< 1 Crónicas 6 >

1 LOS hijos de Leví: Gersón, Coath, y Merari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
2 Los hijos de Coath: Amram, Ishar, Hebrón y Uzziel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
3 Los hijos de Amram: Aarón, Moisés, y Mariam. Los hijos de Aarón: Nadab, Abiú, Eleazar, é Ithamar.
Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
4 Eleazar engendró á Phinees, y Phinees engendró á Abisua:
Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
5 Y Abisua engendró á Bucci, y Bucci engendró á Uzzi;
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
6 Y Uzzi engendró á Zeraías, y Zeraías engendró á Meraioth;
Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
7 Y Meraioth engendró á Amarías, y Amarías engendró á Achîtob;
Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
8 Y Achîtob engendró á Sadoc, y Sadoc engendró á Achîmaas;
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
9 Y Achîmaas engendró á Azarías, y Azarías engendró á Johanan;
Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
10 Y Johanan engendró á Azarías, el que tuvo el sacerdocio en la casa que Salomón edificó en Jerusalem;
Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
11 Y Azarías engendró á Amarías, y Amarías engendró á Achîtob;
Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
12 Y Achîtob engendró á Sadoc, y Sadoc engendró á Sallum;
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
13 Y Sallum engendró á Hilcías, é Hilcías engendró á Azarías;
Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
14 Y Azarías engendró á Seraíah, y Seraíah engendró á Josadec.
Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
15 Y Josadec fué [cautivo] cuando Jehová trasportó á Judá y á Jerusalem por mano de Nabucodonosor.
Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
16 Los hijos de Leví: Gersón, Coath, y Merari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
17 Y estos son los nombres de los hijos de Gersón: Libni, y Simi.
Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
18 Los hijos de Coath: Amram, Ishar, Hebrón, y Uzziel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
19 Los hijos de Merari: Mahali, y Musi. Estas son las familias de Leví, según sus descendencias.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
20 Gersón: Libni su hijo, Joath su hijo, Zimma su hijo,
Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
21 Joab su hijo, Iddo su hijo, Zera su hijo, Jeothrai su hijo.
Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
22 Los hijos de Coath: Aminadab su hijo, Coré su hijo, Asir su hijo,
Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
23 Elcana su hijo, Abiasaph su hijo, Asir su hijo,
Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
24 Thahath su hijo, Uriel su hijo, Uzzia su hijo, y Saúl su hijo.
Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
25 Los hijos de Elcana: Amasai, Achîmoth, y Elcana.
Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
26 Los hijos de Elcana: Sophai su hijo, Nahath su hijo,
Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
27 Eliab su hijo, Jeroham su hijo, Elcana su hijo.
Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
28 Los hijos de Samuel: el primogénito Vasni, y Abías.
Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
29 Los hijos de Merari: Mahali, Libni su hijo, Simi su hijo, Uzza su hijo,
Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
30 Sima su hijo, Haggía su hijo, Assía su hijo.
Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
31 Y estos son á los que David dió cargo de las cosas de la música de la casa de Jehová, después que el arca tuvo reposo:
Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
32 Los cuales servían delante de la tienda del tabernáculo del testimonio en cantares, hasta que Salomón edificó la casa de Jehová en Jerusalem: después estuvieron en su ministerio según su costumbre.
Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
33 Estos pues con sus hijos asistían: de los hijos de Coath, Hemán cantor, hijo de Joel, hijo de Samuel;
Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
34 Hijo de Elcana, hijo de Jeroham, hijo de Eliel, hijo de Thoa;
mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
35 Hijo de Suph, hijo de Elcana, hijo Mahath, hijo de Amasai;
mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
36 Hijo de Elcana, hijo de Joel, hijo de Azarías, hijo de Sophonías;
mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
37 Hijo de Thahat, hijo de Asir, hijo de Abiasaph, hijo de Core;
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
38 Hijo de Ishar, hijo de Coath, hijo de Leví, hijo de Israel.
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
39 Y su hermano Asaph, el cual estaba á su mano derecha: Asaph, hijo de Berachîas, hijo de Sima;
na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
40 Hijo de Michâel, hijo de Baasías, hijo de Malchîas;
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
41 Hijo de Athanai, hijo de Zera, hijo de Adaia;
mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
42 Hijo de Ethán, hijo de Zimma, hijo de Simi;
mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
43 Hijo de Jahat, hijo de Gersón, hijo de Leví.
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
44 Mas los hijos de Merari sus hermanos estaban á la mano siniestra, [es á saber], Ethán hijo de Chîsi, hijo de Abdi, hijo de Maluch;
Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
45 Hijo de Hasabías, hijo de Amasías, hijo de Hilcías;
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
46 Hijo de Amasai, hijo de Bani, hijo de Semer;
mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
47 Hijo de Mahali, hijo de Musi, hijo de Merari, hijo de Leví.
mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
48 Y sus hermanos los Levitas fueron puestos sobre todo el ministerio del tabernáculo de la casa de Dios.
Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
49 Mas Aarón y sus hijos ofrecían perfume sobre el altar del holocausto, y sobre el altar del perfume, en toda la obra del lugar santísimo, y para hacer las expiaciones sobre Israel, conforme á todo lo que Moisés siervo de Dios había mandado.
