< Salmos 73 >

1 Ciertamente bueno es a Israel Dios, a los limpios de corazón.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 Y yo, casi se apartaron mis pies; poco faltó, para que no resbalasen mis pasos.
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 Porque tuve envidia a los malvados, viendo la paz de los impíos.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Porque no hay ataduras para su muerte: antes su fortaleza está entera.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 En el trabajo humano no están: ni son azotados con los hombres.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Por tanto soberbia los corona: cúbrense de vestido de violencia.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Sus ojos están salidos de gruesos: pasan los pensamientos de su corazón.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Soltáronse, y hablan con maldad de hacer violencia: hablan de lo alto.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 Ponen en el cielo su boca: y su lengua pasea la tierra.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Por tanto su pueblo volverá aquí, que aguas en abundancia les son exprimidas.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 Y dirán: ¿Cómo sabe Dios? ¿Y, si hay conocimiento en lo alto?
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 He aquí, estos impíos, y quietos del mundo alcanzaron riquezas:
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Verdaderamente en vano he limpiado mi corazón: y he lavado mis manos en limpieza;
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 Y he sido azotado todo el día: y castigado por las mañanas.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 Si decía: Contar lo he así: he aquí, habré negado la nación de tus hijos.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 Pensaré pues para saber esto: es trabajo en mis ojos.
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 Hasta que venga al santuario de Dios; entonces entenderé la postrimería de ellos.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Ciertamente los has puesto en deslizaderos: hacerlos has caer en asolamientos.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 ¡Cómo han sido asolados! ¡cuán en un punto! Acabáronse: fenecieron con turbaciones.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 Como sueño de el que despierta. Señor, cuando despertares, menospreciarás sus apariencias.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 Ciertamente mi corazón se acedó: y en mis riñones sentía punzadas.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 Mas yo era ignorante, y no entendía; era una bestia acerca de ti.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Aunque yo siempre estaba contigo: y así echaste mano a mi mano derecha:
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 Guiásteme en tu consejo: y después me recibirás con gloria.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 ¿A quién tengo yo en los cielos? Y contigo nada quiero en la tierra.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 Desmáyase mi carne y mi corazón, ¡o roca de mi corazón! que mi porción es Dios para siempre.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 Porque, he aquí, los que se alejan de ti, perecerán: tú cortas a todo aquel que rompe tu pacto.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 Y yo, el acercarme a Dios, me es el bien: he puesto en el Señor Jehová mi esperanza, para contar todas tus obras.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Salmos 73 >