< Proverbios 6 >

1 HIJO mío, si salieres fiador por tu amigo, si tocaste tu mano por el extraño,
Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2 Enlazado eres con las palabras de tu boca, y preso con las razones de tu boca.
basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3 Haz esto ahora, hijo mío, y líbrate, ya que has caído en la mano de tu prójimo: ve, humíllate, y asegúrate de tu amigo.
Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4 No des sueño á tus ojos, ni á tus párpados adormecimiento.
Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5 Escápate como el corzo de la mano [del cazador], y como el ave de la mano del parancero.
Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6 Ve á la hormiga, oh perezoso, mira sus caminos, y sé sabio;
Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7 La cual no teniendo capitán, ni gobernador, ni señor,
Hana akida, afisa au mtawala,
8 Prepara en el verano su comida y allega en el tiempo de la siega su mantenimiento.
lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9 Perezoso, ¿hasta cuándo has de dormir? ¿cuándo te levantarás de tu sueño?
Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10 Un poco de sueño, un poco de dormitar, y cruzar por un poco las manos para reposo:
Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11 Así vendrá tu necesidad como caminante, y tu pobreza como hombre de escudo.
ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12 El hombre malo, el hombre depravado, anda en perversidad de boca;
Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13 Guiña de sus ojos, habla con sus pies, indica con sus dedos;
akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
14 Perversidades hay en su corazón, anda pensando mal en todo tiempo; enciende rencillas.
Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
15 Por tanto su calamidad vendrá de repente; súbitamente será quebrantado, y no [habrá] remedio.
Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
16 Seis cosas aborrece Jehová, y aun siete abomina su alma:
Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
17 Los ojos altivos, la lengua mentirosa, las manos derramadoras de sangre inocente,
Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
18 El corazón que maquina pensamientos inicuos, los pies presurosos para correr al mal,
moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
19 El testigo falso que habla mentiras, y el que enciende rencillas entre los hermanos.
shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
20 Guarda, hijo mío, el mandamiento de tu padre, y no dejes la enseñanza de tu madre:
Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Atalos siempre en tu corazón, enlázalos á tu cuello.
Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 Te guiarán cuando anduvieres; cuando durmieres te guardarán; hablarán contigo cuando despertares.
utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 Porque el mandamiento es antorcha, y la enseñanza luz; y camino de vida las reprensiones de la enseñanza:
Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 Para que te guarden de la mala mujer, de la blandura de la lengua de la extraña.
Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 No codicies su hermosura en tu corazón, ni ella te prenda con sus ojos:
Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 Porque á causa de la mujer ramera [es reducido el hombre] á un bocado de pan; y la mujer caza la preciosa alma del varón.
Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 ¿Tomará el hombre fuego en su seno, sin que sus vestidos se quemen?
Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 ¿Andará el hombre sobre las brasas, sin que sus pies se abrasen?
Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 Así el que entrare á la mujer de su prójimo; no será sin culpa cualquiera que la tocare.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 No tienen en poco al ladrón, cuando hurtare para saciar su alma teniendo hambre:
Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 Empero tomado, paga las setenas, da toda la sustancia de su casa.
Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 Mas el que comete adulterio con la mujer, es falto de entendimiento: corrompe su alma el que tal hace.
Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 Plaga y vergüenza hallará; y su afrenta nunca será raída.
Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 Porque los celos son el furor del hombre, y no perdonará en el día de la venganza.
Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 No tendrá respeto á ninguna redención; ni querrá [perdonar], aunque multipliques los dones.
Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.

< Proverbios 6 >