< Números 33 >

1 ESTAS son las estancias de los hijos de Israel, los cuales salieron de la tierra de Egipto por sus escuadrones, bajo la conducta de Moisés y Aarón.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Y Moisés escribió sus salidas conforme á sus jornadas por mandato de Jehová. Estas, pues, son sus estancias con arreglo á sus partidas.
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 De Rameses partieron en el mes primero, á los quince días del mes primero: el segundo día de la pascua salieron los hijos de Israel con mano alta, á ojos de todos los Egipcios.
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 [Estaban] enterrando los Egipcios los que Jehová había muerto de ellos, á todo primogénito; habiendo Jehová hecho también juicios en sus dioses.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Partieron, pues, los hijos de Israel de Rameses, y asentaron campo en Succoth.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Y partiendo de Succoth, asentaron en Etham, que está al cabo del desierto.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Y partiendo de Etham, volvieron sobre Pi-hahiroth, que está delante de Baalsephon, y asentaron delante de Migdol.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Y partiendo de Pi-hahiroth, pasaron por medio de la mar al desierto, y anduvieron camino de tres días por el desierto de Etham, y asentaron en Mara.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Y partiendo de Mara, vinieron á Elim, donde había doce fuentes de aguas, y setenta palmeras; y asentaron allí.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Y partidos de Elim, asentaron junto al mar Bermejo.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 Y partidos del mar Bermejo, asentaron en el desierto de Sin.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Y partidos del desierto de Sin, asentaron en Dophca.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Y partidos de Dophca, asentaron en Alús.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Y partidos de Alús, asentaron en Rephidim, donde el pueblo no tuvo aguas para beber.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Y partidos de Rephidim, asentaron en el desierto de Sinaí.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Y partidos del desierto de Sinaí, asentaron en Kibroth-hataava.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Y partidos de Kibroth-hataava, asentaron en Haseroth.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Y partidos de Haseroth, asentaron en Ritma.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Y partidos de Ritma, asentaron en Rimmón-peres.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Y partidos de Rimmón-peres, asentaron en Libna.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Y partidos de Libna, asentaron en Rissa.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Y partidos de Rissa, asentaron en Ceelatha.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Y partidos de Ceelatha, asentaron en el monte de Sepher.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Y partidos del monte de Sepher, asentaron en Harada.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Y partidos de Harada, asentaron en Maceloth.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Y partidos de Maceloth, asentaron en Tahath.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Y partidos de Tahath, asentaron en Tara.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Y partidos de Tara, asentaron en Mithca.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Y partidos de Mithca, asentaron en Hasmona.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Y partidos de Hasmona, asentaron en Moseroth.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Y partidos de Moseroth, asentaron en Bene-jaacán.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Y partidos de Bene-jaacán, asentaron en el monte de Gidgad.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Y partidos del monte de Gidgad, asentaron en Jotbatha.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Y partidos de Jotbatha, asentaron en Abrona.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Y partidos de Abrona, asentaron en Esion-geber.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Y partidos de Esion-geber, asentaron en el desierto de Zin, que es Cades.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Y partidos de Cades, asentaron en el monte de Hor, en la extremidad del país de Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Y subió Aarón el sacerdote al monte de Hor, conforme al dicho de Jehová, y allí murió á los cuarenta años de la salida de los hijos de Israel de la tierra de Egipto, en el mes quinto, en el primero del mes.
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 Y era Aarón de edad de ciento y veinte y tres años, cuando murió en el monte de Hor.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Y el Cananeo, rey de Arad, que habitaba al mediodía en la tierra de Canaán, oyó como habían venido los hijos de Israel.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Y partidos del monte de Hor, asentaron en Salmona.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Y partidos de Salmona, asentaron en Phunón.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Y partidos de Phunón, asentaron en Oboth.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Y partidos de Oboth, asentaron en Ije-abarim; en el término de Moab.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Y partidos de Ije-abarim, asentaron en Dibon-gad.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Y partidos de Dibon-gad, asentaron en Almon-diblathaim.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Y partidos de Almon-diblathaim, asentaron en los montes de Abarim, delante de Nebo.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Y partidos de los montes de Abarim, asentaron en los campos de Moab, junto al Jordán de Jericó.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 Finalmente asentaron junto al Jordán, desde Beth-jesimoth hasta Abel-sitim, en los campos de Moab.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Y habló Jehová á Moisés en los campos de Moab junto al Jordán de Jericó, diciendo:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 Habla á los hijos de Israel, y diles: Cuando hubiereis pasado el Jordán á la tierra de Canaán,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 Echaréis á todos los moradores del país de delante de vosotros, y destruiréis todas sus pinturas, y todas sus imágenes de fundición, y arruinaréis todos sus altos;
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Y echaréis [los moradores de] la tierra, y habitaréis en ella; porque yo os la he dado para que la poseáis.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Y heredaréis la tierra por suertes por vuestras familias: á los muchos daréis mucho por su heredad, y á los pocos daréis menos por heredad suya: donde le saliere la suerte, allí la tendrá cada uno: por las tribus de vuestros padres heredaréis.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 Y si no echareis los moradores del país de delante de vosotros, sucederá que los que dejareis de ellos serán por aguijones en vuestros ojos, y por espinas en vuestros costados, y afligiros han sobre la tierra en que vosotros habitareis.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 Será además, que haré á vosotros como yo pensé hacerles á ellos.
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Números 33 >