< Proverbios 30 >

1 PALABRAS de Agur, hijo de Jachê: La profecía que dijo el varón á Ithiel, á Ithiel y á Ucal.
Maneno ya Aguri mwana wa Yake - mausia: Mtu huyu alimwambia Ithieli, kwa Ithiel na Ukali:
2 Ciertamente más rudo soy yo que ninguno, ni tengo entendimiento de hombre.
Hakika nipo kama mnyama kuliko mwanadamu na sina ufahamu wa wanadamu.
3 Yo ni aprendí sabiduría, ni conozco la ciencia del Santo.
Sijajifunza hekima, wala sina maarifa ya Mtakatifu.
4 ¿Quién subió al cielo, y descendió? ¿quién encerró los vientos en sus puños? ¿quién ató las aguas en un paño? ¿quién afirmó todos los términos de la tierra? ¿cuál es su nombre, y el nombre de su hijo, si sabes?
Je ni nani amekwenda juu mbinguni na kurudi chini? Je ni nani aliyekusanya upepo kwenye mikono yake? Je ni nani aliyekusanya maji kwenye kanzu? Je ni nani aliyeziimarisha ncha za dunia yote? Jina lake ni nani, na jina la mtoto wake ni nani? Hakika unajua!
5 Toda palabra de Dios [es] limpia; es escudo á los que en él esperan.
Kila neno la Mungu limejaribiwa, yeye ni ngao kwa wale wanaokimbilia kwake.
6 No añadas á sus palabras, porque no te reprenda, y seas hallado mentiroso.
Usiyaongezee maneno haya, au atakukemea, na utathibitishwa kuwa mwongo.
7 Dos cosas te he demandado; no me [las] niegues antes que muera.
Vitu viwili ninakuomba, usivikatalie kwangu kabla sijafa:
8 Vanidad y palabra mentirosa aparta de mí. No me des pobreza ni riquezas; manténme del pan que he menester;
Majivuno na uongo viweke mbali nami. Usinipe umasikini wala utajiri, nipe tu chakula ninachohitaji.
9 No sea que me harte, y [te] niegue, y diga, ¿Quién es Jehová? ó no sea que siendo pobre, hurte, y blasfeme el nombre de mi Dios.
Maana nikipata vingi zaidi, nitakukana wewe na kusema, “Yehova ni nani?” Au kama nitakuwa masikini, nitaiba na kukufuru jina la Mungu wangu.
10 No acuses al siervo ante su señor, porque no te maldiga, y peques.
Usimkashifu mtumwa mbele ya bwana wake, au atakulaani na utapata hatia.
11 Hay generación que maldice á su padre, y á su madre no bendice.
Kizazi ambacho kinachomlaa baba yao na hakimbariki mama yao,
12 Hay generación limpia en su opinión, si bien no se ha limpiado su inmundicia.
kizazi hicho ni safi katika macho yao wenyewe, lakini hawajaoshwa uchafu wao.
13 Hay generación cuyos ojos son altivos, y cuyos párpados son alzados.
Hicho ni kizazi- jinsi gani macho yao yanakiburi na kope zao zimeinuka juu! -
14 Hay generación cuyos dientes son espadas, y sus muelas cuchillos, para devorar á los pobres de la tierra, y de entre los hombres á los menesterosos.
kuna kizazi ambacho meno yao ni upanga, na mifupa ya taya zao ni visu, ili waweze kumrarua masikini wamtoe duniani na mhitaji atoke miongoni mwa wanadamu.
15 La sanguijuela tiene dos hijas [que se llaman], Trae, trae. Tres cosas hay que nunca se hartan; [aun] la cuarta nunca dice, Basta:
Ruba anamabinti wawili, “Toa na Toa” wanalia. Kuna vitu vitatu ambavyo havitosheki, vinne ambavyo havisememi, “Inatosha”:
16 El sepulcro, y la matriz estéril, la tierra no harta de aguas, y el fuego que jamás dice, Basta. (Sheol h7585)
Kuzimu, tumbo tasa, nchi yenye kiu kwa maji, na moto usiosema, “Inatosha.” (Sheol h7585)
17 El ojo que escarnece á su padre, y menosprecia la enseñanza de la madre, los cuervos lo saquen de la arroyada, y tráguenlo los hijos del águila.
