< Salmos 69 >

1 Sálvame, o! Dios, porque las aguas han entrado hasta el alma.
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
2 Estoy zabullido en cieno profundo, que no hay pie; soy venido en profundos de aguas, y la corriente me ha anegado.
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
3 He trabajado llamando; mi garganta se ha enronquecido; han desfallecido mis ojos de esperar a mi Dios.
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 Hánse aumentado más que los cabellos de mi cabeza los que me aborrecen sin causa; hánse fortalecido mis enemigos, los que me destruyen sin porqué: lo que no hurté, entonces lo volví.
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 Dios, tú sabes mi insensatez; y mis delitos no te son ocultos.
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 No sean avergonzados por mí, los que te esperan, Señor Jehová de los ejércitos; no sean confusos por mí los que te buscan, o! Dios de Israel.
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 Porque por ti he sufrido vergüenza; confusión ha cubierto mi rostro.
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 He sido extrañado de mis hermanos, y extraño a los hijos de mi madre.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 Porque el zelo de tu casa me comió, y los denuestos de los que te denuestan, cayeron sobre mí.
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 Y lloré con ayuno de mi alma, y esto me ha sido por afrenta.
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
11 Y puse saco por mi vestido, y fui a ellos por proverbio.
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 Hablaban contra mí los que se sentaban a la puerta, y en las canciones de los bebedores de sidra.
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 Y yo enderazaba mi oración a ti, o! Jehová, al tiempo de la buena voluntad: o! Dios, por la multitud de tu misericordia óyeme, por la verdad de tu salud.
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 Escápame del lodo, y no sea yo anegado; y sea yo librado de los que me aborrecen, y de los profundos de las aguas.
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 No me anegue el ímpetu de las aguas, ni me suerba la hondura, ni el pozo cierre sobre mí su boca.
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Oyeme, Jehová; porque benigna es tu misericordia: conforme a la multitud de tus miseraciones mira por mí.
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 Y no escondas tu rostro de tu siervo; porque estoy angustiado; apresúrate, óyeme.
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 Acércate a mi alma, redímela: por causa de mis enemigos líbrame.
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19 Tú sabes mi afrenta, y mi confusión, y mi vergüenza; delante de ti están todos mis enemigos.
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20 La afrenta ha quebrantado mi corazón; y he tenido dolor; y he esperado quien se compadeciese de mí, y no lo hubo, y consoladores, y no hallé.
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21 Y pusieron en mi comida hiel; y en mi sed me dieron a beber vinagre.
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22 Sea su mesa delante de ellos por lazo; y lo que es por paces, les sea por tropezón.
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23 Sean oscurecidos sus ojos para ver; y haz siempre titubear sus lomos.
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24 Derrama sobre ellos tu ira, y el furor de tu enojo les comprenda.
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25 Sea su palacio asolado; en sus tiendas no haya morador.
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 Porque persiguieron al que tú heriste: y cuentan del dolor de los que tú mataste.
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Pon maldad sobre su maldad, y no entren en tu justicia.
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 Sean raídos del libro de los vivientes: y no sean escritos con los justos.
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 Y yo afligido, y dolorido: tu salud, o! Dios, me defenderá.
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 Yo alabaré el nombre de Dios con canción; y magnificarle he con alabanza.
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 Y agradará a Jehová más que buey, y becerro, que echa cuernos y uñas.
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 Verán los humildes, y regocijarse han: buscád a Dios, y vivirá vuestro corazón.
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 Porque Jehová oye a los menesterosos, y no menosprecia a sus prisioneros.
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 Alábenle los cielos y la tierra, las mares y todo lo que se mueve en ellas.
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35 Porque Dios guardará a Sión, y reedificará las ciudades de Judá, y habitarán allí, y heredarla han.
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
36 Y la simiente de sus siervos la heredará; y los que aman su nombre habitarán en ella.
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.

< Salmos 69 >