< Salmos 113 >

1 Aleluya. ALABAD, siervos de Jehová, alabad el nombre de Jehová.
Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
2 Sea el nombre de Jehová bendito, desde ahora y para siempre.
Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
3 Desde el nacimiento del sol hasta donde se pone, sea alabado el nombre de Jehová.
Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
4 Alto sobre todas las naciones es Jehová; sobre los cielos su gloria.
Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
5 ¿Quién como Jehová nuestro Dios, que ha enaltecido su habitación,
Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
6 Que se humilla á mirar en el cielo y en la tierra?
atazamaye chini angani na duniani?
7 El levanta del polvo al pobre, y al menesteroso alza del estiércol,
Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
8 Para hacerlos sentar con los príncipes, con los príncipes de su pueblo.
ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
9 El hace habitar en familia á la estéril, gozosa [en ser] madre de hijos. Aleluya.
Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!

< Salmos 113 >