< Éxodo 39 >

1 Y DEL jacinto, y púrpura, y carmesí, hicieron las vestimentas del ministerio para ministrar en el santuario, y asimismo hicieron las vestiduras sagradas para Aarón; como Jehová lo había mandado á Moisés.
Na kutokana na ule uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili wakafanya mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Basi wakafanya yale mavazi matakatifu yaliyokuwa kwa ajili ya Aruni, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
2 Hizo también el ephod de oro, de cárdeno y púrpura y carmesí, y lino torcido.
Basi akaifanya ile naivera ya dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
3 Y extendieron las planchas de oro, y cortaron hilos para tejerlos entre el jacinto, y entre la púrpura, y entre el carmesí, y entre el lino, con delicada obra.
Kisha wakafua mabamba ya dhahabu yawe mabamba membamba, naye akakata nyuzi za kufuma pamoja na ule uzi wa bluu na ile sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kile kitani bora, kama kazi ya mjenzi.
4 Hiciéronle las hombreras que se juntasen; y uníanse en sus dos lados.
Wakaifanyia vipande vya begani vilivyounganishwa. Iliunganishwa kwenye miisho yake miwili.
5 Y el cinto del ephod que estaba sobre él, era de lo mismo, conforme á su obra; de oro, jacinto, y púrpura, y carmesí, y lino torcido; como Jehová lo había mandado á Moisés.
Nao mshipi, uliokuwa juu yake ili kuifunga, ulikuwa wa kitambaa kilekile kulingana na ufundi wake, wa dhahabu, uzi wa bluu, na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
6 Y labraron las piedras oniquinas cercadas de engastes de oro, grabadas de grabadura de sello con los nombres de los hijos de Israel:
Kisha wakafanya mawe ya shohamu yaliyopangwa kwenye mapambo ya dhahabu, yaliyochongwa kwa michoro ya muhuri kulingana na majina ya wana wa Israeli.
7 Y púsolas sobre las hombreras del ephod, por piedras de memoria á los hijos de Israel; como Jehová lo había á Moisés mandado.
Bezaleli akayaweka kwenye vile vipande vya begani vya naivera yawe mawe ya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
8 Hizo también el racional de primorosa obra, como la obra del ephod, de oro, jacinto, y púrpura, y carmesí, y lino torcido.
Kisha akafanya kile kifuko cha kifuani kwa ufundi wa mjenzi, kama ule ufundi wa naivera, kutokana na dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
9 Era cuadrado: doblado hicieron el racional: su longitud era de un palmo, y de un palmo su anchura, doblado.
Kilikuwa mraba kilipokunjwa. Walikifanya kile kifuko cha kifuani, kinapokunjwa, shubiri moja urefu wake na shubiri moja upana wake.
10 Y engastaron en él cuatro órdenes de piedras. El primer orden era un sardio, un topacio, y un carbunclo: este el primer orden.
Kisha wakakijaza kwa mistari minne ya mawe. Mstari wa zabarijadi, topazi na zumaridi ulikuwa mstari wa kwanza.
11 El segundo orden, una esmeralda, un zafiro, y un diamante.
Nao mstari wa pili ulikuwa feruzi, yakuti na yaspi.
12 El tercer orden, un ligurio, un ágata, y un amatista.
Nao mstari wa tatu ulikuwa jiwe la leshemi, akiki na amethisti.
13 Y el cuarto orden, un berilo, un onix, y un jaspe: cercadas y encajadas en sus engastes de oro.
Nao mstari wa nne ulikuwa krisolito na shohamu na yashefi. Yaliwekwa katika mapambo ya dhahabu katika mahali pake.
14 Las cuales piedras eran conforme á los nombres de los hijos de Israel, doce según los nombres de ellos; como grabaduras de sello, cada una con su nombre según las doce tribus.
Na mawe hayo yalikuwa kulingana na majina ya wana wa Israeli. Yalikuwa kumi na mawili kulingana na majina yao, kwa michongo ya muhuri, kila moja kulingana na jina lake kwa ajili ya yale makabila kumi na mawili.
