< Proverbios 4 >

1 OID, hijos, la doctrina de un padre, y estad atentos para que conozcáis cordura.
Wanangu, sikilizeni, fundisho la baba, na zingatieni ili mjue maana ya ufahamu.
2 Porque os doy buena enseñanza; no desamparéis mi ley.
Mimi ninawapa mafundisho mazuri; msiyaache mafundisho yangu.
3 Porque yo fuí hijo de mi padre, delicado y único delante de mi madre.
Mimi nilikuwa mwana kwa baba yangu, mpole na mtoto pekee kwa mama yangu,
4 Y él me enseñaba, y me decía: Mantenga tu corazón mis razones, guarda mis mandamientos, y vivirás:
baba alinifundisha akiniambia, “Moyo wako uzingatie sana maneno yangu; shika amri zangu nawe uishi.
5 Adquiere sabiduría, adquiere inteligencia; no te olvides ni te apartes de las razones de mi boca;
Jipatie hekima na ufahamu; usisahau na kuyakataa maneno ya kinywa changu;
6 No la dejes, y ella te guardará; ámala, y te conservará.
usiiache hekima nayo itakulinda; ipenda nayo itakuhifadhi salama.
7 Sabiduría ante todo: adquiere sabiduría: y ante toda tu posesión adquiere inteligencia.
Hekima ni kitu cha muhimu sana, hivyo jipatie hekima na tumia namna zote kuweza kupata ufahamu.
8 Engrandécela, y ella te engrandecerá: ella te honrará, cuando tú la hubieres abrazado.
Tunza hekima nayo itakutukuza; ikumbatie nayo itakuheshimu.
9 Adorno de gracia dará á tu cabeza: corona de hermosura te entregará.
Hekima itaweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako; itakupa taji zuri.
10 Oye, hijo mío, y recibe mis razones; y se te multiplicarán años de vida.
Mwanangu, sikiliza, na kuzingatia maneno yangu, nawe utapata miaka mingi ya maisha yako.
11 Por el camino de la sabiduría te he encaminado, y por veredas derechas te he hecho andar.
Ninakuelekeza katika njia ya hekima, nimekuongoza katika mapito yaliyonyooka.
12 Cuando anduvieres no se estrecharán tus pasos; y si corrieres, no tropezarás.
Unapotembea, hakuna atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia hutajikwaa.
13 Ten el consejo, no lo dejes; guárdalo, porque eso es tu vida.
Shika mwongozo wala usiuache, utakuongoza, maana ni uzima wako.
14 No entres por la vereda de los impíos, ni vayas por el camino de los malos.
Usifuate njia ya waovu wala usiende katika njia ya watendao uovu.
15 Desampárala, no pases por ella; apártate de ella, pasa.
Jiepushe nayo, usipite katika njia hiyo; geuka na upite njia nyingine.
16 Porque no duermen ellos, si no hicieren mal; y pierden su sueño, si no han hecho caer.
Maana hawawezi kulala mpaka wafanye ubaya na hupotewa na usingizi hadi wasababishe mtu kujikwaa.
17 Porque comen pan de maldad, y beben vino de robos.
Maana wao hula mkate wa uovu na hunywa divai ya vurugu.
18 Mas la senda de los justos es como la luz de la aurora, que va en aumento hasta que el día es perfecto.
Bali njia ya mwenye kutenda haki ni kama mwanga ung'aao, huangaza zaidi na zaidi hadi mchana inapowasili kwa ukamilifu.
19 El camino de los impíos es como la oscuridad: no saben en qué tropiezan.
Njia ya waovu ni kama giza - hawajui ni kitu gani huwa wanajikwaa juu yake.
20 Hijo mío, está atento á mis palabras; inclina tu oído á mis razones.
Mwanangu, zingatia maneno yangu; sikiliza kauli zangu.
21 No se aparten de tus ojos; guárdalas en medio de tu corazón.
Usiziache zikaondoka machoni pako; uzitunze katika moyo wako.
22 Porque son vida á los que las hallan, y medicina á toda su carne.
Maana maneno yangu ni uzima kwa wenye kuyapata na afya katika mwili wao.
23 Sobre toda cosa guardada guarda tu corazón; porque de él mana la vida.
Ulinde salama moyo wako na uukinge kwa bidii zote; kwa kuwa katika moyo hububujika chemichemi za uzima.
24 Aparta de ti la perversidad de la boca, y aleja de ti la iniquidad de labios.
Jiepushe na kauli za udanganyifu na ujiepushe na mazungumzo ya ufisadi.
25 Tus ojos miren lo recto, y tus párpados en derechura delante de ti.
Macho yako yatazame mbele kwa unyoofu na kwa uthabiti tazama mbele sawasawa.
26 Examina la senda de tus pies, y todos tus caminos sean ordenados.
Usawazishe pito la mguu wako; na njia zako zote zitakuwa salama.
27 No te apartes á diestra, ni á siniestra: aparta tu pie del mal.
Usigeuke upande wa kulia au kushoto; ondoa mguu wako mbali na uovu.

< Proverbios 4 >