< Salmos 121 >

1 Cántico gradual. ALZARÉ mis ojos á los montes, de donde vendrá mi socorro.
Nitayainua macho yangu nitazame milimani. Msaada wangu utatoka wapi?
2 Mi socorro [viene] de Jehová, que hizo los cielos y la tierra.
Msaada wangu unatoka kwa Yahwe, aliyezifanya mbingu na nchi.
3 No dará tu pie al resbaladero; ni se dormirá el que te guarda.
Hatauacha mguu wako uteleze; yeye akulindaye hatasinzia.
4 He aquí, no se adormecerá ni dormirá el que guarda á Israel.
Tazama, mlinzi wa Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi kamwe.
5 Jehová es tu guardador: Jehová es tu sombra á tu mano derecha.
Yahwe ni mlinzi wako; Yahwe ni uvuli mkono wako wa kuume.
6 El sol no te fatigará de día, ni la luna de noche.
Jua halitakudhuru wakati wa mchana, wala mwezi wakati wa usiku.
7 Jehová te guardará de todo mal: él guardará tu alma.
Yahwe atakulinda na madhara yote, na ataulinda uhai wako.
8 Jehová guardará tu salida y tu entrada, desde ahora y para siempre.
Yahwe atakulinda katika yote ufanyayo sasa na hata milele.

< Salmos 121 >