< Salmos 73 >

1 Ciertamente bueno es a Israel Dios, a los limpios de corazón.
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 Y yo, casi se apartaron mis pies; poco faltó, para que no resbalasen mis pasos.
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 Porque tuve envidia a los malvados, viendo la paz de los impíos.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 Porque no hay ataduras para su muerte: antes su fortaleza está entera.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 En el trabajo humano no están: ni son azotados con los hombres.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 Por tanto soberbia los corona: cúbrense de vestido de violencia.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 Sus ojos están salidos de gruesos: pasan los pensamientos de su corazón.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 Soltáronse, y hablan con maldad de hacer violencia: hablan de lo alto.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 Ponen en el cielo su boca: y su lengua pasea la tierra.
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 Por tanto su pueblo volverá aquí, que aguas en abundancia les son exprimidas.
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 Y dirán: ¿Cómo sabe Dios? ¿Y, si hay conocimiento en lo alto?
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 He aquí, estos impíos, y quietos del mundo alcanzaron riquezas:
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 Verdaderamente en vano he limpiado mi corazón: y he lavado mis manos en limpieza;
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 Y he sido azotado todo el día: y castigado por las mañanas.
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 Si decía: Contar lo he así: he aquí, habré negado la nación de tus hijos.
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 Pensaré pues para saber esto: es trabajo en mis ojos.
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 Hasta que venga al santuario de Dios; entonces entenderé la postrimería de ellos.
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 Ciertamente los has puesto en deslizaderos: hacerlos has caer en asolamientos.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 ¡Cómo han sido asolados! ¡cuán en un punto! Acabáronse: fenecieron con turbaciones.
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 Como sueño de el que despierta. Señor, cuando despertares, menospreciarás sus apariencias.
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 Ciertamente mi corazón se acedó: y en mis riñones sentía punzadas.
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 Mas yo era ignorante, y no entendía; era una bestia acerca de ti.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 Aunque yo siempre estaba contigo: y así echaste mano a mi mano derecha:
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 Guiásteme en tu consejo: y después me recibirás con gloria.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 ¿A quién tengo yo en los cielos? Y contigo nada quiero en la tierra.
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 Desmáyase mi carne y mi corazón, ¡o roca de mi corazón! que mi porción es Dios para siempre.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 Porque, he aquí, los que se alejan de ti, perecerán: tú cortas a todo aquel que rompe tu pacto.
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Y yo, el acercarme a Dios, me es el bien: he puesto en el Señor Jehová mi esperanza, para contar todas tus obras.
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.

< Salmos 73 >