< 2 Reyes 1 >

1 Después de la muerte de Acab, Moab se rebeló contra Israel.
Baada ya kifo cha Mfalme Ahabu, nchi ya Moabu iliasi dhidi ya Israeli.
2 Entonces Ocozías se cayó de la ventana de su habitación en Samaria y estaba enfermo. Y envió a los hombres, y les dijo: Haz una pregunta a Baal-zebub, el dios de Ecrón, sobre el resultado de mi enfermedad, para ver si estoy bien o no.
Basi Ahazia alikuwa ameanguka huko Samaria kutoka baraza ya chumba chake cha juu, akaumia. Hivyo akatuma wajumbe, akiwaambia, “Nendeni mkaulize kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni, mkaone kama nitapona kutokana na kuumia huku.”
3 Pero el ángel del Señor le dijo a Elías el Tisbe: Ve ahora, a encuentro con los hombres enviados por el rey de Samaria, pregunta: ¿Es porque no hay Dios en Israel, que vas? para obtener direcciones de Baal-zebub, el dios de Ecrón?
Lakini malaika wa Bwana akamwambia Eliya, Mtishbi, “Panda ukakutane na wajumbe wa mfalme wa Samaria, uwaulize, ‘Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana mnakwenda kumuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni?’
4 Escucha las palabras del Señor: Nunca más volverás a bajar de la cama a la que has subido, pero la muerte sin duda te llegará. Entonces Elías se fue.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana, ‘Hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!’” Hivyo Eliya akaenda.
5 Y los hombres que había enviado regresaron al rey; Y él les preguntó: ¿Por qué han vuelto?
Wajumbe waliporudi kwa mfalme, akawauliza, “Kwa nini mmerudi?”
6 Y le dijeron: En nuestro camino tuvimos una reunión con un hombre que dijo: Vuelve al rey que te envió y dile: El Señor dice: ¿Acaso no hay Dios en Israel? ¿Que envías para hacerle una pregunta a Baal-zebub, el dios de Ecrón? Por esta razón, no te levantarás de la cama en la que te has acostado, pero la muerte sin duda te llegará.
Wakamjibu, “Mtu fulani alikuja kukutana nasi, naye akatuambia, ‘Rudini kwa mfalme aliyewatuma na mkamwambie, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ndiyo maana unawatuma watu kwenda kuuliza kwa Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa hiyo hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”’”
7 Y él les dijo: ¿Qué clase de hombre fue quien vino y les dijo estas palabras?
Mfalme akawauliza, “Alikuwa mtu wa namna gani ambaye mlikutana naye, akawaambia hili?”
8 Y ellos respondieron: Era un hombre velludo, con una banda de cuero alrededor de su cuerpo. Entonces él dijo: Es Elías el Tisbe.
Wakamjibu, “Alikuwa mtu aliyekuwa na vazi la manyoya na mkanda wa ngozi kiunoni mwake.” Mfalme akasema, “Huyo alikuwa ni Eliya, Mtishbi.”
9 Entonces el rey le envió un capitán de cincuenta con sus cincuenta hombres; y subió a él donde estaba sentado en la cima de una colina, y le dijo: Oh hombre de Dios, el rey ha dicho: Desciende.
Ndipo mfalme akamtuma mkuu mmoja wa kikosi pamoja na kikosi chake cha askari hamsini kwa nabii Eliya. Yule mkuu wa kikosi akamwendea Eliya, aliyekuwa ameketi juu ya kilima, na kumwambia, “Mtu wa Mungu, mfalme anasema, ‘Shuka chini!’”
10 Y Elías, en respuesta, dijo al capitán de los cincuenta: Si soy hombre de Dios, que el fuego descienda del cielo sobre ti y sobre tus cincuenta hombres, y te ponga fin. Entonces el fuego bajó del cielo y puso fin a él y a sus cincuenta hombres.
Eliya akamjibu yule mkuu wa kikosi, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza yule mkuu wa kikosi pamoja na watu wake.
11 Entonces el rey envió a otro capitán de cincuenta con sus cincuenta hombres; Y dijo a Elías: Oh hombre de Dios, el rey dice: Desciende pronto.
Aliposikia hili, mfalme akatuma kwa Eliya mkuu wa kikosi mwingine na askari wake hamsini. Yule mkuu wa kikosi akamwambia Eliya, “Mtu wa Mungu, hili ndilo asemalo mfalme, ‘Shuka chini mara moja!’”
12 Y Elías, en respuesta, dijo: Si soy hombre de Dios, que descienda fuego del cielo sobre ti y sobre tus cincuenta hombres, y te ponga fin. Y el fuego de Dios descendió del cielo y puso fin a él y a sus cincuenta hombres.
Eliya akajibu, “Ikiwa mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke kutoka mbinguni ukuteketeze wewe na watu wako hamsini!” Ndipo moto wa Mungu ukashuka kutoka mbinguni, ukamteketeza yeye na watu wake hamsini.
13 Entonces envió a un tercer capitán de cincuenta con sus cincuenta hombres; y el tercer capitán de los cincuenta subió, y, arrodillado ante Elías, pidiendo misericordia de él, dijo: Oh hombre de Dios, deja que mi vida y la vida de estos tus cincuenta siervos te sean de valor.
Hivyo mfalme akatuma mkuu wa kikosi wa tatu na watu wake hamsini. Huyu mkuu wa kikosi wa tatu akapanda na kupiga magoti mbele ya Eliya, akiomba, “Mtu wa Mungu, tafadhali niachie uhai wangu na uhai wa hawa watu hamsini, watumishi wako!
14 Porque el fuego bajó del cielo y puso fin a los dos primeros capitanes de los cincuenta y a sus hombres; Pero ahora deja que mi vida sea de valor en tus ojos.
Tazama, moto umeshuka kutoka mbinguni na kuwateketeza wale wakuu wa vikosi viwili vya kwanza pamoja na watu wao. Lakini sasa niachie uhai wangu!”
15 Entonces el ángel del Señor dijo a Elías: Desciende con él; No le tengas miedo. Entonces se levantó y descendió con él al rey.
Malaika wa Bwana akamwambia Eliya, “Shuka pamoja naye, usimwogope.” Hivyo Eliya akainuka na kushuka pamoja naye kwa mfalme.
16 Y él le dijo: Esta es la palabra del Señor: Porque enviaste a los hombres a hacerle una pregunta a Baal-zebub, el dios de Ecrón, como si en Israel no hubiera Dios, por esta razón nunca más volverás a bajar de la cama. a lo que has subido, pero la muerte ciertamente vendrá a ti.
Akamwambia mfalme, “Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli wa kumuuliza habari, ndiyo maana ukatuma wajumbe kuuliza Baal-Zebubu, mungu wa Ekroni? Kwa sababu umefanya hili, kamwe hutaondoka kwenye kitanda unachokilalia. Hakika utakufa!”
17 Y vino a él la muerte, como el Señor había dicho por boca de Elías. Y Joram se hizo rey en su lugar en el segundo año del gobierno de Joram, hijo de Josafat, rey de Judá; porque nunca tuvo hijos.
Hivyo akafa, sawasawa na lile neno la Bwana ambalo Eliya alikuwa amesema. Kwa kuwa Ahazia hakuwa na mwana, Yoramu akawa mfalme baada yake katika mwaka wa pili wa Yehoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda.
18 Los demás hechos de Ocozías, ¿no están registrados en el libro de la historia de los reyes de Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahazia na yale aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?

< 2 Reyes 1 >