< Salmos 80 >

1 Al Músico principal: sobre Sosannim Eduth: Salmo de Asaph. OH Pastor de Israel, escucha: tú que pastoreas como á ovejas á José, que estás entre querubines, resplandece.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 Despierta tu valentía delante de Ephraim, y de Benjamín, y de Manasés, y ven á salvarnos.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Oh Dios, haznos tornar; y haz resplandecer tu rostro, y seremos salvos.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Jehová, Dios de los ejércitos, ¿hasta cuándo humearás tú contra la oración de tu pueblo?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Dísteles á comer pan de lágrimas, y dísteles á beber lágrimas en gran abundancia.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Pusístenos por contienda á nuestros vecinos: y nuestros enemigos se burlan entre sí.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Oh Dios de los ejércitos, haznos tornar; y haz resplandecer tu rostro, y seremos salvos.
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Hiciste venir una vid de Egipto: echaste las gentes, y plantástela.
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Limpiaste [sitio] delante de ella, é hiciste arraigar sus raíces, y llenó la tierra.
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Los montes fueron cubiertos de su sombra; y sus sarmientos [como] cedros de Dios.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 Extendió sus vástagos hasta la mar, y hasta el río sus mugrones.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 ¿Por qué aportillaste sus vallados, y la vendimian todos los que pasan por el camino?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 Estropeóla el puerco montés, y pacióla la bestia del campo.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Oh Dios de los ejércitos, vuelve ahora: mira desde el cielo, y considera, y visita esta viña,
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 Y la planta que plantó tu diestra, y el renuevo que para ti corroboraste.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 Quemada á fuego está, asolada: perezcan por la reprensión de tu rostro.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Sea tu mano sobre el varón de tu diestra, sobre el hijo del hombre que para ti corroboraste.
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 Así no nos volveremos de ti: vida nos darás, é invocaremos tu nombre.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Oh Jehová, Dios de los ejércitos, haznos tornar; haz resplandecer tu rostro, y seremos salvos.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< Salmos 80 >