15 Hicieron también sobre el racional las cadenas pequeñas de hechura de trenza, de oro puro.
Nao wakafanya juu ya kile kifuko cha kifuani minyororo yenye mashada, msokoto wa kamba, wa dhahabu safi.
16 Hicieron asimismo los dos engastes y los dos anillos, de oro; los cuales dos anillos de oro pusieron en los dos cabos del racional.
Kisha wakafanya mapambo mawili ya dhahabu na pete mbili za dhahabu na kuziweka hizo pete mbili kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani.
17 Y pusieron las dos trenzas de oro en aquellos dos anillos á los cabos del racional.
Baada ya hilo wakapitisha zile kamba mbili za dhahabu kwenye zile pete mbili zilizo kwenye miisho ya kile kifuko cha kifuani.
18 Y fijaron los dos cabos de las dos trenzas en los dos engastes, que pusieron sobre las hombreras del ephod, en la parte delantera de él.
Nao wakapitisha ile miisho miwili ya zile kamba mbili kwenye yale mapambo mawili. Halafu wakaiweka juu ya vile vipande vya begani vya naivera, mbele yake.
19 E hicieron dos anillos de oro, que pusieron en los dos cabos del racional en su orilla, á la parte baja del ephod.
Kisha wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani kwenye upindo wake ulio upande unaoelekea ile efodi upande wa ndani.
20 Hicieron además dos anillos de oro, los cuales pusieron en las dos hombreras del ephod, abajo en la parte delantera, delante de su juntura, sobre el cinto del ephod.
Halafu wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka juu ya vile vipande viwili vya begani vya efodi upande wake wa chini, sehemu yake ya mbele, karibu na mahali pake pa kuungania, juu ya ule mshipi wa naivera.
21 Y ataron el racional de sus anillos á los anillos del ephod con un cordón de jacinto, para que estuviese sobre el cinto del mismo ephod, y no se apartase el racional del ephod; como Jehová lo había mandado á Moisés.
Mwishowe wakakifunga kile kifuko cha kifuani kwa pete zake kwenye zile pete za efodi kwa uzi wa bluu, ili kipate kuwa juu ya mshipi wa efodi na kile kifuko cha kifuani kisiondoke juu ya efodi, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
22 Hizo también el manto del ephod de obra de tejedor, todo de jacinto,
Bezaleli akafanya lile koti la naivera, lote la uzi wa zambarau, kazi ya mshonaji.
23 Con su abertura en medio de él, como el cuello de un coselete, con un borde en derredor de la abertura, porque no se rompiese.
Na sehemu wazi ya hilo koti ilikuwa katikati yake, kama sehemu wazi ya vazi la chuma. Sehemu hiyo iliyo wazi ilikuwa na ukingo kuizunguka pande zote ili isiraruke.
24 E hicieron en las orillas del manto las granadas de jacinto, y púrpura, y carmesí, y lino torcido.
Halafu wakafanya kwenye upindo wa hilo koti makomamanga ya uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, vilivyosokotwa pamoja.
25 Hicieron también las campanillas de oro puro, las cuales campanillas pusieron entre las granadas por las orillas del manto alrededor entre las granadas:
Wakafanya kengele za dhahabu safi na kuziweka kengele hizo katikati ya makomamanga kwenye upindo wa lile koti kuzunguka pande zote, katikati ya makomamanga;
26 Una campanilla y una granada, una campanilla y una granada alrededor, en las orillas del manto, para ministrar; como Jehová lo mandó á Moisés.
kengele na komamanga, kengele na komamanga kwenye upindo wa hilo koti kuzunguka pande zote, kwa ajili ya kuhudumu, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
27 Igualmente hicieron las túnicas de lino fino de obra de tejedor, para Aarón y para sus hijos;
Kisha wakafanya zile kamba za kitani bora, kwa ajili ya Haruni na wanawe.
