< Salmos 41 >

1 Al Músico principal: Salmo de David. BIENAVENTURADO el que piensa en el pobre: en el día malo lo librará Jehová.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
2 Jehová lo guarde, y le dé vida: sea bienaventurado en la tierra, y no lo entregues á la voluntad de sus enemigos.
Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3 Jehová lo sustentará sobre el lecho del dolor: mullirás toda su cama en su enfermedad.
Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
4 Yo dije: Jehová, ten misericordia de mí; sana mi alma, porque contra ti he pecado.
Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
5 Mis enemigos dicen mal de mí [preguntando]: ¿Cuándo morirá, y perecerá su nombre?
Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
6 Y si venía á ver[me], hablaba mentira: su corazón se amontonaba iniquidad; y salido fuera, hablába[la].
Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
7 Reunidos murmuraban contra mí todos los que me aborrecían: contra mí pensaban mal, [diciendo de mí]:
Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
8 Cosa pestilencial de él se ha apoderado; y el que cayó en cama, no volverá á levantarse.
“Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
9 Aun el hombre de mi paz, en quien yo confiaba, el que de mi pan comía, alzó contra mí el calcañar.
Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
10 Mas tú, Jehová, ten misericordia de mí, y hazme levantar, y daréles el pago.
Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
11 En esto habré conocido que te he agradado, que mi enemigo no se holgará de mí.
Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
12 En cuanto á mí, en mi integridad me has sustentado, y me has hecho estar delante de ti para siempre.
Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
13 Bendito sea Jehová, el Dios de Israel, por siglos de siglos. Amén y Amén.
Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.

< Salmos 41 >