< Salmos 88 >

1 Jehová Dios de mi salud, día y noche clamo delante de ti.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
2 Entre delante de ti mi oración: inclina tu oído a mi clamor.
Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
3 Porque mi alma está harta de males: y mi vida ha llegado a la sepultura. (Sheol h7585)
Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
4 Soy contado con los que descienden al sepulcro: soy como hombre sin fuerza;
Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
5 Librado entre los muertos. Como los matados que duermen en el sepulcro: que no te acuerdas más de ellos, y que son cortados de tu mano.
Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
6 Hásme puesto en el hoyo profundo: en tinieblas, en honduras.
Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
7 Sobre mí se ha acostado tu ira: y con todas tus ondas me has afligido. (Selah)
Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
8 Has alejado de mí mis conocidos: hásme puesto a ellos por abominaciones: estoy encerrado, y no saldré.
Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
9 Mis ojos enfermaron a causa de mi aflicción: te he llamado, o! Jehová, cada día he extendido a ti mis manos.
nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
10 ¿Harás milagro a los muertos? ¿Levantarse han los muertos para alabarte? (Selah)
Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
11 ¿Será contada en el sepulcro tu misericordia? ¿tu verdad en la perdición?
Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
12 ¿Será conocida en las tinieblas tu maravilla? ¿y tu justicia en la tierra del olvido?
Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
13 Y yo a ti, o! Jehová, he clamado: y de mañana te previno mi oración.
Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
14 ¿Por qué, o! Jehová, desechas a mi alma? ¿ por qué escondes tu rostro de mí?
Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
15 Yo soy afligido y menesteroso: desde la mocedad he llevado tus temores, he estado medroso.
Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
16 Sobre mí han pasado tus iras; tus espantos me han cortado.
Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
17 Hánme rodeado como aguas de continuo: hánme cercado a una.
Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
18 Has alejado de mí el amigo y el compañero; y mis conocidos en las tinieblas.
Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

< Salmos 88 >