Jicho ambalo linamdhihaki baba na kudharau utii kwa mama, macho yake yatadonolewa na kunguru wa bondeni, na ataliwa na tai.
18 Tres cosas me son ocultas; aun tampoco sé la cuarta:
Kuna vitu vitatu ambavyo vinanishangaza, vinne ambavyo sivifahamu:
19 El rastro del águila en el aire; el rastro de la culebra sobre la peña; el rastro de la nave en medio de la mar; y el rastro del hombre en la moza.
njia ya tai angani; njia ya nyoka juu ya mwamba; njia ya meli kwenye moyo wa bahari; na njia ya mtu pamoja mwanake kijana.
20 Tal es el rastro de la mujer adúltera: come, y limpia su boca, y dice: No he hecho maldad.
Hii ni njia ya mzinzi- anakula na kufuta kinywa chake na kusema, “sijafanya ubaya wowote.”
21 Por tres cosas se alborota la tierra, y la cuarta no puede sufrir:
Chini ya vitu vitatu dunia hutetemeka na vinne haiwezi kuvivumilia:
22 Por el siervo cuando reinare; y por el necio cuando se hartare de pan;
mtumwa anapokuwa mfalme; mpumbavu anaposhiba vyakula;
23 Por la aborrecida cuando se casare; y por la sierva cuando heredare á su señora.
mwanamke anayechukiwa anapoolewa; kijakazi anapochukua nafasi ya mkuu wake.
24 Cuatro cosas son de las más pequeñas de la tierra, y las mismas son más sabias que los sabios:
Vitu vinne duniani ni vidogo na bado vinabusara:
25 Las hormigas, pueblo no fuerte, y en el verano preparan su comida;
mchwa ni viumbe ambao sio imara, lakini huandaa chakula chao wakati wa hari,
26 Los conejos, pueblo nada esforzado, y ponen su casa en la piedra;
Wibari siyo viumbe wenye nguvu, lakini hutengeneza makazi yake kwenye miamba.
27 Las langostas, no tienen rey, y salen todas acuadrilladas;
Nzige hawana mfalme, lakini wote wanamwendo wa mpangilio.
28 La araña, ase con las manos, y está en palacios de rey.
Kama mjusi, unaweza kumkunja kwa mikono yako miwili, lakini wanapatikana katika majumba ya wafalme.
29 Tres cosas hay de hermoso andar, y la cuarta pasea muy bien:
Kuna vitu vitatu ambavyo ni fahari katika mwendo na vinne ambavyo ni fahari katika namna ya kutembea:
30 El león, fuerte entre todos los animales, que no torna atrás por nadie;
simba, aliyeimara miongoni mwa wanyama- wala hajiepushi na kitu chochote;
31 El [lebrel] ceñido de lomos; asimismo el macho cabrío; y un rey contra el cual ninguno se levanta.
jogoo anayetembea kwa mikogo; mbuzi; na mfalme ambaye askari wapo kando yake.
32 Si caiste, [fué] porque te enalteciste; y si mal pensaste, [pon] el dedo sobre la boca.
Kama umekuwa mpumbavu, jitukuze mwenyewe, au kama umekuwa ukisimamia vibaya- weka mkono wako juu ya kinywa chako.
33 Ciertamente el que exprime la leche, sacará manteca; y el que recio se suena las narices, sacará sangre: y el que provoca la ira, causará contienda.
Kama kusuka maziwa hufanya siagi na pua ya mtu hutoa damu kama imepigwa, basi matendo yanayofanywa kwa hasira huzalisha mafarakano.

< Proverbios 30 >