< Salmos 2 >

1 ¿POR qué se amotinan las gentes, y los pueblos piensan vanidad?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 Estarán los reyes de la tierra, y príncipes consultarán unidos contra Jehová, y contra su ungido, [diciendo]:
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 Rompamos sus coyundas, y echemos de nosotros sus cuerdas.
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 El que mora en los cielos se reirá; el Señor se burlará de ellos.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Entonces hablará á ellos en su furor, y turbarálos con su ira.
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 Yo empero he puesto mi rey sobre Sión, monte de mi santidad.
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 Yo publicaré el decreto: Jehová me ha dicho: Mi hijo eres tú; yo te engendré hoy.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Pídeme, y te daré por heredad las gentes, y por posesión tuya los términos de la tierra.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Quebrantarlos has con vara de hierro: como vaso de alfarero los desmenuzarás.
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 Y ahora, reyes, entended: admitid corrección, jueces de la tierra.
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Servid á Jehová con temor, y alegraos con temblor.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Besad al Hijo, porque no se enoje, y perezcáis en el camino, cuando se encendiere un poco su furor. Bienaventurados todos los que en él confían.
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.

< Salmos 2 >