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
50 Y los hijos de Aarón son estos: Eleazar su hijo, Phinees su hijo, Abisua su hijo;
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
51 Bucci su hijo, Uzzi su hijo, Zeraías su hijo;
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
52 Meraioth su hijo, Amarías su hijo, Achîtob su hijo;
Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
53 Sadoc su hijo, Achîmaas su hijo.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
54 Y estas son sus habitaciones, conforme á sus domicilios y sus términos, [las] de los hijos de Aarón por las familias de los Coathitas, porque de ellos fué la suerte:
Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
55 Les dieron pues á Hebrón en tierra de Judá, y sus ejidos alrededor de ella.
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
56 Mas el territorio de la ciudad y sus aldeas se dieron á Caleb, hijo de Jephone.
Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Y á los hijos de Aarón dieron las ciudades de Judá de acogimiento, [es á saber], á Hebrón, y á Libna con sus ejidos;
Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
58 A Jathir, y Esthemoa con sus ejidos, y á Hilem con sus ejidos, y á Debir con sus ejidos;
Hileni, Debiri,
59 A Asán con sus ejidos, y á Beth-semes con sus ejidos:
Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
60 Y de la tribu de Benjamín, á Geba con sus ejidos, y á Alemeth con sus ejidos, y á Anathoth con sus ejidos. Todas sus ciudades fueron trece ciudades, [repartidas] por sus linajes.
Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
61 A los hijos de Coath, que quedaron de su parentela, [dieron] diez ciudades de la media tribu de Manasés por suerte.
Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
62 Y á los hijos de Gersón, por sus linajes, [dieron] de la tribu de Issachâr, y de la tribu de Aser, y de la tribu de Nephtalí, y de la tribu de Manasés en Basán, trece ciudades.
Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Y á los hijos de Merari, por sus linajes, de la tribu de Rubén, y de la tribu de Gad, y de la tribu de Zabulón, [se dieron] por suerte doce ciudades.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
64 Y dieron los hijos de Israel á los Levitas ciudades con sus ejidos.
Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
65 Y dieron por suerte de la tribu de los hijos de Judá, y de la tribu de los hijos de Simeón, y de la tribu de los hijos de Benjamín, las ciudades que nombraron por sus nombres.
Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
66 Y á los linajes de los hijos de Coath [dieron] ciudades con sus términos de la tribu de Ephraim.
Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
67 Y diéronles las ciudades de acogimiento, á Sichêm con sus ejidos en el monte de Ephraim, y á Gezer con sus ejidos,
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
68 Y á Jocmeam con sus ejidos, y á Beth-oron con sus ejidos,
Yokmeamu, Beth-Horoni,
69 Y á Ajalón con sus ejidos, y á Gath-rimmón con sus ejidos.
Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
70 De la media tribu de Manasés, á Aner con sus ejidos, y á Bilam con sus ejidos, para los del linaje de los hijos de Coath que habían quedado.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
71 Y á los hijos de Gersón [dieron] de la familia de la media tribu de Manasés, á Golan en Basán con sus ejidos y á Astharoth con sus ejidos;
Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
72 Y de la tribu de Issachâr, á Cedes con sus ejidos, á Dobrath con sus ejidos,
Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
73 Y á Ramoth con sus ejidos, y á Anem con sus ejidos;
Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
74 Y de la tribu de Aser, á Masal con sus ejidos, y á Abdón con sus ejidos,
Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
75 Y á Ucoc con sus ejidos, y á Rehob con sus ejidos;
Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
76 Y de la tribu de Nephtalí, á Cedes en Galilea con sus ejidos, y á Ammón con sus ejidos, á Chîriath-jearim con sus ejidos.
Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
77 Y á los hijos de Merari que habían quedado, [dieron] de la tribu de Zabulón á Rimmono con sus ejidos, y á Thabor con sus ejidos;
Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
78 Y de la otra parte del Jordán de Jericó, al oriente del Jordán, [dieron], de la tribu de Rubén, á Beser en el desierto con sus ejidos; y á Jasa con sus ejidos,
Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
79 Y á Chêdemoth con sus ejidos, y á Mephaath con sus ejidos;
Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
80 Y de la tribu de Gad, á Ramot en Galaad con sus ejidos, y á Mahanaim con sus ejidos,
Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
81 Y á Hesbón con sus ejidos, y á Jacer con sus ejidos.
Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.

< 1 Crónicas 6 >