< Job 39 >

1 ¿Sabes tú el tiempo en que paren las cabras monteses? ¿ó miraste tú las ciervas cuando están pariendo?
Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
2 ¿Contaste tú los meses de su preñez, y sabes el tiempo cuando han de parir?
Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
3 Encórvanse, hacen salir sus hijos, pasan sus dolores.
Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
4 Sus hijos están sanos, crecen con el pasto: salen y no vuelven á ellas.
Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
5 ¿Quién echó libre al asno montés, y quién soltó sus ataduras?
Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
6 Al cual yo puse casa en la soledad, y sus moradas en lugares estériles.
ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
7 Búrlase de la multitud de la ciudad: no oye las voces del arriero.
Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
8 Lo oculto de los montes es su pasto, y anda buscando todo lo que está verde.
Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
9 ¿Querrá el unicornio servirte á ti, ni quedar á tu pesebre?
Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
10 ¿Atarás tú al unicornio con su coyunda para el surco? ¿labrará los valles en pos de ti?
Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
11 ¿Confiarás tú en él, por ser grande su fortaleza, y le fiarás tu labor?
Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
12 ¿Fiarás de él que te tornará tu simiente, y que [la] allegará en tu era?
Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
13 ¿[Diste tú] hermosas alas al pavo real, ó alas y plumas al avestruz?
Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
14 El cual desampara en la tierra sus huevos, y sobre el polvo los calienta,
Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
15 Y olvídase de que los pisará el pie, y que los quebrará bestia del campo.
husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
16 Endurécese para con sus hijos, como si no fuesen suyos, no temiendo que su trabajo haya sido en vano:
Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
17 Porque le privó Dios de sabiduría, y no le dió inteligencia.
kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
18 Luego que se levanta en alto, búrlase del caballo y de su jinete.
Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
19 ¿Diste tú al caballo la fortaleza? ¿vestiste tú su cerviz de relincho?
Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
20 ¿Le intimidarás tú como á alguna langosta? El resoplido de su nariz es formidable:
Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
21 Escarba la tierra, alégrase en su fuerza, sale al encuentro de las armas:
Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
22 Hace burla del espanto, y no teme, ni vuelve el rostro delante de la espada.
Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
23 Contra él suena la aljaba, el hierro de la lanza y de la pica:
Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
24 Y él con ímpetu y furor escarba la tierra, sin importarle el sonido de la bocina;
Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
25 [Antes como] que dice entre los clarines: ¡Ea!, y desde lejos huele la batalla, el grito de los capitanes, y la vocería.
Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
26 ¿Vuela el gavilán por tu industria, y extiende hacia el mediodía sus alas?
Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
27 ¿Se remonta el águila por tu mandamiento, y pone en alto su nido?
Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
28 Ella habita y está en la piedra, en la cumbre del peñasco y de la roca.
Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
29 Desde allí acecha la comida: sus ojos observan de muy lejos.
Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
30 Sus pollos chupan la sangre: y donde hubiere cadáveres, allí está.
Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.

< Job 39 >