłeś jak mój sługa Dawid, który przestrzegał moich przykazań i który chodził za mną całym swym sercem, czyniąc tylko to, co jest prawe w moich oczach;
9 Umefanya maovu mengi kuliko wote waliokutangulia. Umejitengenezea miungu mingine, sanamu za chuma, umenighadhibisha na kunitupa nyuma yako.
Lecz postępowałeś gorzej niż wszyscy, którzy byli przed tobą. Ty bowiem poszedłeś i uczyniłeś sobie obcych bogów i odlane posągi, aby mnie pobudzić do gniewu, mnie zaś rzuciłeś za plecy.
10 “‘Kwa sababu ya hili, nitaleta maafa juu ya nyumba ya Yeroboamu. Nitakatilia mbali kutoka kwa Yeroboamu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, mtumwa au mtu huru. Nitachoma nyumba ya Yeroboamu mpaka iteketee yote kama mtu achomaye kinyesi.
Dlatego sprowadzę nieszczęście na dom Jeroboama i wytępię z Jeroboama każdego, aż do najmniejszego szczenięcia, każdego więźnia i opuszczonego w Izraelu, i usunę ostatki domu Jeroboama, jak usuwa się gnój, aż do końca.
11 Mbwa watawala wale walio wa nyumba ya Yeroboamu watakaofia ndani ya mji na ndege wa angani watajilisha kwa wale watakaofia mashambani. Bwana amesema!’
Tego, kto [z domu] Jeroboama umrze w mieście, zjedzą psy, a tego, kto umrze na polu, zjedzą powietrzne ptaki, ponieważ tak powiedział PAN.
12 “Kukuhusu wewe, rudi nyumbani. Wakati utakapotia mguu katika mji wako, kijana atakufa.
Ty zaś wstań i idź do swego domu, [a] gdy wejdziesz do miasta, dziecko umrze.
13 Israeli yote itamwombolezea na kumzika. Kwa sababu ni yeye pekee wa nyumba ya Yeroboamu atakayezikwa, kwa sababu ni yeye peke yake ndani ya nyumba ya Yeroboamu ambaye Bwana, Mungu wa Israeli, ameona kitu chema kwake.
I cały Izrael będzie je opłakiwał, i pogrzebie je, bo jedynie ono [z domu] Jeroboama zejdzie do grobu, gdyż w nim znalazło się [coś] dobrego względem PANA, Boga Izraela, w domu Jeroboama.
14 “Bwana atajiinulia mwenyewe mfalme juu ya Israeli ambaye ataikatilia mbali jamaa ya Yeroboamu. Siku ndiyo hii! Nini? Naam, hata sasa hivi.
PAN zaś ustanowi sobie króla nad Izraelem, który wytępi dom Jeroboama w tym samym dniu. A co [mówię, wzbudzi]? I owszem, już [wzbudził].
15 Naye Bwana ataipiga Israeli, hata iwe kama unyasi unaosukwasukwa juu ya maji. Ataingʼoa Israeli kutoka nchi hii nzuri aliyowapa baba zao na kuwatawanya ngʼambo ya Mto Frati, kwa sababu wamemghadhibisha Bwana kwa kutengeneza nguzo za Ashera
I PAN uderzy Izraela [tak], że [się zachwieje], jak się chwieje trzcina w wodzie, i wykorzeni Izraela z tej dobrej ziemi, którą dał ich ojcom, i rozproszy ich za rzeką za to, że uczynili sobie gaje, pobudzając PANA do gniewu.
16 Naye atawaacha Israeli kwa ajili ya makosa ya Yeroboamu aliyoyatenda na kusababisha Israeli kuyatenda.”
I tak porzuci on Izraela z powodu grzechów Jeroboama, który grzeszył i skłonił Izraela do grzechu.
17 Kisha mke wa Yeroboamu akainuka, akaondoka kwenda Tirsa. Mara alipokanyaga kizingiti cha mlango, kijana akafa.
Wtedy żona Jeroboama wstała, wyruszyła i przybyła do Tirsy. Gdy przekroczyła próg domu, dziecko umarło.
