< Salmos 91 >

1 EL que habita al abrigo del Altísimo, morará bajo la sombra del Omnipotente.
Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
2 Diré yo á Jehová: Esperanza mía, y castillo mío; mi Dios, en él confiaré.
Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
3 Y él te librará del lazo del cazador: de la peste destruidora.
Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
4 Con sus plumas te cubrirá, y debajo de sus alas estarás seguro: escudo y adarga es su verdad.
Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
5 No tendrás temor de espanto nocturno, ni de saeta que vuele de día;
Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
6 Ni de pestilencia que ande en oscuridad, ni de mortandad que en medio del día destruya.
wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
7 Caerán á tu lado mil, y diez mil á tu diestra: [mas] á ti no llegará.
Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
8 Ciertamente con tus ojos mirarás, y verás la recompensa de los impíos.
Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
9 Porque tú has puesto á Jehová, [que es] mi esperanza, al Altísimo por tu habitación,
Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
10 No te sobrevendrá mal, ni plaga tocará tu morada.
basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
11 Pues que á sus ángeles mandará acerca de ti, que te guarden en todos tus caminos.
Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
12 En las manos te llevarán, porque tu pie no tropiece en piedra.
Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
13 Sobre el león y el basilisco pisarás; hollarás al cachorro del león y al dragón.
Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
14 Por cuanto en mí ha puesto su voluntad, yo también lo libraré: pondrélo en alto, por cuanto ha conocido mi nombre.
Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
15 Me invocará, y yo le responderé: con él estaré yo en la angustia: lo libraré, y le glorificaré.
Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
16 Saciarélo de larga vida, y mostraréle mi salud.
Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”

< Salmos 91 >