< 1 Nyakati 14 >

1 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, waashi na maseremala ili kumjengea jumba la kifalme.
Potem Hiram, król Tyru, wysłał posłów do Dawida wraz z drewnem cedrowym, murarzami i cieślami, aby mu zbudowali dom.
2 Naye Daudi akatambua kwamba Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na kwamba ufalme wake umetukuzwa kwa ajili ya Israeli, watu wake.
I Dawid poznał, że PAN potwierdził jego królowanie nad Izraelem, gdyż wywyższył jego królestwo ze względu na swój lud Izraela.
3 Huko Yerusalemu Daudi akaoa wake wengine zaidi na akawa baba wa wana na mabinti wengi.
Dawid pojął więcej żon w Jerozolimie i spłodził więcej synów i córek.
4 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
A oto imiona tych, którzy mu się urodzili w Jerozolimie: Szammua, Szobab, Natan, Salomon;
5 Ibihari, Elishua, Elpeleti,
Jibchar, Eliszua, Elpalet;
6 Noga, Nefegi, Yafia,
Noga, Nefeg, Jafia;
7 Elishama, Beeliada na Elifeleti.
Eliszama, Beeliada i Elifelet.
8 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli yote, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akatoka ili kwenda kukabiliana nao.
Kiedy Filistyni usłyszeli, że Dawid został namaszczony na króla nad całym Izraelem, wszyscy Filistyni wyruszyli, aby go szukać. Gdy Dawid usłyszał o tym, wyszedł naprzeciw nich.
9 Basi Wafilisti walikuwa wameingia na kushambulia Bonde la Warefai,
Filistyni przybyli i rozciągnęli się w dolinie Refaim.
10 Hivyo Daudi akamuuliza Mungu: “Je, niende kuwashambulia hao Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, nitawatia mikononi mwako.”
I Dawid radził się Boga, mówiąc: Czy mam wyruszyć przeciw Filistynom i czy wydasz ich w moje ręce? PAN mu odpowiedział: Wyruszaj, a wydam ich w twoje ręce.
11 Hivyo Daudi pamoja na watu wake wakakwea mpaka Baal-Perasimu, akawashinda huko. Akasema, “Kama maji yafurikavyo, Mungu amewafurikia adui zangu kwa kutumia mkono wangu.” Kwa hiyo mahali pale pakaitwa Baal-Perasimu.
A gdy przybyli do Baal-Perasim, tam Dawid ich pobił. Wtedy Dawid powiedział: Bóg rozerwał moich wrogów przez moją rękę, jak rozrywają się wody. Dlatego nazwał to miejsce Baal-Perasim.
12 Wafilisti walikuwa wameacha miungu yao huko, Daudi akaamuru iteketezwe kwa moto.
I porzucili tam swoje bożki, a Dawid rozkazał spalić je ogniem.
13 Kwa mara nyingine Wafilisti wakavamia lile bonde;
Lecz Filistyni znowu rozciągnęli się w dolinie.
14 hivyo Daudi akamuuliza Mungu tena, naye Mungu akamjibu, “Usiwapandie moja kwa moja, bali wazungukie na uwashambulie kutoka mbele ya hiyo miti ya miforosadi.
Dawid więc ponownie radził się Boga, a Bóg mu odpowiedział: Nie ruszaj na nich, ale odwróć się od nich, abyś natarł na nich od strony drzew morwowych.
15 Mara usikiapo sauti ya kwenda juu ya hiyo miti ya miforosadi, hapo ndipo utoke upigane vita, kwa sababu hiyo itaonyesha kwamba Mungu amekutangulia ili kupiga jeshi la Wafilisti.”
A gdy usłyszysz odgłos kroków wśród wierzchołków drzew morwowych, wtedy wyruszysz do bitwy, gdyż Bóg wyruszył przed tobą, aby pobić wojska Filistynów.
16 Kwa hiyo Daudi akafanya kama alivyoagizwa na Mungu, wakalipiga jeshi la Wafilisti kuanzia Gibeoni hadi Gezeri.
I Dawid uczynił tak, jak mu rozkazał Bóg, i pobili wojska Filistynów od Gibeonu aż do Gezer.
17 Hivyo umaarufu wa Daudi ukaenea katika kila nchi, naye Bwana akayafanya mataifa yote kumwogopa Daudi.
I w ten sposób rozsławiło się imię Dawida na wszystkich ziemiach, a PAN sprawił, że bały się go wszystkie narody.

< 1 Nyakati 14 >