18 Wakamzika na Israeli yote ikamwombolezea, kama Bwana alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake, nabii Ahiya.
I pogrzebali je, i cały Izrael je opłakiwał zgodnie ze słowem PANA, które zapowiedział przez swego sługę, proroka Achiasza.
19 Matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, vita vyake na jinsi alivyotawala, vimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
Pozostałe zaś dzieje Jeroboama, jak walczył i jak królował, są zapisane w kronikach o królach Izraela.
20 Yeroboamu akawatawala kwa miaka ishirini na miwili, kisha akalala na baba zake. Naye Nadabu mwanawe akawa mfalme baada yake.
A czas, który królował Jeroboam, wynosił dwadzieścia dwa lata. Potem zasnął ze swoimi ojcami, a jego syn Nadab królował w jego miejsce.
21 Rehoboamu mwana wa Solomoni alikuwa mfalme wa Yuda. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na moja alipoanza kutawala, naye akatawala miaka kumi na saba huko Yerusalemu, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua kutoka makabila yote ya Israeli ili apate kuliweka humo Jina lake. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni.
Roboam zaś, syn Salomona, królował w Judzie. Roboam [miał] czterdzieści jeden lat, gdy zaczął królować, a królował siedemnaście lat w Jerozolimie, w mieście, które PAN wybrał spośród wszystkich pokoleń Izraela, aby tam przebywało jego imię. Jego matka miała na imię Naama, [była] Ammonitką.
22 Yuda wakatenda maovu machoni pa Bwana. Kwa dhambi walizotenda wakachochea hasira yake yenye wivu zaidi kuliko baba zao walivyofanya.
I Juda czynił to, co złe w oczach PANA, i swoimi grzechami, które popełniali, pobudzali go do zazdrości bardziej niż to wszystko, co czynili ich ojcowie.
23 Pia wakajijengea mahali pa juu pa kuabudia miungu, mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kilichoinuka na kila mti uliotanda.
Pobudowali sobie bowiem wyżyny, posągi i gaje na każdym wysokim wzgórzu i pod każdym zielonym drzewem.
24 Walikuwepo hata wanaume mahanithi wa mahali pa ibada za sanamu katika nchi; watu wakajiingiza katika kutenda machukizo ya mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
Byli też w tej ziemi sodomici. Postępowali oni według wszystkich obrzydliwości pogan, których PAN wypędził sprzed synów Izraela.
25 Katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu.
A w piątym roku króla Roboama, przeciw Jerozolimie nadciągnął Sziszak, król Egiptu.
26 Akachukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao zote za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
I zabrał skarby domu PANA oraz skarby domu królewskiego, zabrał wszystko. Zabrał też wszystkie złote tarcze, które wykonał Salomon.
27 Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
Zamiast nich król Roboam wykonał spiżowe tarcze i powierzył je dowódcy straży przybocznej, która strzegła drzwi domu królewskiego.
28 Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana, walinzi walizichukua hizo ngao, na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
Ilekroć król wchodził do domu PANA, straż je nosiła, a potem odnosiła do wartowni.
29 Kwa matukio mengine ya utawala wa Rehoboamu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
A pozostałe dzieje Roboama i wszystko, co czynił, czyż nie są zapisane w kronikach królów Judy?
30 Kulikuwa na vita vinavyoendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
I trwała wojna między Roboamem a Jeroboamem po wszystkie dni.
31 Naye Rehoboamu akalala na baba zake, na akazikwa pamoja nao katika Mji wa Daudi. Mama yake aliitwa Naama, ambaye alikuwa Mwamoni. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.
Potem Roboam zasnął ze swoimi ojcami i został pogrzebany z nimi w mieście Dawida. A jego matka miała na imię Naama, [była] Ammonitką. I jego syn Abijam królował w jego miejsce.

< 1 Wafalme 14 >