< Salmos 74 >

1 ¿Por qué o! Dios, nos has desechado para siempre? ¿ por qué ha humeado tu furor contra las ovejas de tu dehesa?
Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
2 Acuérdate de tu congregación, que adquiriste de tiempo antiguo: cuando redimiste la vara de tu heredad, este monte de Sión, donde has habitado.
Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
3 Levanta tus pies a los asolamientos eternos: a todo enemigo que ha hecho mal en el santuario.
Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
4 Tus enemigos han bramado en medio de tus sinagogas: han puesto en ellas sus señas, señas.
Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
5 Nombrado era, como si lo llevara al cielo, el que metía las hachas en el monte de la madera para el edificio del santuario.
Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
6 Y ahora con hachas y martillos han quebrado todas sus entalladuras.
Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
7 Han puesto a fuego tus santuarios, el tabernáculo de tu nombre han ensuciado en tierra.
Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
8 Dijeron en su corazón: Destruyámoslos de una vez: quemaron todas las sinagogas de Dios en la tierra.
Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
9 No vemos ya nuestras señales: no hay más profeta, ni hay con nosotros quien sepa: ¿hasta cuándo?
Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
10 ¿Hasta cuándo, o! Dios, nos afrentará el angustiador? ¿blasfemará el enemigo perpetuamente tu nombre?
Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
11 ¿Por qué retráes tu mano, y tu diestra la escondes dentro de tu seno?
Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
12 Y Dios ha sido mi rey de tiempo antiguo: el que obraba saludes en medio de la tierra.
Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
13 Tú hendiste la mar con tu fortaleza: quebrantaste cabezas de ballenas en las aguas.
Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
14 Tú magullaste las cabezas del leviatán: le diste por comida al pueblo de los desiertos.
Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
15 Tú abriste fuente y río: tú secaste ríos impetuosos.
Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
16 Tuyo es el día, tuya también es la noche: tú aparejaste la lumbre y el sol.
Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
17 Tú estableciste todos los términos de la tierra: el verano y el invierno tú los formaste.
Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
18 Acuérdate de esto, que el enemigo ha dicho afrentas a Jehová: y que el pueblo insensato ha blasfemado tu nombre.
Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
19 No entregues a las bestias el alma de tu tórtola: y no olvides para siempre la compañía de tus afligidos.
Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
20 Mira al concierto: porque las oscuridades de la tierra se han henchido de habitaciones de violencia.
Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
21 No vuelva avergonzado el abatido: el afligido y el menesteroso alabarán tu nombre.
Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
22 Levántate, o! Dios, pleitea tu pleito: acuérdate de tu injuria con que el insensato te injuria cada día.
Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
23 No olvides las voces de tus enemigos: el tropel de los que se levantan contra ti sube continuamente.
Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.

< Salmos 74 >