< Salmos 26 >

1 Salmo de David. JÚZGAME, oh Jehová, porque yo en mi integridad he andado: confiado he asimismo en Jehová, no vacilaré.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 Pruébame, oh Jehová, y sondéame: examina mis riñones y mi corazón.
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 Porque tu misericordia está delante de mis ojos, y en tu verdad ando.
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 No me he sentado con hombres de falsedad; ni entré con los [que andan] encubiertamente.
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 Aborrecí la reunión de los malignos, y con los impíos nunca me senté.
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 Lavaré en inocencia mis manos, y andaré alrededor de tu altar, oh Jehová:
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 Para exclamar con voz de acción de gracias, y para contar todas tus maravillas.
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 Jehová, la habitación de tu casa he amado, y el lugar del tabernáculo de tu gloria.
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 No juntes con los pecadores mi alma, ni con los hombres de sangres mi vida:
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 En cuyas manos está el mal, y su diestra está llena de sobornos.
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 Yo empero andaré en mi integridad: redímeme, y ten misericordia de mí.
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 Mi pie ha estado en rectitud: en las congregaciones bendeciré á Jehová.
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.

< Salmos 26 >