< Salmos 96 >

1 CANTAD á Jehová canción nueva; cantad á Jehová, toda la tierra.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 Cantad á Jehová, bendecid su nombre: anunciad de día en día su salud.
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Contad entre las gentes su gloria, en todos los pueblos sus maravillas.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 Porque grande es Jehová, y digno de suprema alabanza; terrible sobre todos los dioses.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 Porque todos los dioses de los pueblos son ídolos: mas Jehová hizo los cielos.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 Alabanza y magnificencia delante de él: fortaleza y gloria en su santuario.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Dad á Jehová, oh familias de los pueblos, dad á Jehová la gloria y la fortaleza.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 Dad á Jehová la honra debida á su nombre: tomad presentes, y venid á sus atrios.
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 Encorvaos á Jehová en la hermosura de [su] santuario: temed delante de él, toda la tierra.
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Decid en las gentes: Jehová reinó, también afirmó el mundo, no será conmovido: juzgará á los pueblos en justicia.
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Alégrense los cielos, y gócese la tierra: brame la mar y su plenitud.
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 Regocíjese el campo, y todo lo que en él está: entonces todos los árboles del bosque rebosarán de contento,
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 Delante de Jehová que vino: porque vino á juzgar la tierra. Juzgará al mundo con justicia, y á los pueblos con su verdad.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.

< Salmos 96 >