< Salmos 76 >

1 Dios es conocido en Judá: Dios, en Israel es grande su nombre.
Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
2 Y en Salem está su tabernáculo: y su habitación en Sión.
Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
3 Allí quebró las saetas del arco: el escudo, y la espada, y la guerra. (Selah)
Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
4 Ilustre eres tú, y fuerte, más que los montes de caza.
Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
5 Los fuertes de corazón fueron despojados; durmieron su sueño, y nada hallaron en sus manos todos los varones fuertes.
Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
6 Por tu reprensión, o! Dios de Jacob, es adormecido el carro y el caballo.
Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
7 Tú eres terrible, tú: ¿y quién parará delante de ti en comenzando tu ira?
Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
8 Desde los cielos hiciste oír juicio: la tierra tuvo temor, y cesó,
Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
9 Cuando, o! Dios, te levantaste al juicio, para salvar a todos los mansos de la tierra. (Selah)
wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
10 Ciertamente la ira del hombre te confesará: los restos de las iras constreñirás.
Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
11 Prometéd, y pagád a Jehová, vuestro Dios, todos los que estáis al rededor de él: traigan presentes al terrible.
Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
12 El que quita el espíritu a los príncipes: terrible a los reyes de la tierra.
Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.

< Salmos 76 >