< Salmos 109 >

1 Al Músico principal: Salmo de David. OH Dios de mi alabanza, no calles;
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 Porque boca de impío y boca de engañador se han abierto sobre mí: han hablado de mí con lengua mentirosa,
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 Y con palabras de odio me rodearon; y pelearon contra mí sin causa.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 En pago de mi amor me han sido adversarios: mas yo oraba.
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 Y pusieron contra mí mal por bien, y odio por amor.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 Pon sobre él al impío: y Satán esté á su diestra.
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 Cuando fuere juzgado, salga impío; y su oración sea para pecado.
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 Sean sus días pocos: tome otro su oficio.
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 Sean sus hijos huérfanos, y su mujer viuda.
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 Y anden sus hijos vagabundos, y mendiguen; y procuren [su pan lejos] de sus desolados hogares.
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 Enrede el acreedor todo lo que tiene, y extraños saqueen su trabajo.
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 No tenga quien le haga misericordia; ni haya quien tenga compasión de sus huérfanos.
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 Su posteridad sea talada; en segunda generación sea raído su nombre.
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 Venga en memoria cerca de Jehová la maldad de sus padres, y el pecado de su madre no sea borrado.
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 Estén siempre delante de Jehová, y él corte de la tierra su memoria.
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 Por cuanto no se acordó de hacer misericordia, y persiguió al hombre afligido y menesteroso y quebrantado de corazón, para matar[lo].
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 Y amó la maldición, y vínole; y no quiso la bendición, y ella se alejó de él.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 Y vistióse de maldición como de su vestido, y entró como agua en sus entrañas, y como aceite en sus huesos.
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 Séale como vestido con que se cubra, y en lugar de cinto con que se ciña siempre.
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 Este sea el pago de parte de Jehová de los que me calumnian, y de los que hablan mal contra mi alma.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 Y tú, Jehová Señor, haz conmigo por amor de tu nombre: líbrame, porque tu misericordia es buena.
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 Porque yo estoy afligido y necesitado; y mi corazón está herido dentro de mí.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 Voime como la sombra cuando declina; soy sacudido como langosta.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 Mis rodillas están debilitadas á causa del ayuno, y mi carne desfallecida por falta de gordura.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 Yo he sido para ellos objeto de oprobio; mirábanme, y meneaban su cabeza.
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Ayúdame, Jehová Dios mío: sálvame conforme á tu misericordia.
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 Y entiendan que esta es tu mano; [que] tú, Jehová, has hecho esto.
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 Maldigan ellos, y bendice tú: levántense, mas sean avergonzados, y regocíjese tu siervo.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 Sean vestidos de ignominia los que me calumnian; y sean cubiertos de su confusión como con manto.
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 Yo alabaré á Jehová en gran manera con mi boca, y le loaré en medio de muchos.
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 Porque él se pondrá á la diestra del pobre, para librar su alma de los que le juzgan.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.

< Salmos 109 >