< Salmos 81 >

1 Cantád a Dios nuestra fortaleza: cantád con júbilo al Dios de Jacob.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Tomád la canción, y dad al adufe: a la arpa de alegría, con el salterio.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Tocád la trompeta en la nueva luna, en el día señalado: en el día de nuestra solemnidad.
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 Porque estatuto es de Israel: juicio del Dios de Jacob.
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 Por testimonio en José le ha constituido, cuando salió sobre la tierra de Egipto: donde oí lenguaje que no entendía.
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 Quité entonces su hombro de debajo de la carga: sus manos se quitaron de las ollas.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 En la angustia llamaste, y yo te libré; te respondí en el secreto del trueno; te probé sobre las aguas de Meriba. (Selah)
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Oye, pueblo mío, y protestarte he: Israel, si me oyeres;
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 No habrá en ti dios ajeno: ni te encorvarás a dios extraño.
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 Yo soy Jehová tu Dios, que te hice subir de la tierra de Egipto: ensancha tu boca, y henchirla he.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 Mas mi pueblo no oyó mi voz: e Israel no me quiso a mí.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 Y dejélos a la dureza de su corazón; caminaron en sus consejos.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 ¡O si mi pueblo me oyera, si Israel anduviera en mis caminos!
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 En nada derribara yo a sus enemigos: y volviera mi mano sobre sus adversarios.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 Los aborrecedores de Jehová le hubieran mentido: y el tiempo de ellos fuera para siempre.
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 Y Dios le hubiera mantenido de grosura de trigo: y de miel de la piedra te hubiera hartado.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”

< Salmos 81 >