< Salmos 88 >

1 Canción: Salmo para los hijos de Coré: al Músico principal: para cantar sobre Mahalath: Masquil de Hemán Ezrahita. OH Jehová, Dios de mi salud, día y noche clamo delante de ti.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
2 Entre mi oración en tu presencia: inclina tu oído á mi clamor.
Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
3 Porque mi alma está harta de males, y mi vida cercana al sepulcro. (Sheol h7585)
Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
4 Soy contado con los que descienden al hoyo, soy como hombre sin fuerza:
Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
5 Libre entre los muertos, como los matados que yacen en el sepulcro, que no te acuerdas más de ellos, y que son cortados de tu mano.
Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
6 Hasme puesto en el hoyo profundo, en tinieblas, en honduras.
Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
7 Sobre mí se ha acostado tu ira, y me has afligido con todas tus ondas. (Selah)
Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
8 Has alejado de mí mis conocidos: hasme puesto por abominación á ellos: encerrado estoy, y no puedo salir.
Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
9 Mis ojos enfermaron á causa de mi aflicción: hete llamado, oh Jehová, cada día; he extendido á ti mis manos.
nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
10 ¿Harás tú milagro á los muertos? ¿levantaránse los muertos para alabarte? (Selah)
Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
11 ¿Será contada en el sepulcro tu misericordia, ó tu verdad en la perdición?
Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
12 ¿Será conocida en las tinieblas tu maravilla, ni tu justicia en la tierra del olvido?
Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
13 Mas yo á ti he clamado, oh Jehová; y de mañana mi oración te previno.
Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
14 ¿Por qué, oh Jehová, desechas mi alma? ¿por qué escondes de mí tu rostro?
Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
15 Yo soy afligido y menesteroso: desde la mocedad he llevado tus terrores, he estado medroso.
Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
16 Sobre mí han pasado tus iras; tus espantos me han cortado.
Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
17 Hanme rodeado como aguas de continuo; hanme cercado á una.
Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
18 Has alejado de mí el amigo y el compañero; y mis conocidos [se esconden] en la tiniebla.
Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

< Salmos 88 >