< 1 Nyakati 25 >

1 Daudi, pamoja na majemadari wa jeshi, wakawatenga baadhi ya wana wa Asafu, wana wa Hemani na wana wa Yeduthuni, kwa ajili ya huduma ya kutoa unabii, wakitumia vinubi, zeze na matoazi. Hii ndiyo orodha ya watu waliofanya huduma hii:
Moreover David and the captains of the host separated to the service of the sons of Asaph, and of Heman, and of Jeduthun, who should prophesy with harps, with psalteries, and with cymbals: and the number of the workmen according to their service was:
2 Kutoka kwa wana wa Asafu walikuwa: Zakuri, Yosefu, Nethania na Asarela. Wana wa Asafu walikuwa chini ya usimamizi wa Asafu, ambaye alitoa unabii chini ya usimamizi wa mfalme.
Of the sons of Asaph; Zaccur, and Joseph, and Nethaniah, and Asarelah, the sons of Asaph under the hands of Asaph, who prophesied according to the order of the king.
3 Wana wa Yeduthuni walikuwa sita: Gedalia, Seri, Yeshaya, Shimei, Hashabia, na Matithia, nao walikuwa chini ya usimamizi wa baba yao Yeduthuni, wao walikuwa wakitoa unabii wakitumia vinubi, wakimshukuru na kumtukuza Bwana.
Of Jeduthun: the sons of Jeduthun; Gedaliah, and Zeri, and Jeshaiah, Hashabiah, and Mattithiah, six, under the hands of their father Jeduthun, who prophesied with a harp, to give thanks and to praise the LORD.
4 Wana wa Hemani walikuwa: Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli na Yeremothi, Hanania, Hanani, Eliatha, Gidalti na Romamti-Ezeri, Yoshbekasha, Malothi, Hothiri na Mahaziothi.
Of Heman: the sons of Heman; Bukkiah, Mattaniah, Uzziel, Shebuel, and Jerimoth, Hananiah, Hanani, Eliathah, Giddalti, and Romamti-ezer, Joshbekashah, Mallothi, Hothir, [and] Mahazioth:
5 Wote hawa walikuwa wana wa Hemani mwonaji wa mfalme. Aliwapata wana hawa kutokana na ahadi ya Mungu ili kumwinua. Mungu alimpa Hemani wana kumi na wanne na binti watatu.
All these [were] the sons of Heman the king's seer in the words of God, to lift up the horn. And God gave to Heman fourteen sons and three daughters.
6 Hawa wanaume wote walikuwa chini ya usimamizi wa baba yao kwa ajili ya uimbaji katika Hekalu la Bwana wakitumia matoazi, zeze na vinubi, kwa ajili ya huduma katika nyumba ya Mungu. Asafu, Yeduthuni na Hemani walikuwa chini ya usimamizi wa mfalme.
All these [were] under the hands of their father for song [in] the house of the LORD, with cymbals, psalteries, and harps, for the service of the house of God, according to the king's order to Asaph, Jeduthun, and Heman.
7 Pamoja na ndugu zao wote walikuwa wamefundishwa na kuwa stadi wa uimbaji kwa Bwana. Idadi yao walikuwa 288.
So the number of them, with their brethren that were instructed in the songs of the LORD, [even] all that were skillful, was two hundred and eighty eight.
8 Vijana kwa wazee, walimu kwa wanafunzi, wote walipanga kazi zao kwa kupiga kura.
And they cast lots, ward against [ward], as well the small as the great, the teacher as the scholar.
9 Kura ya kwanza, ambayo ilikuwa kwa ajili ya Asafu, ilimwangukia Yosefu, wanawe na jamaa zake, 12 Ya pili ikamwangukia Gedalia, yeye na wanawe pamoja na jamaa zake, 12
Now the first lot came forth for Asaph to Joseph: the second to Gedaliah, who with his brethren and sons [were] twelve:
10 Ya tatu ikamwangukia Zakuri, wanawe na jamaa zake, 12
The third to Zaccur, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
11 ya nne ikamwangukia Isri, // wanawe na jamaa zake, 12
The fourth to Izri, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
12 ya tano ikamwangukia Nethania, wanawe na jamaa zake, 12
The fifth to Nethaniah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
13 ya sita ikamwangukia Bukia, wanawe na jamaa zake, 12
The sixth to Bukkiah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
14 ya saba ikamwangukia Yesarela, // wanawe na jamaa zake, 12
The seventh to Jesharelah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
15 ya nane ikamwangukia Yeshaya, wanawe na jamaa zake, 12
The eighth to Jeshaiah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
16 ya tisa ikamwangukia Matania, wanawe na jamaa zake, 12
The ninth to Mattaniah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
17 ya kumi ikamwangukia Shimei, wanawe na jamaa zake, 12
The tenth to Shimei, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
18 ya kumi na moja ikamwangukia Azareli, // wanawe na jamaa zake, 12
The eleventh to Azareel, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
19 ya kumi na mbili ikamwangukia Hashabia, wanawe na jamaa zake, 12
The twelfth to Hashabiah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
20 ya kumi na tatu ikamwangukia Shubaeli, wanawe na jamaa zake, 12
The thirteenth to Shubael, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
21 ya kumi na nne ikamwangukia Matithia, wanawe na jamaa zake, 12
The fourteenth to Mattithiah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
22 ya kumi na tano ikamwangukia Yeremothi, wanawe na jamaa zake, 12
The fifteenth to Jeremoth, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
23 Ya kumi na sita ikamwangukia Hanania, wanawe na jamaa zake, 12
The sixteenth to Hananiah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
24 ya kumi na saba ikamwangukia Yoshbekasha, wanawe na jamaa zake, 12
The seventeenth to Joshbekashah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
25 ya kumi na nane ikamwangukia Hanani, wanawe na jamaa zake, 12
The eighteenth to Hanani, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
26 ya kumi na tisa ikamwangukia Malothi, wanawe na jamaa zake, 12
The nineteenth to Mallothi, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
27 ya ishirini ikamwangukia Eliatha, wanawe na jamaa zake, 12
The twentieth to Eliathah, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
28 ya ishirini na moja ikamwangukia Hothiri, wanawe na jamaa zake, 12
The one and twentieth to Hothir, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
29 ya ishirini na mbili ikamwangukia Gidalti, wanawe na jamaa zake, 12
The two and twentieth to Giddalti, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
30 ya ishirini na tatu ikamwangukia Mahaziothi, wanawe na jamaa zake, 12
The three and twentieth to Mahazioth, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve:
31 ya ishirini na nne ikamwangukia Romamti-Ezeri, wanawe na jamaa zake, 12.
The four and twentieth to Romamti-ezer, [he], his sons, and his brethren, [were] twelve.

< 1 Nyakati 25 >