< Salmos 146 >

1 Aleluya. ALABA, oh alma mía, á Jehová.
Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
2 Alabaré á Jehová en mi vida: cantaré salmos á mi Dios mientras viviere.
Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
3 No confiéis en los príncipes, ni en hijo de hombre, porque no hay en él salud.
Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
4 Saldrá su espíritu, tornaráse en su tierra: en aquel día perecerán sus pensamientos.
Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
5 Bienaventurado aquel en cuya ayuda es el Dios de Jacob, cuya esperanza es en Jehová su Dios:
Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
6 El cual hizo los cielos y la tierra, la mar, y todo lo que en ellos hay; que guarda verdad para siempre;
Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
7 Que hace derecho á los agraviados; que da pan á los hambrientos: Jehová suelta á los aprisionados;
Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
8 Jehová abre [los ojos] á los ciegos; Jehová levanta á los caídos; Jehová ama á los justos.
Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
9 Jehová guarda á los extranjeros; al huérfano y á la viuda levanta; y el camino de los impíos trastorna.
Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
10 Reinará Jehová para siempre; tu Dios, oh Sión, por generación y generación. Aleluya.
Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.

< Salmos 146 >