< Salmos 38 >

1 Salmo de David, para recordar. JEHOVÁ, no me reprendas en tu furor, ni me castigues en tu ira.
Yahwe, usinikemee katika hasira yako; usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Porque tus saetas descendieron á mí, y sobre mí ha caído tu mano.
Kwa kuwa mishale yako hunichoma, na mkono wako huniangusha chini.
3 No hay sanidad en mi carne á causa de tu ira; ni hay paz en mis huesos á causa de mi pecado.
Mwili wangu wote unaumwa kwa sababu ya hasira yako; kwa sababu ya dhambi zangu mifupa yangu haina afya.
4 Porque mis iniquidades han pasado mi cabeza: como carga pesada se han agravado sobre mí.
Kwa maana maovu yangu yamenielemea; yamekuwa mzigo mzito kwangu.
5 Pudriéronse, corrompiéronse mis llagas, á causa de mi locura.
Vidonda vyangu vimeoza na vinanuka kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6 Estoy encorvado, estoy humillado en gran manera, ando enlutado todo el día.
Nimepindika na kuwa mnyonge kila siku; ninaenenda katika maombolezo siku zote.
7 Porque mis lomos están llenos de irritación, y no hay sanidad en mi carne.
Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
8 Estoy debilitado y molido en gran manera; bramo á causa de la conmoción de mi corazón.
Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
9 Señor, delante de ti están todos mis deseos; y mi suspiro no te es oculto.
Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
10 Mi corazón está acongojado, hame dejado mi vigor; y aun la misma luz de mis ojos no está conmigo.
Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
11 Mis amigos y mis compañeros se quitaron de delante de mi plaga; y mis cercanos se pusieron lejos.
Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.
12 Y los que buscaban mi alma armaron lazos; y los que procuraban mi mal hablaban iniquidades, y meditaban fraudes todo el día.
Wale wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego kwa ajili yangu. Wao ambao hutafuta kunidhuru huongea maneno ya uharibifu na husema maneno ya uongo siku nzima.
13 Mas yo, como [si fuera] sordo, no oía; [y estaba] como un mudo, [que] no abre su boca.
Lakini, niko kama mtu kiziwi na sisikii lolote; niko kama mtu bubu ambaye hasemi lolote.
14 Fuí pues como un hombre que no oye, y que en su boca no tiene reprensiones.
Niko kama mtu asiye sikia na mbaye hawezi kujibu.
15 Porque á ti, oh Jehová, esperé yo: tú responderás, Jehová Dios mío.
Hakika ninakungoja wewe, Yahwe; wewe utanijibu, Bwana Mungu wangu.
16 Porque dije: Que no se alegren de mí: cuando mi pie resbalaba, sobre mí se engrandecían.
Ninasema hivi ili kwamba maadui zangu wasije wakafurahia juu yangu. Ikiwa mguu wangu utateleza, watanifanyia mambo mabaya.
17 Empero yo estoy á pique de claudicar, y mi dolor está delante de mí continuamente.
Kwa kuwa niko karibu mashakani, na niko katika maumivu ya mara kwa mara.
18 Por tanto denunciaré mi maldad; congojaréme por mi pecado.
Ninatubu makosa yangu; ninahuzunika kwa dhambi zangu.
19 Porque mis enemigos están vivos [y] fuertes: y hanse aumentado los que me aborrecen sin causa:
Lakini maadui zangu ni wengi; wale wanichukiao ni wengi.
20 Y pagando mal por bien me son contrarios, por seguir yo lo bueno.
Wao wananilipa mabaya kwa mema; wanavurumiza shutuma kwangu ingawa nimefuata lililo jema.
21 No me desampares, oh Jehová: Dios mío, no te alejes de mí.
Usinitelekeze, Yahwe, Mungu wangu, usikae mbali nami.
22 Apresúrate á ayudarme, oh Señor, mi salud.
Njoo haraka unisaidie, Bwana, wokovu wangu.

< Salmos 38 >