< 1 Nyakati 9 >

1 Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
Tak wszyscy Izraelici byli spisani w rodowodach, a oto zostały one zapisane w księdze królów Izraela i Judy, [a] ci zostali uprowadzeni do Babilonu z powodu swego przestępstwa.
2 Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
Pierwszymi mieszkańcami, którzy weszli do swych posiadłości w swoich miastach, byli Izraelici, kapłani, Lewici i Netinici.
3 Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
W Jerozolimie mieszkali spośród synów Judy, Beniamina, Efraima i Manassesa:
4 Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Utaj, syn Ammihuda, syna Omriego, syna Imriego, syna Baniego, z synów Peresa, syna Judy.
5 Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
Z Szilonitów: pierworodny Asajasz i jego synowie.
6 Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
Z synów Zeracha: Jeuel i ich braci, sześciuset dziewięćdziesięciu.
7 Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
Z synów Beniamina: Sallu, syn Meszullama, syna Hodawiasza, syna Hassenuy;
8 Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
I Jibnejasz, syn Jerochama, Ela, syn Uzziego, syna Mikriego, i Meszullam, syn Szefatiasza, syna Reuela, syna Jibniasza.
9 Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
Ich braci według rodowodów [było] dziewięćset pięćdziesięciu sześciu. Ci wszyscy [byli] naczelnikami rodów według domów swoich ojców.
10 Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
Z kapłanów: Jedajasz, Jehojarib, Jakin;
11 Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
I Azariasz, syn Chilkiasza, syna Meszullama, syna Sadoka, syna Merajota, syna Achituba, przełożonego domu Bożego;
12 Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
I Adajasz, syn Jerochama, syna Paszchura, syna Malkiasza, i Maasaj, syn Adiela, syna Jachzery, syna Meszullama, syna Meszillemita, syna Immera;
13 Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
Ich braci, naczelników swoich rodów, [było] tysiąc siedmiuset sześćdziesięciu, ludzi zdolnych do pełnienia służby w domu Bożym.
14 Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
A z Lewitów: Szemejasz, syn Chaszuba, syna Azrikama, syna Chaszabiasza, z synów Merariego;
15 Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
I Bakbakar, Cheresz, Galal, Mattaniasz, syn Micheasza, syna Zikriego, syna Asafa;
16 Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
I Obadiasz, syn Szemajasza, syna Galala, syna Jedutuna, i Berechiasz, syn Asy, syna Elkany, który mieszkał we wsiach Netofatytów.
17 Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
A odźwierni: Szallum, Akkub, Talmon, Achiman i ich bracia. Szallum [był ich] zwierzchnikiem;
18 Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
[Który] aż dotąd [stawał] przy bramie królewskiej od wschodu. Ci byli odźwiernymi w obozach synów Lewiego.
19 Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
Szallum, syn Korego, syna Ebiazafa, syna Koracha, i jego bracia z domu jego ojca, Korachici, pełnili służbę, [byli] stróżami progów namiotu, a ich ojcowie byli stróżami wejścia do obozu PANA.
20 Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
Pinchas, syn Eleazara, był niegdyś zwierzchnikiem nad nimi, a PAN był z nim.
21 Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
Zachariasz, syn Meszelemiasza, [był] odźwiernym przy wejściu do Namiotu Zgromadzenia.
22 Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
Wszystkich wybranych na odźwiernych przy bramach było dwustu dwunastu. Byli oni policzeni według ich rodowodu w swoich osiedlach, a ustanowił ich Dawid i Samuel, widzący.
23 Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
Oni więc i ich synowie [czuwali] nad bramami domu PANA, w domu namiotu, jako stróże.
24 Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
Odźwierni znajdowali się z czterech stron: od wschodu, od zachodu, od północy i od południa.
25 Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
Ich bracia zaś, [mieszkający] w swoich osiedlach, przychodzili co siódmy dzień, w swoich porach, aby [być] z nimi.
26 Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
Czterej bowiem naczelni odźwierni pełnili stałą służbę. [Byli] to Lewici [odpowiedzialni] za komnaty i skarbiec domu Bożego;
27 Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
I nocowali dokoła domu Bożego, gdyż do nich należała straż i obowiązek otwierania [go] każdego ranka.
28 Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
[Niektórzy] z nich mieli pieczę nad naczyniami do służby, by je wnosić i wynosić w tej samej liczbie.
29 Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
[Inni] spośród nich byli ustanowieni [do opieki] nad naczyniami i przyborami Miejsca Najświętszego – nad mąką pszenną, winem, oliwą, kadzidłem i wonnościami.
30 Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
A niektórzy z synów kapłanów sporządzali olejki z wonności.
31 Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
Mattitiasz, spośród Lewitów, pierworodny Szalluma Korachity, był przełożonym nad tym, co przygotowane w patelniach.
32 Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
[Niektórzy] ich bracia spośród synów Kehata [byli] ustanowieni [do opieki] nad chlebami pokładnymi, aby [je] przygotowywać w każdy szabat.
33 Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
Ci [byli] śpiewakami, naczelnikami rodów Lewitów, którzy mieszkają w komnatach; byli wolni od innych zajęć, gdyż we dnie i w nocy zajmowali się tą służbą.
34 Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
Byli oni naczelnikami rodów Lewitów, naczelnikami według swoich rodowodów, a mieszkali w Jerozolimie.
35 Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
W Gibeonie mieszkał Jejel, ojciec Gibeona, a jego żona miała na imię Maaka;
36 mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
A jego synem pierworodnym był Abdon, a następni to: Sur, Kisz, Baal, Neer, Nadab;
37 Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
I Gedor, Achio, Zachariasz, i Miklot.
38 Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
A Miklot spłodził Szimmeama. Tamci również mieszkali ze swoimi braćmi w Jerozolimie naprzeciw swoich braci.
39 Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
Neer spłodził Kisza, a Kisz spłodził Saula, a Saul spłodził Jonatana, Malkiszuę, Abinadaba i Eszbaala.
40 Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
Synem Jonatana [był] Meribbaal, a Meribbaal spłodził Micheasza.
41 Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
Synowie zaś Micheasza to: Piton, Melek, Tarea i [Achaz].
42 Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
Achaz spłodził Jarę, a Jara spłodził Alemeta, Azmaweta i Zimriego, a Zimri spłodził Mosę.
43 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
Mosa spłodził Bineę, a jego synem [był] Rafa, jego synem [był] Elasa, jego synem [był] Asel.
44 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.
Asel miał sześciu synów, a oto ich imiona: Azrikam, Bokru, Izmael, Szeariasz, Obadiasz i Chanan. Ci [byli] synami Asela.

< 1 Nyakati 9 >