< Proverbios 21 >

1 COMO los repartimientos de las aguas, así está el corazón del rey en la mano de Jehová: á todo lo que quiere lo inclina.
Moyo wa mfalme ni mfereji wa maji katika mkono wa Yehova; anaugeuza popote anakopenda.
2 Todo camino del hombre es recto en su opinión: mas Jehová pesa los corazones.
Kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe, lakini ni Yehova anayeipima mioyo.
3 Hacer justicia y juicio es á Jehová más agradable que sacrificio.
Kutenda haki na adili hukubaliwa zaidi na Yehova kuliko sadaka.
4 Altivez de ojos, y orgullo de corazón, y el brillo de los impíos, son pecado.
Macho ya kiburi na moyo wa majivuno- taa ya waovu- ni dhambi.
5 Los pensamientos del solícito ciertamente [van] á abundancia; mas todo presuroso, indefectiblemente á pobreza.
Mipango ya mwenye juhudi huelekea kwenye mafanikio tu, bali kila mtu anayetenda kwa haraka huelekea umasikini.
6 Allegar tesoros con lengua de mentira, es vanidad desatentada de aquellos que buscan la muerte.
Kujipatia utajiri kwa ulimi wa uongo ni mvuke unaopita upesi na mtego ambao unafisha.
7 La rapiña de los impíos los destruirá; por cuanto no quisieron hacer juicio.
Vurugu ya waovu itawaburuta mbali, maana wanakataa kutenda haki.
8 El camino del hombre perverso es torcido y extraño: mas la obra del limpio es recta.
Njia ya mwenye hatia ni ukatiri, bali mwenye usafi hutenda yaliyo ya haki.
9 Mejor es vivir en un rincón de zaquizamí, que con la mujer rencillosa en espaciosa casa.
Bora kuishi kwenye kona ya juu darini kuliko katika nyumba pamoja na mke mgonvi.
10 El alma del impío desea mal: su prójimo no le parece bien.
Hamu ya mwovu ni uchu wa mabaya; jirani yake haoni ukarimu katika macho yake.
11 Cuando el escarnecedor es castigado, el simple se hace sabio; y cuando se amonestare al sabio, aprenderá ciencia.
Mwenye dhihaka anapoadhibiwa mjinga hupata busara, na mtu mwenye busara anapofundishwa, anaongeza maarifa.
12 Considera el justo la casa del impío: [cómo] los impíos son trastornados por el mal.
Atendaye haki huilinda nyumba ya mwovu; huwashusha waovu kwenye uharibifu.
13 El que cierra su oído al clamor del pobre, también él clamará, y no será oído.
Anayeziba masikio yake kwenye kilio cha masikini, pia atalia, lakini hatajibiwa.
14 El presente en secreto amansa el furor, y el don en el seno, la fuerte ira.
Zawadi ya siri hutuliza hasira na zawadi ya kificho hutuliza ghadhabu kuu.
15 Alegría es al justo hacer juicio; mas quebrantamiento á los que hacen iniquidad.
Haki ikitendeka, huleta furaha kwa mwenye kutenda wema, lakini huleta hofu kubwa kwa watenda mabaya.
16 El hombre que se extravía del camino de la sabiduría, vendrá á parar en la compañía de los muertos.
Yule anayezurura kutoka kwenye njia ya ufahamu, atapumzika kwenye kusanyiko la wafu.
17 Hombre necesitado será el que ama el deleite: y el que ama el vino y ungüentos no enriquecerá.
Anayependa raha atakuwa masikini; anayependa divai na mafuta hawezi kuwa tajiri.
18 El rescate del justo es el impío, y por los rectos el prevaricador.
Mtu mbaya ni fidia kwa yule atendaye haki, na mdanganyifu ni fidia kwa waaminifu.
19 Mejor es morar en tierra del desierto, que con la mujer rencillosa é iracunda.
Bora kuishi jangwani kuliko kuishi pamoja na mwanamke ambaye huchochea sana ugomvi na malalamiko.
20 Tesoro codiciable y pingüe hay en la casa del sabio; mas el hombre insensato lo disipará.
Hazina yenye thamani na mafuta vipo nyumbani kwa mwenye busara, bali mtu mpumbavu huviharibu.
21 El que sigue la justicia y la misericordia, hallará la vida, la justicia, y la honra.
Mtu atendaye haki na mwema -huyu mtu hupata uzima, haki na heshima.
22 La ciudad de los fuertes tomó el sabio, y derribó la fuerza en que ella confiaba.
Mtu mwenye busara huupima mji wa mashujaa, na huiangusha ngome wanayoitumaini.
23 El que guarda su boca y su lengua, su alma guarda de angustias.
Anayelinda kinywa chake na ulimi wake hujilinda mwenyewe na taabu.
24 Soberbio y presuntuoso escarnecedor es el nombre del que obra con orgullosa saña.
Mtu mwenye kiburi na maringo- “Dhihaka” ndilo jina lake - hutenda kwa majivuno na kujidai.
25 El deseo del perezoso le mata, porque sus manos no quieren trabajar.
Shauku ya mtu mvivu itamuua, maana mikono yake hukataa kufanya kazi.
26 Hay quien todo el día codicia: mas el justo da, y no desperdicia.
Kwa siku nzima hupatwa na uchu na uchu zaidi, lakini atendaye haki hutoa na wala hazuii.
27 El sacrificio de los impíos es abominación: ¡cuánto más ofreciéndolo con maldad!
Sadaka ya mwovu ni chukizo; huwa ni chukizo zaidi anapoileta kwa nia mbaya.
28 El testigo mentiroso perecerá: mas el hombre que oye, permanecerá en su dicho.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali anayesikiliza ataongea kwa muda wote.
29 El hombre impío afirma su rostro: mas el recto ordena sus caminos.
Mtu mwovu huufanya uso wake kuwa mgumu, bali mtu mwadilifu ni thabiti juu ya njia zake.
30 No hay sabiduría, ni inteligencia, ni consejo, contra Jehová.
Hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna shauri linaloweza kusimama kinyume na Yehova.
31 El caballo se apareja para el día de la batalla: mas de Jehová es el salvar.
Farasi hutayarishwa kwa siku ya mapigano, lakini ushindi hupatikana kwa Yehova.

< Proverbios 21 >