28 Asimismo la mitra de lino fino, y los adornos de los chapeos (tiaras) de lino fino, y los pañetes de lino, de lino torcido;
Na kile kilemba cha kitani bora na yale mavalio ya kichwani ya mapambo ya kitani bora na zile suruali za kitani bora kilichosokotwa,
29 También el cinto de lino torcido, y de jacinto, y púrpura, y carmesí, de obra de recamador; como Jehová lo mandó á Moisés.
na ule ukumbuu wa kitani bora kilichosokotwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kazi ya mfumaji, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
30 Hicieron asimismo la plancha de la diadema santa de oro puro, y escribieron en ella de grabadura de sello, el rótulo, SANTIDAD Á JEHOVÁ.
Mwishowe wakafanya lile bamba linalong’aa, ishara takatifu ya wakfu, kutokana na dhahabu safi na kuandika juu yake maandishi kwa mchongo wa muhuri: “Utakatifu kwa Yahweh.”
31 Y pusieron en ella un cordón de jacinto, para colocarla en alto sobre la mitra; como Jehová lo había mandado á Moisés.
Kisha wakalitia uzi wa bluu ili waliweke juu ya kile kilemba upande wa juu. Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
32 Y fué acabada toda la obra del tabernáculo, del tabernáculo del testimonio: é hicieron los hijos de Israel como Jehová lo había mandado á Moisés: así lo hicieron.
Basi kazi ya ile maskani ya hema la mkutano ikafikia mwisho wake. Kwa maana wana wa Israeli waliendelea kufanya kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
33 Y trajeron el tabernáculo á Moisés, el tabernáculo y todos sus vasos; sus corchetes, sus tablas, sus barras, y sus columnas, y sus basas;
Nao wakaileta maskani kwa Musa, lile hema pamoja na vyombo vyake vyote, kulabu zake, viunzi vyake vya mbao, miti yake na nguzo zake na vikalio vyake,
34 Y la cubierta de pieles rojas de carneros, y la cubierta de pieles de tejones, y el velo del pabellón;
na kifuniko chake cha ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko chake cha ngozi za sili na pazia la kisitiri,
35 El arca del testimonio, y sus varas, y la cubierta;
na sanduku la ushuhuda na miti yake na kifuniko.
36 La mesa, todos sus vasos, y el pan de la proposición;
Wakaleta meza, vyombo vyake vyote, na ule mkate wa wonyesho,
37 El candelero limpio, sus candilejas, las lámparas que debían mantenerse en orden, y todos sus vasos, y el aceite para la luminaria;
kile kinara cha taa cha dhahabu safi, taa zake, ule mstari wa taa, na vyombo vyake vyote na yale mafuta ya kuangazia taa,
38 Y el altar de oro, y el aceite de la unción, y el perfume aromático, y el pabellón para la puerta del tabernáculo;
na madhabahu ya dhahabu na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba uliotiwa manukato na kile kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema,
39 El altar de metal, con su enrejado de metal, sus varas, y todos sus vasos; y la fuente, y su basa;
ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, miti yake na vyombo vyake vyote, ile beseni na kinara chake,
40 Las cortinas del atrio, y sus columnas, y sus basas, y el pabellón para la puerta del atrio, y sus cuerdas, y sus estacas, y todos los vasos del servicio del tabernáculo, del tabernáculo del testimonio;
Wakaleta mapazia ya ua, nguzo zake na vikalio vyake na kile kisitiri kwa ajili ya lango la ua, kamba zake za hema na misumari yake ya hema na vyombo vyote kwa ajili ya utumishi wa maskani, kwa ajili ya hema ya kukutania.
41 Las vestimentas del servicio para ministrar en el santuario, las sagradas vestiduras para Aarón el sacerdote, y las vestiduras de sus hijos, para ministrar en el sacerdocio.
Wakaleta yale mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika patakatifu, yale mavazi matakatifu kwa ajili ya Aruni kuhani na mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani.
42 En conformidad á todas las cosas que Jehová había mandado á Moisés, así hicieron los hijos de Israel toda la obra.
Kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa, hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyoufanya utumishi wote.
43 Y vió Moisés toda la obra, y he aquí que la habían hecho como Jehová había mandado; y bendíjolos.
Naye Musa akaiona ile kazi yote, na, tazama, walikuwa wameifanya kama vile Yahweh alivyokuwa ameamuru. Hivyo ndivyo walivyokuwa wamefanya. Basi Musa akawabariki.

< Éxodo 39 >